Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu Amuaga Mkurugenzi Mkazi wa Benki Ya Dunia Kanda ya Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe


▪️Apongeza mchango wake katika maendeleo nchini.

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Mei 17, 2026 ameshiriki katika hafla ya kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Kanda ya Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, Nathan Belete, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Mwigulu alimpongeza Nathan kwa mchango wake mkubwa katika kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Benki ya Dunia pamoja na kuunga mkono juhudi za maendeleo katika sekta mbalimbali nchini.



Amesema kuwa imeshuhudiwa ongezeko kubwa na la kihistoria la ushirikiano kati ya Tanzania na Benki ya Dunia, ambapo takribani dola za Marekani bilioni 4.27 zilipatikana kupitia miradi na programu mbalimbali.

“Niruhusuni kwa mara nyingine kutoa shukrani zangu za dhati kwa Nathan kwa huduma yake ya kujitolea na mchango wake mkubwa katika safari ya maendeleo ya Tanzania, na kumtakia mafanikio mema katika majukumu yake mapya,” amesema Dkt. Mwigulu.


Aliongeza kuwa mchango wa Nathan katika kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Benki ya Dunia utaendelea kukumbukwa na kuthaminiwa.

“Mchango wako katika safari ya maendeleo ya Tanzania pamoja na kuimarisha ushirikiano wetu na Benki ya Dunia utaendelea kukumbukwa na kuthaminiwa daima. Nakushukuru sana,” amesema.

Kwa upande wake, Nathan Belete amesema anajivunia kazi iliyofanyika nchini Tanzania katika kipindi chake cha utumishi na kueleza kuwa ana matumaini makubwa kuhusu mustakabali wa maendeleo ya nchi.

“Ninajivunia kazi ambayo tumeifanya nchini Tanzania. Ninajivunia mustakabali wa programu yetu hapa nchini. Ninaamini kuna fursa kubwa na za kipekee sana,” amesema Nathan.


Aidha, Amempongeza Dkt. Mwigulu kwa nia yake ya dhati ya kuiona Tanzania ikipiga hatua za kimaendeleo kutokana na jitihada zake kubwa za kufuatilia fedha za bajeti kutoka kwa washirika wa maendeleo.

“Mheshimiwa Waziri wa Fedha wakati huo, ambaye sasa ni Waziri Mkuu, alisema, tunahitaji kusukuma mageuzi. Ili nchi hii ikue na kubadilika, lazima tusukume mageuzi. Lakini huwezi kunipa fedha za kiwango cha kununua chapati ili kufanya mageuzi makubwa, na kwasasa fedha za bajeti kutoka benki ya dunia imekua kutoka dola za marekani milioni 250 hadi Dola Milioni 750”

Aidha, amesema Tanzania ina nafasi kubwa ya maendeleo ikilinganishwa na mataifa mengi barani Afrika kutokana na rasilimali na fursa zilizopo.

“Kama Mwafrika, huenda sipaswi kusema kwamba Tanzania ina uwezo mkubwa zaidi kuliko nchi nyingine, hata kuliko nchi yangu mwenyewe. Lakini kwa kweli naamini kuwa Tanzania ina uwezo mkubwa zaidi kuliko nchi nyingi nyingine,” amesema.

Naye, Naibu Wazara wa Fedha Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemshukuru Nathan kwa utumishi wake uliotukuka na mchango wake mkubwa katika kuunga mkono juhudi za maendeleo ya Tanzania.

Kadhalika, amemuhakikishia Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia ajaye kuwa Wizara ya Fedha itafanya kazi kwa karibu naye katika kuendeleza vipaumbele vya maendeleo nchini hasa katika kipindi ambacho Tanzania inatekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Tanzania 2050

Kwa Upande wake Waziri wa Ujenzi Abdalah Ulega amemshukuru Nathan kwa kusaidia utekekezaji wa miradi mbalimbali katika ya ujenzi nchini.

“Nathan hukuwa tu mwakilishi wa Benki ya Dunia, bali rafiki wa kweli wa matarajio yetu ya maendeleo. utaalam wako ulithaminiwa na imani yako katika maendeleo ya Tanzania iligusa mioyo ya wengi, Tanzania itaendelea itakukumbuka”

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Caroline Nombo amesema Nathan ameacha alama kubwa katika maendeleo ya sekta ya elimu nchini kupitia programu mbalimbali zilizofadhiliwa na Benki ya Dunia.

“Tunatoa pongezi na shukrani zetu za dhati kwako, ndugu yetu Nathan, kwa huduma yako ya kujitolea kwa nchi yetu na hasa kwa sekta yetu. Uongozi wako, kujitolea kwako na ushirikiano wako umechangia kwa kiasi kikubwa safari ya maendeleo ya elimu nchini Tanzania, hususan katika mageuzi na maboresho yanayoendelea,” amesema Prof. Nombo.

Ameeleza kuwa kupitia programu ya SEQUIP, zaidi ya wasichana 10,000 waliokuwa katika hatari ya kukosa elimu wamewezeshwa kuendelea na masomo yao na kutimiza ndoto zao za kielimu.

“Kupitia mwongozo wako, ushirikiano kati ya nchi yetu na Benki ya Dunia umewezesha kufikisha matokeo yenye maana katika sekta ya elimu kwa mamilioni ya watoto wa Kitanzania,” ameongeza.

Naye Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Bi. Sauda Msemo amesema ushirikiano kati ya Tanzania na Benki ya Dunia umekuwa na mchango mkubwa katika mageuzi ya sekta ya fedha nchini.

Amesema ushirikiano huo umechangia kuimarisha uwezo wa taasisi za kifedha, kukuza ujumuishwaji wa kifedha pamoja na kuongeza uimara na ufanisi wa mfumo wa fedha nchini.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...