Prof. Mkumbo amesisitiza kuwa katika kutekeleza Dira 2050, Tanzania inalenga kuwa na uchumi unaotegemea maarifa na ushindani wa kimataifa. Ili kufikia lengo hilo amewahimiza wawekezaji wa China kutotumia mtaji pekee, bali kuleta ujuzi wa mifumo ya kisasa ya teknologia.



