Juliana Masaburi ampongeza Rais Dkt.Samia kwa uwekezaji wa zaidi ya shilingi billioni 400 katika bandari ya mtwara

GEORGE MARATO TV
0

 


Mbunge wa Viti Maalum(Vijana Taifa) Mhe. Juliana Masaburi amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji wa miundombinu ya zaidi ya shilingi Bilioni 400 katika Bandari ya Mtwara.

Akizungumza wakati wa kutembelea bandari hiyo,Juliana amesema kuwa uwekezaji huo utachochea Maendeleo ya kiuchumi katika mkoa wa Mtwara na Taifa kwa ujumla.

Aidha Mhe. Juliana Masaburi amempongeza Meneja wa Bandari ya Mtwara, Ndugu Fernand Nyati kwa kusimamia vyema Bandari ya Mtwara na kujipanga vyema kwa maandalizi ya kusafirisha Korosho kwa kupokea Meli zaidi ya 3 zenye makasha ya kusafirisha Korosho hizo.

Katika ziara hiyo,Mhe.Juliana aliambatana baraza la umoja wa vijana wa chama chamapinduzi (UVCCM)Mkoa Mtwara ambapo Mwenyekiti wa umoja huo,Komredi Abuu Athumani amesema kuwa wameamua kumleta Mgeni, Mhe. Juliana Masaburi kutembelea Bandari ya Mtwara ili aone uwekezaji wa Serikali na Baraza la Vijana lipate la kujifunza kupitia Bandari hiyo.

Mbunge Juliana Didas Masaburi ameenda Mtwara kwa ajili ya kushiriki Kikao cha Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mtwara kilichofanyika 05 Oktoba, 2024 katika Ukumbi wa Bandari ya Mtwara

Aidha, Mhe. Juliana Masaburi akiwa katika Kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Mtwara ametoa kiasi cha shilingi Milioni Moja (1,000,000) na Matofali 1000 kwaajili ya ujenzi wa nyumba ya Katibu wa UVCCM Mkoa wa Mtwara na pia, amegawa vyeti vya pongezi kwa wadau wa UVCCM Mkoa wa Mtwara.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top