Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa jana Agosti 21, 2024 alikuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Kizimkazi lililolenga kukuza Utalii Zanzibar, ambalo lilifanyika katika uwanja wa Shekha Dimbani, Zanzibar.
Akizungumza katika Tamasha hilo Mheshimiwa Majaliwa aliwasihi Watanzania waendelee kushirikiana, kuimarisha utamaduni na kujenga taifa lenye maendeleo na umoja.Aidha, aliwapongeza Dkt Samia Suluhu Hassan na Rais Dkt Hussein Mwinyi kwa juhudi kubwa za kukuza utalii nchini.


