Kanali Mtambi Awapa Somo Vijana Tarime

GEORGE MARATO TV
0

 


Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 16 Januari, 2026 amekuwa mgeni rasmi katika kikao cha vijana wa Wilaya ya Tarime kilichoandaliwa na Chifu wa Wakurya Koo ya Wakenye Mhe. Christopher Gachuma ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) kutoka Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika kikao hicho, Kanali Mtambi amewataka vijana wa Wilaya ya Tarime kubadilika kifikra na matendo ili kuweza kufaidi fursa mbalimbali zilizopo katika Wilaya ya Tarime na Mkoa wa Mara kwa jumla. 




Mhe. Mtambi amesema Mji wa Tarime na Mkoa wa Mara unafursa nyingi na kusipokuwa na amani na utulivu fursa hizo zitawafaidisha watu waliopo katika Mikoa mingine. 

Mhe. Mtambi pia amewasikiliza vijana na kupokea kero, changamoto na mapendekezo yao kuhusiana na utatuzi wa changamoto zinazowakabili. 





Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Chifu wa Watimbaru Ndugu Peter Zakaria na viongozi wengine katika jamii na kimefanyika katika ukumbi wa Hoteli ya CMG, Tarime.







Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top