Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Jinsi Mashine za Kusaga za Solar Zilivyo Suluhisho Mbadala wa Mashine za Mafuta Katika Gharama za Uendeshaji na Uhifadhi wa Mazingira



Na Emmanuel  Chibasa

Mashine za kusaga ni vifaa vinavyotumika kusaga na kukoboa nafaka Kwa ajili ya kupata chakula kutoka Katika mazao mbalimbali kama vile mahindi, mihogo, ulezi, mtama, mpunga pamoja na bidhaa nyingine za kilimo.

Kuna aina tofauti za mashine za kusaga nafaka ambazo pia zinatumia vyanzo tofauti vya uzalishaji wa umeme, ambazo ni mashine zinazotumia umeme wa gridi, mashine zinazotumia mafuta ya dizel pamoja na mashine zinazotumia nishati ya umeme jua yani Solar.

Katika maeneo ya vijijini bado kuna baadhi ya maeneo ambayo hayajafikiwa na umeme wa gridi, wananchi  wanatumia mashine za kusaga zinazotumia mafuta  zinaendeshwa kwa kutumia injini inayotumia mafuta ya diseli kama chanzo cha nguvu kuendesha mfumo wa magurudumu na gia zinazowezesha nafaka kukobolewa na kusagwa.

Katika makala yetu leo, George Marato Tv Tunaangazia huduma za kusaga nafaka kwa mashine zinazotumia mafuta ya disel kwa kuangalia changamoto za gharama za uendeshaji na uhifadhi wa mazingira lakini pia kuangalia matumizi ya teknolojia ya nishati ya jua yani Solar, inavyoweza kusaidia kutumika kama mbadala wa matumizi ya mashine za mafuta Katika maeneo ambayo hayajafikiwa na umeme wa gridi kama suluhisho la Kupunguza gharama za uendeshaji wa biashara hiyo pamoja uhifadhi wa Mazingira Kwa wananchi wa wilaya ya Musoma Mkoani mara.

Kisiwa cha Rukuba ni miongoni mwa visiwa vinavyopatikana Ziwa Victoria katika Wilaya ya Musoma mkoa wa Mara, ambapo kutokana na  eneo la ardhi sehemu kubwa kuzungukwa na maji, bado kisiwa hiki hakijafikiwa na huduma ya umeme wa gridi, hali inayopelekea wakazi wa eneo hilo, kutegemea nishati ya umeme jua pamoja na jenereta zinazotumia mafuta kupata huduma ya umeme kupata mwanga pamoja na Kuendesha shughuli mbalimbali za ujasiliamali zinazotegemea nishati ya umeme Ikiwa ni pamoja na matumizi ya mashine za kusaga nafaka zinazotumia mafuta ya disel ambazo zinatajwa kuwa na changamoto za gharama za uendeshaji na uchafuzi wa mazingira.

Licha ya mashine za kusaga zinazotumia mafuta ya disel kutajwa  kuwa na changamoto ya gharama katika uendeshaji pamoja na wataalam wa maswala ya Mazingira kueleza kuwa zinachafua pia mazingira kutokana na moshi wa mafuta  wakati wa kusaga, lakini baadhi ya watumiaji wa mashine hizo wanasema pia kuna faida zake ikiwa ni pamoja na kupatikana kwa urahisi hususani katika maeneo yasiyo na umeme wa gridi kama vile maeneo ya visiwa.

Mbali na faida hizi lakini watumiaji wa mashine hizi pia wanasema zipo changamoto kadhaa zinazowakabili kama vile, gharama kubwa za uendeshaji kwa bei ya mafuta ya disel kuzidi kuongezeka hasa maeneo ya vijijini, ambapo hakuna vituo vya kuuza mafuta kama ilivyo maeneo ya mjini, gharama za matengenezo ambapo Injini zinahitaji kubadilisha mafuta, vipuri, na mara nyingine kuitaji matengenezo makubwa lakini hakuna maduka yanayouza Vifaa Katika maeneo Yao.

Jumanne Milunda, mkazi wa kisiwa cha Rukuba, anayejishughulisha na biashara ya mashine ya kusaga inayotumia mafuta ya disel kwa miaka muda sasa, anasema kutokana na kukosekana kwa umeme wa gridi katika kisiwa hicho wakazi wa eneo hilo utegemea mashine hiyo ya kusaga inayotumia disel kusaga nafaka kwa ajili ya chakula.

“Nimewekeza kwenye biashara hii ya mashine ya kusaga inayotumia mafuta kutoka na huku hakuna Huduma ya umeme wa Tanesco au ule wa REA, lakini changamoto ni kubwa. Mafuta ni ghali sana, tunalazimika kuyasafirisha kutoka mji wa Musoma kwa boti hiyo pia ni gharama tutatumia Katika Biashara hii Kila siku na inamaana mafuta yakikosa basi huduma nayo inasimama.

Muda mwingine mashine inaharibika na huku tulipo hakuna duka la vifaa hivyo inakubidi uagize huko mjini, jambo linalolazimu kusimamisha biashara kwa siku kadhaa na Kwa kweli, kama Teknolojia hiyo ipo basi watuletee  sababu itakua mbadala wa kutusaidia Katika gharama za uendeshaji  na wakazi watapata Huduma Kwa  bei nafuu na rahisi zaidi.” Amesema Milunda

Naye Bwire Mkama mfanyabiashara ya mashine Musoma anasema awali alikua anatumia mashine ya kusaga inayotumia mafuta ya disel na kero aliyokua anaipata ni namna ya kuiwasha mashine hiyo Pindi anapopata wateja.

"Kero kubwa niliyokua naipata ni wakati wa kuwasha mashine unatumia nguvu kubwa kuzungusha Kwa mkono  handle mpaka mashine ikubali kuwaka unakua umetumia nguvu sana, Sasa Ile kuwasha mara Kwa mara inachosha sababu sio kama zile za umeme unabonyeza tu swichi mashine inawaka na unabonyeza sehemu ya kuzima inazima

Pia mashine hizo uwezi kusaga nafaka kigodo kama ilivyo hizi zinatumia umeme mtu anaweza kuja na hata kilo mbili ukamsagia lakini Ile ya mafuta ukisaga kama hivi unajikuta unapata hasara kwenye mafuta, zile zinahitaji upate wateja wengi ufanye Kazi Kwa mara moja ndio utaiona faida"Amesema Bwire

Kwa upande chausiku Mgeta mama wa familia na mkazi wa kisiwa hicho anasema hawana njia nyingine mbadala ambayo inawawezesha kusaga nafaka zao ili kupata unga kama ilivyo maeneo ya mjini ukinunua mahindi au udaga kwenye mshine haulipi tena hela ya kusaga kwa sababu mashine ni nyingi na zinatumia umeme lakini huku kwetu kutokana na mashine kuwa chache na zinatumia mafuta kwa debe moja tunasaga kwa kuanzia Shilingi 1000 hadi 1500.

Changamoto hii inayompata Jumanne Milunda na aliyopitia Bwire Mkama pia inawapata watoa huduma wengine katika maeneo ya vijijini katika maeneo ambayo hayajafikiwa na umeme wa gridi, lakini wakipatiwa elimu ya matumizi ya teknolojia ya mashine za kusaga zinazotumia nishati ya umeme jua itakua suhulisho Katika kuondokana na Changamoto hizo katika kutoa huduma Kwa Wananchi.

Mashine za kusaga zinazotumia nishati ya jua zinatajwa kuchukua nafasi kama suluhisho endelevu katika kupunguza gharama za uendeshaji na rafiki kwa mazingira sababu zinatumia paneli za jua kukusanya nishati, ambayo inahifadhiwa kwenye betri au kutumika moja kwa moja kuendesha mashine bila Kutoa moshi unaochafua hewa

Faida kubwa zinazotajwa na wataalam wa nishati ya umeme jua katika matumizi ya mashine ya kusaga inayotumia solar, ni pamoja na kutumia gharama nafuu za uendeshaji ambapo mtumiaji atakua hana haja ya kununua mafuta mara kwa mara ili kutoa huduma hiyo kwa wateja wake, mashine hizo hazitoi moshi wala kelele, ni rafiki kwa maeneo ya mbali ambayo hayahitaji miundombinu ya umeme wa gridi, hivyo yanafaa vijijini lakini pia nishati ya jua ni ya bure na inapatikana kwa urahisi.

Innocent Mwita ni mtaalam wa nishati mbadala anasema kuna faida kubwa kwa watoa huduma wa mashine za kusaga nafaka na bidhaa nyingine za kilimo katika kuwekeza hasa katika maeneo ya vijijini ambayo hayajafikiwa pia na umeme wa gridi 

  "Mashine hizi zinatoa fursa kwa wajasiriamali wa vijijini kuwekeza katika biashara ya kusaga nafaka kwa gharama ndogo, wafanyabiashara wa vijijini wakiwekeza katika teknolojia hii wataona jinsi teknolojia hii ilivyo suluhisho katika kuwasaidia l kupunguza gharama za uendeshaji na kuongeza faida.

Pia anatoa wito kwa serikali kuweka mazingira wezeshi kwa uwekezaji wa nishati ya jua kwa kuendelea kutoa  ruzuku kwa mashine hizi, kuweka sera bora za nishati mbadala, na kutoa elimu kwa wananchi. Ikiwa tutafanya hivi, tunaweza kusaidia vijiji kama Rukuba kupunguza umasikini na kuboresha maisha ya watu." Amesema Mwita.

Mkurugenzi wa teknolojia ya nishati jadidifu wa wakala wa nishati vijijini(REA) Mhandisi Advera Mwijage akiwa mkoani Kagera tarehe 7 Novemba 2024, alisema kuwa serikali imetenga shilingi bilioni 8 kupitia kwa wakala wa nishati vijiji(REA) kwa ajili ya kusambaza umeme ndani ya visiwa 118 vilivyopo maeneo mbalimbali nchi nzima.

“Serikali imetenga fedha hizo ili kuwafikishia wananchi wote wanaoishi maeneo ya visiwa na yale ambayo sio rafiki kufikiwa na gridi ya taifa na ilisaini mkataba na benki ya dunia ili kuwezesha upatikanaji wa nishati ambayo ni salama kwa Tanzania.” Alisema Advera

Serikali inatekeleza Mpango Mkuu wa Nishati Vijijini (REMP) 2022/23 hadi 2029/30 ambao unasaidia utekelezaji wa lengo la Tanzania la kupanua upatikanaji wa huduma za nishati za kisasa katika maeneo ya vijijini, sambamba na Lengo namba 7 la Maendeleo Endelevu (SDG 7) na Ajenda ya Utekelezaji wa Serikali ya SE4All (Nishati kwa Wote).

Wakati mashine za kusaga za disel zimekuwa nguzo muhimu kwa jamii za vijijini ambapo umeme wa gridi haujafika, changamoto zake zinafanya matumizi ya mashine za solar kuwa suluhisho bora. Uwekezaji wa serikali, mashirika binafsi, na wajasiriamali katika teknolojia ya nishati ya jua ni hatua muhimu kuelekea maendeleo endelevu na kupunguza umasikini kwa jamii ambazo hazijafikiwa na miundombinu ya umeme wa gridi.















Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...