Machi 07, 2026
*Mkuu wa Majeshi asema: Hakuna jambo la fidia
*Aibua nderemo, shangwe kwa wananchi
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ametoa majibu ya mgogoro wa ardhi baina ya wakazi wa Wilaya ya Monduli na Jeshi la Wananchi ambao wamedumu tangu 2004 baada ya kumpigia simu Mkuu wa Majeshi nchini na kumweleza kilio cha wanaMonduli.
Waziri Mkuu alichukua hatua hiyo jana jioni (Ijumaa, Machi 6, 2026) wakati. na wananchi na viongozi mbalimbali kwenye mkutano wa hadhara ambao katika uwanja wa Barafu Mto wa Mbu, wilayani Monduli, mkoani Arusha.
Akitoa majibu baada ya maongezi yao, Dkt. Mwigulueleza wananchi hao kwamba Mkuu wa Majeshi nchini ameridhia hoja yao ndiyo Mbunge wa Monduli, Isack Joseph pamoja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Namelok Sokoine ambao waliomba suala la fidia lisiwepo bali wananchi waachiwe kuendelea na jeshi kama ilivyokuwa zamani.
“Mkuu wa Majeshi ameridhia kwamba hakuna jambo la fidia. Makubaliano mliyokuwa nayo awali ya mafunzo na malisho yaendelee vilevile.
Waziri Mkuu alitoa rai kwa watendaji wa Halmashauri akiwataka waheshimu na kulinda maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya malisho ya mifugo ili kuepusha rasilimali na kufanya shughuli za ufugaji zinaendelea kwa tija. "Maeneo yanayohusu wafugaji tusiyadokoe, tusiyachanganye. Tuendelee kulinda maeneo ya wafugaji bila kuyachanganya na matumizi mengine."
Mapema, Mbunge wa Monduli, Isack Joseph alimuomba Waziri Mkuu afuatilie suala hilo ili wanaotaka kumiliki eneo hilo kwa kudai fidia, wasipatiwe fursa hiyo bali libakishwe kuwa eneo huru kwa Jeshi la Wananchi na kwa wapo. Eneo hilo lina kilometa za mraba 870 ambazo ni sawa na ekari 214,981.68
Pia alimuomba afuatilie suala la malipo ya mabomba ya maji kwenye kiwanda cha Pipes Industries ambacho kinatengeneza mabomba kwa ajili ya mradi wa maji wa vijiji 13 vya Monduli wenye thamani ya sh. pesa 20.3. Mradi huo unatarajiwa kutoa umbali wa km. 45 kutoka Ngaramtoni hadi Monduli mjini.
Vilevile, mbunge huyo alieleza changamoto zinazoikabili sekta ya utalii katika eneo la Mto wa Mbu kwamba licha ya kuwa eneo hilo lina vivutio vikubwa vya utalii, bado linasimamiwa kama Game Controlled Area, jambo linalosababisha watalii wengi kukwepa kulitembelea na hivyo kudhoofisha uchumi wa wilaya hiyo.
Naye, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Namelok Sokoine akisisitiza kuhusu eneo hilo alisema anakubaliana na maelezo ya Mbunge wake, Bw. Isack Joseph kwa vile anatambua kuwa wafugaji mbadala zaidi ya mifugo yao. "Kitu pekee ambacho wazazi wetu wanaweza kutuachia kama urithi wa ardhi yetu," alisema.
Alisema kwamba marehemu baba yake (hayati Edward Moringe Sokoine) alitambua umuhimu wa ardhi na malisho ndipo aliamua kutenga eneo la jeshi kufanyia mafunzo lakini pia ambalo wafugaji wangeweza kulilisha mifugo yao pale. “Nia yake kubwa ni maeneo yale yasiweze kuuzwa kwa watu wengine, njia pekeee ilikua ni kuwapa jeshi walitumie mafunzo lakini pia wafugaji walitumie wakati hakuna mafunzo.”
Alisema kuwa mwaka jana kupitia mbunge wao mstaafu, Fredrick Lowassa, walikuwa na vikao na Waziri wa Ulinzi kuhusu suala hilo na wakaazimia kuwa hawako tayari kufidiwa kwa kuwa hawana mahali pengine pa kwenda.
“Sisi wafugaji hatuna pa kupeleka ardhi mifugo yetu.
Mwisho




