Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

HESLB yatilia mkazo PPP kutanua wigo wa ufadhili wa wanafunzi


Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga

Elimu ni gharama. Elimu ina mahitaji mengi ambayo yanahitaji fedha ili kuyakamilisha ili kupata utulivu wa kujifunza darasani. Serikali inasimamia na kutekeleza kikamilifu Sera ya Elimumsingi Bila Ada ambapo hutumia fedha nyingi kuwezesha upatikanaji wa mahitaji muhimu shuleni ili shughuli za ufundishaji na ujifunzaji ziweze kufanyika vizuri na kuwapunguzia mzigo wazazi na walezi gharama za kusomesha watoto wao.

Kupitia Sera ya Elimumsingi Bila Ada, fedha zinawafikia walengwa ipasavyo. Serikali hutuma fedha moja kwa moja katika akaunti za benki za shule ili zigharimie masuala mbalimbali ya kuendesha shule kama vile shughuli za utawala, taaluma, mitihani, ukarabati, michezo na mahitaji mengine kadha wa kadha. Sambamba na hilo, serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inatoa ufadhili kwa wanafunzi wanaosoma Stashahada kwa kozi za kipaumbele, Shahada ya kwanza na kuendelea katika kozi mbalimbali ili kwa pamoja vijana wa Kitanzania waweze kupata haki yao ya msingi ya elimu.

Kutokana na maboresho makubwa yaliyofanywa na serikali katika shule za msingi na sekondari, hasa uboreshaji na ujenzi wa miundombinu ya kujifunza pamoja na uwepo wa walimu mahiri, idadi ya wanafunzi wanaojiunga na vyuo vya kati na taasisi za elimu ya juu imeongezeka sana huku wengi wakiwa na sifa ya kupata mikopo hiyo. Ikumbukwe kuwa kadri idadi ya waombaji mikopo inavyoongezeka ndivyo mahitaji ya fedha za mikopo yanavyoongezeka pia. Ili kuendana na ongezeko la wanafunzi wanaojiunga vyuo vya kati na juu, HESLB imechukua hatua ya kuunganisha nguvu kati ya sekta ya umma na binafsi (Public and Private Partnership - PPP) ili kutafuta vyanzo vingine vya fedha au wafadhili nje na serikali kuhakikisha wanafunzi wenye sifa wanapata mikopo hiyo.

Katikati ya mahitaji makubwa ya fedha ya kugharamia elimu ya kati na ya juu, PPP haikwepeki, ni muhimu sana. Kimsingi, HESLB imeanzisha mashirikiano na taasisi za umma na binafsi zenye uwezo wa kufadhili wanafunzi ili wanafunzi wengi zaidi wapate mikopo. Lengo ni baadhi ya wanafunzi kupata mikopo kupitia HESLB na wengine wapate kupitia taasisi nyingine zenye kutoa ufadhili wa elimu, ili hatimaye kuwepo na kundi kubwa linalonufaika na ufadhili kukidhi mahitaji yaliyopo.

Mnamo Oktoba 2025, HESLB ilisaini makubaliano na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) ambapo NCAA imetoa ufadhili kwa wanafunzi wanaodahiliwa vyuoni kutoka jamii zinazozunguka Hifadhi ya Ngorongoro. Kamishna Mkuu wa NCAA, Abdul-Razaq Badru amesema "Tutaanza kwa kuwafadhili jumla ya wanafunzi 50 watakaodahiliwa kwenye fani za Sayansi ya Anga, Mali Kale na Akiolojia pamoja na Uhifadhi wa Wanyamapori."

Januari 29, 2026, Mkurugenzi  Mtendaji wa HESLB, Dk. Bill Kiwia, alifanya ziara Jijini Arusha kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Compassion International Tanzania (CIT) ikiwa ni jitihada za HESLB kuongeza vyanzo mbadala vya ufadhili (alternative financing). Katika ziara hiyo, HESLB na CIT walisaini tamko la nia ya kushirikiana (Statement of Intention to Collaborate) ili kuwatambua wanafunzi wanaotoka mazingira magumu ili wapate kipaumbele katika upangaji wa mikopo. Jambo hili ni jema sana.

Kama hiyo haitoshi, Machi 26, 2026, HESLB ilifanya kikaokazi na taasisi 205 zilizosajiliwa na HESLB na zinazotoa ufadhili wa wanafunzi kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kwani taasisi hizo zina mchango mkubwa katika kutanua wigo wa wanufaika wa mikopo ya elimu nchini. Kikaokazi hicho kilifanyika katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) Jijini Arusha. Pamoja na mambo mengine, Dk. Kiwia amesema kikao hicho ni muhimu na kina lengo la kuboresha ufanisi wa utendajikazi na kuongeza wigo wa wanafunzi wanaofadhiliwa na taasisi hizo huku akiishukuru serikali kwa kutoa shilingi trilioni 3.6 kugharamia mikopo ya elimu katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Kwa kumalizia, ni vyema watu binafsi, taasisi za dini na mashirika mbalimbali wajitokeze kuiunga mkono HESLB kufadhili wanafunzi ili wanafunzi wengi zaidi wapate mikopo badala ya kuiachia serikali pekee jukumu la kutoa mikopo ya elimu ya kati na juu. Nakumbuka Machi 14, 2026, HESLB iliandaa futari maalum katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam. Katika futari hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya HESLB, Prof. Hamisi Dihenga, alitoa wito kwa wadau kujitokeza kutoa ufadhili wa masomo (Scholarship). 

"Nia yetu ni kuendelea kumsaidia Mheshimiwa Rais katika juhudi za kuimarisha elimu ya juu nchini. Tupo tayari kushirikiana na wadau wengine kama ambavyo kumeshakubaliana na NCAA ambao wao watafadhili wanafunzi 50 wa vyuo vikuu, tunaomba wadau wengine pia wajitokeze tuwasaidie vijana wetu," amesema Prof. Dihenga. Kiukweli, ongezeko kubwa la wanafunzi vyuoni, linahitaji PPP kuweza kukidhi mahitaji makubwa ya fedha yaliyopo kugharamia masomo. Wadau jitokezeni, bila hivyo hatutoboi aisee.






Maoni: 0620 800 462.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...