Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM-Taifa, Mhe. Stephen Wasira, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), aliyefika kujitambulisha katika Ofisi za CCM, Lumumba, Jijini Dar es Salaam, baada ya hivi karibuni kuteuliwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hasssan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.




