Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Benki ya Dunia, Sadc Zampongeza Rais Samia Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo



📌 Dkt. Biteko asema nia njema ya Rais Samia iungwe mkono kuleta maendeleo kwa Watanzania

📌 Dkt. Biteko ampongeza Mbunge Kiswaga kwa Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini ikiwemo Wilaya ya Magu.

Amesema hayo leo Desemba 23, 2024 wilayani Magu mkoani Mwanza katika Mkutano Mkuu Maalum ambapo taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu Jimbo la Magu kwa mwaka 2020 hadi 2024 iliwasilishwa.


“Mhe. Rais amefanya kazi kubwa ya kupigiwa mfano na anastahili pongezi, nataka niwaambieni kuna watu wengine wanaumia tukimpongeza Rais Samia, lakini wajue hatutoi pongezi hizi peke yetu hata huko duniani kwa mfano Benki ya Dunia na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wanampongeza kwa ukuaji wa uchumi wa nchi yetu kwa asilimia 5.1,” amesema Dkt. Biteko.

Amesema pia kuwa Rais Samia ana nia njema na anataka kuona Watanzania wanapata maendeleo.

Ameongeza kuwa maendeleo katika Jimbo la Magu hayakuja kwa bahati mbaya isipokuwa kwa mipango na hivyo anawapongeza wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Magu kwa tamko la pongezi kwa Rais Samia kwa kuwapa fedha kiasi cha shilingi 143.9 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Ametaja baadhi ya miradi iliyotekelezwa na Serikali “ Barabara za lami zimeunganisha mikoa yote nchi nzima, tuna ndege za abiria na mizigo, tumejenga shule nyingi na sasa tunajenga shule za kata maeneo mbalimbali nchini. Maendeleo yanaonekana kwa macho na sisi ni kazi yetu kusema haya kwa wivu mkubwa,”

Kuhusu umeme Dkt. Biteko amesema katika kijiji kimoja pekee ambacho hakina umeme, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 600 kwa ajili ya kupeleka umeme huku mipango ya kupeleka umeme katika kisiwa ikiendelea.

Aidha, amempongeza Mbunge wa Jimbo la Magu, Mhe. Kiswaga kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo.


Dkt. Biteko amesema “CCM ni chama kiongozi hivyo wanaCCM tembeeni kifua mbele hubirini yanayofanywa na chama chenu waonesheni watu maendeleo yaliyotokea msiwapuuze,”

Pamoja na hayo amempongeza Mhe. Kiswaga kwa kusimamia miradi ya maendeleo huku akiwaasa wanachama wa CCM kushirikiana na viongozi kwa ngazi zote ili kuendelea kuimarisha chama huku akiwapongeza kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika Jimbo lao.

Mbunge wa Jimbo la Magu, Mhe. Boniventura Kiswaga wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu Jimbo la Magu kwa mwaka 2020 hadi 2024 amesema Serikali ya Rais Samia imeendelea kuwapa fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ikiwemo shilingi bilioni 78 kwa ajili ya ujenzi wa barabara na madaraja.

Amebainisha kuwa Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) wametoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 48 kwa ajili ya kujenga daraja la Simiyu.

“Kwenye sekta ya maji tumepokea shilingi bilioni 12 kwa ajili ya kujenga tanki lenye lita za ujazo milioni 5 litakalohudumia kata 14,” amesema Mhe. Kiswaga.

Amesema Rais Samia katika bajeti ya mwaka huu ametenga fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ikiwemo ya kutoa maji Ihale, kujenga tanki lenye ujazo wa lita milioni 2 pamoja na mradi wa kuchimba visima virefu.

Katika upande wa sekta ya elimu, amesema “Tumepokea fedha kiasi cha shilingi bilioni zaidi ya 31, tumemaliza ujenzi wa sekondari za kata sasa tunaendelea kujenga sekondari za vijiji nia yetu ni kumpelekea maendeleo kwa wananchi,”

Vilevile, katika afya wilaya hiyo imepokea shilingi bilioni 10 ambapo wamekarabati na kujenga vituo vipya vya afya.

Aidha, ameshukuru Rais Samia kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Jimbo lake.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda amepongeza Mhe. Kiswaga kwa kuandaa mkutano utakaotoa fursa kwa wananchi kuelezwa yale aliyotekeleza katika kuwaletea maendeleo.



“Kwa miaka mitatu Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan imeleta shilingi trilioni 5.6 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo hapa Magu,”

Mhe. Mtanda amesema baada ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, CCM Magu imeshinda katika vijiji 78 kati ya 82 na katika vitongoji 508, imeshinda vitongoji 484 huku akiwataka wananchi kudumisha amani mara baada ya uchaguzi huo.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Magu, Enos Kalambo amesema kuwa Rais Samia na Mbunge wao Kiswaga wamefanyakazi kubwa ya kuwaletea maendeleo katika wilaya hiyo hivyo wananchi waendelee kuwapa ushirikiano katika kutekeleza majukumu yao.







 

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...