Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amekagua mradi wa ujenzi wa barabara kipande cha Mbulu – Garbabi (km 25), ambacho ni sehemu ya barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa (km 389) inayojengwa kwa kiwango cha lami.
Mradi huo unaotekelezwa na Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) unalenga kuboresha mawasiliano ya barabara, kuimarisha usafirishaji wa watu na bidhaa, na kuchochea ukuaji wa uchumi katika maeneo husika.
Hadi sasa, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 41.7, ambapo jumla ya shilingi bilioni 36.3 zitatumika kukamilisha ujenzi. Mpaka sasa malipo ya shilingi bilioni 12.5 tayari yameshafanyika.




