Rais Mstaafu Awamu ya Nne wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, akiwasili Kisiwani Pemba kwa ajili ya Sherehe ya Uzinduzi wa Jengo la Afisi ya Uhamiaji na Makaazi ya Askari,Wilaya ya Micheweni, mkoa wa Kaskazini Pemba, ambapo amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mgeni Hassan Yahaya. Uzinduzi huo ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.Uzinduzi huo utafanyika leo,tarehe 4 Januari,2026.
Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.








Comments
Post a Comment