Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Makamu wa Rais Azindua Jengo La Viongozi Mashuhuri Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali imejizatiti kuhakikisha Sekta ya Uchukuzi inaimarika ili kuliweka Taifa kwenye nafasi nzuri ya ushindani wa kibiashara, kuongeza mapato ya fedha za kigeni na kukuza mchango wa sekta hiyo katika pato la Taifa.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa uzinduzi wa Jengo la Viongozi Mashuhuri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Amesema pamoja na ujenzi wa jengo hilo, Serikali ya Awamu ya Sita imejipanga kikamilifu kuendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kisekta kama ilivyoainishwa katika Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2050, Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo ya Taifa na Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2025).


Makamu wa Rais amesisitiza kwamba, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu na huduma mbalimbali katika Viwanja vya Ndege, huduma za usafiri wa barabara, usafiri majini na usafiri kwa njia ya reli. Halikadhalika amesema, Serikali itaendelea na uboreshaji wa  huduma za Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) kwa lengo  kuboresha usafiri wa ndani, kuunganisha Tanzania na nchi nyingine, kupunguza gharama za usafirishaji na kuimarisha uchumi wa Tanzania na biashara za kimataifa.

Vilevile, Makamu wa Rais amesema ili kuboresha huduma za usafiri na usafirishaji, Serikali imedhamiria kuunganisha huduma za Sekta ya Uchukuzi, kama vile uunganishaji wa huduma za Viwanja vya Ndege,  usafiri wa barabara, maji na reli. Mathalan, mradi wa kimkakati unaoendelea wa ujenzi wa barabara za Mwendokasi (BRT) kati ya eneo la Posta na Gongo la Mboto utaunganishwa na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere ili kurahisisha huduma za usafiri katika jiji la Dar es Salaam.


Hali kadhalika, hatua za utekelezaji zinaendelea ili kuhakikisha huduma za reli zinaunganishwa na viwanja vya Ndege vya kimataifa, hususan Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro.

Aidha, Makamu wa Rais amesema Jitihada hizo kubwa zinazofanywa na Serikali zinalenga kurahisisha huduma za usafiri na usafirishaji ili kuchochea ukuaji wa uchumi kitaifa na kikanda. Ameongeza kwamba, hiyo inatokana na fursa na faida za kijiografia za Tanzania, ambayo ni lango kuu la biashara la nchi zaidi ya nane  zilizopo Kusini, Mashariki na Kati ya Bara la Afrika, na kiunganishi cha Bara la Afrika na nchi za Mashariki ya Kati na Mbali.


Makamu wa Rais amesema, dhamira ya Serikali ni kuendeleza utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati, ikiwemo, ujenzi wa reli ya kisasa  kwa vipande na maeneo yote yaliyobaki kuelekea Tabora, Mwanza na Kigoma hadi Musongati (Burundi), uboreshwaji wa Bandari ya Dar es Salaam na Bandari nyingine za kimkakati za Tanga, Mtwara, Kisiwa Mgao, Mbamba Bay, Kigoma na Bagamoyo, uboreshaji wa reli ya TAZARA, ujenzi na ukarabati wa barabara za lami zinazounganisha Tanzania na nchi za jirani.

Pia, Makamu wa Rais amesema uwekezaji wa Serikali katika Sekta ya Uchukuzi umeleta manufaa makubwa. Mathalan, mchango  wa Sekta ya Uchukuzi katika Pato la Taifa uliongezeka kutoka 7.2% (2023) hadi 7.5% (2024). Kasi ya ukuaji wa Sekta ya Uchukuzi iliongezeka kutoka 4.1% (2023) hadi 4.2% (2024) na katika kipindi cha hivi karibuni  ilikua kwa wastani wa 5.4%.

Makamu wa Rais ametoa rai kwa kwa Watanzania wote kutambua wajibu wa kuilinda na kuitunza miundombinu inayoendelea kuwekezwa na Serikali kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Kwa upande wake Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amesema Wizara itaendelea kuhakikisha miradi ya Viwanja vya Ndege nchini inaendelea kutekelezwa ili kuongeza huduma ya usafiri wa Anga na hivyo kufungua na kuchochea shughuli mbalimbali za kiuchumi nchini.

 

Amesema Serikali katika kuhakikisha inaendelea kuimarisha shughuli utalii, biashara na kilimo,Wizara kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania inaendelea na hatua za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ya viwanja vipya vya Serengeti, Kagera na Njombe na mara baada ya kukamilika itatafuta fedha kwaajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Awali akitoa taarifa ya mradi wa Jengo la Viongozi Mashuhuri, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Abdul Mombokaleo amesema mradi huo ni sehemu ya utakelezaji wa mpango mkakati wa Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi kuhusu uimarishaji wa Miundombinu na huduma za Viwanja vya Ndege.

Jengo la Viongozi Mashuhuri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, limejengwa mahsusi kwaajili ya kuhudumia wageni na Viongozi mashuhuri wa ndani na nje ya nchi. Jengo hilo ni hatua muhimu katika kuimarisha taswira ya Taifa na kuongeza hadhi ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere katika ngazi ya kimataifa.











 


Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...