Rais Samia Aagiza Uwazi Manunuzi ya Umma, Asisitiza Uwajibikaji

GEORGE MARATO TV
0


Rais Samia Suluhu Hassan ameagiza kuimarishwa kwa uwazi na uwajibikaji katika manunuzi ya umma, akielekeza taasisi zinazokiuka taratibu kutajwa hadharani na kuchukuliwa hatua.

Akizungumza tarehe 30 Machi, 2026, Ikulu Dar es Salaam, wakati wa kupokea Taarifa ya Mwaka ya Tathmini ya Utendaji wa Ununuzi wa Umma, Rais Samia amesema sehemu kubwa ya fedha za Serikali hutumika katika manunuzi ya umma, hivyo usimamizi madhubuti ni muhimu kulinda rasilimali za wananchi.

“Ripoti zijazo zitaje wazi taasisi zinazofanya vibaya na zinazofanya vizuri, ili kuongeza uwajibikaji na kuchukua hatua stahiki,” amesema Rais Samia.

Amesema hatua hiyo inalenga kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha za umma na kuhakikisha rasilimali za Serikali zinatumika kwa manufaa yaliyokusudiwa.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top