Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dkt Mwigulu: Tuache Tabia ya Kuzoea Matatizo


*Afanya ziara ya kushtukiza Hospitali ya Wilaya Nachingwea

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewaonya watendaji na watumishi wa umma waache tabia ya kuzoea matatizo hasa katika sehemu zinazotoa huduma kwa wananchi.

Ametoa onyo hilo jana (Jumapili, Desemba 21, 2025) wakati akizungumza na wagonjwa na watumishi wa Hospitali ya Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi alipofanya ziara ya kushtukiza ili kujionea hali halisi ya utoaji huduma siku za wikiendi katika hospitali hiyo.

Waziri Mkuu ambaye alikuwa na ratiba ya kukagua ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, mara baada ya kuwasili wilayani humo akitokea Ruangwa, aliamua kuanzia kwanza hospitalini kisha akaenda kwenye ukaguzi wa jengo hilo.

Akiwa hospitalini hapo, alienda moja kwa moja kwenye chumba cha daktari wa zamu ili apate utaratibu wa kumhudumia mgonjwa pindi anapofika hospitalini na akaelezwa kwamba ni lazima mgonjwa aanzie mapokezi na kukata cheti ndipo aje kwa daktari.

Hata hivyo, Waziri Mkuu alikuta wagonjwa wawili nje ya vyumba vya madaktari ambao mmoja wao alikuwa na cheti lakini mwingine hakuwa nacho na alishapita mapokezi bila kuelezwa chochote. Na vyumba vya madaktari havikuwa na wagonjwa, licha ya kuwa madaktari walikuwemo

“Wekeni utaratibu wa kuwaelekeza wagonjwa waende wapi mara tu wanapofika hospitalini. Hapa si mahali pa kuja kufanya matembezi, mtu akija hapa anahitaji kupewa huduma,” alisema wakati akiongea na Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Dkt. Ramadhani Mahiga.

“Naibu Waziri wa Afya toa maelekezo kwa hospitali zote, mgonjwa akifika hospitalini asikilizwe na kuelekezwa wapi pa kwenda. Akifika kwa daktari, kama hakuna mgonjwa mwingine, hana sababu ya kusubirishwa kama tulivyoona hapa,” alisema wakati akitoa maagizo kwa Dkt. Florence Samizi ambaye alikuwepo kwenye ziara hiyo.

“Kuna utaratibu wa kuzoea matatizo, kama kwenye chumba cha daktari hakuna mgonjwa au chumba kingine chochote hakuna mgonjwa, tusiweke mazoea ya kuwangojesha wagonjwa. Tuwahudumie mara moja. Tusidhani kwamba tunapowasubirisha sana, ndiyo sisi tumekuwa mabosi. Haya mambo ni ya huduma, tujirekebishe,” alisisitiza.

Waziri Mkuu alikwenda eneo la maabara na kuzungumza na wagonjwa waliokuwa wakisubiri majibu yao ili kubaini kama kuna ucheleweshaji wowote wa utoaji huduma. Huko alielezwa utaratibu wa vipimo ukoje na muda wa kusubiri kwa baadhi ya vipimo.

Akiwa katika wodi ya wazazi, Waziri Mkuu aliwatembelea akinamama 12 waliokuwemo wodini, kuongea nao na kisha kupewa maelezo ya huduma zinazotolewa na hospitali hiyo. Akitoa maelezo hayo, mkunga na msimamizi wa wodi hiyo, Bw. Dennis Namwembe alisema kwa siku moja, akinamama kati ya sita hadi 10 wanajifungua hospitalini hapo na kwa mwezi mmoja wanaojifungua wanafikia 200.

“Kuhusu huduma ya upasuaji kwa akinamama wanaojifungua, idadi yao inaweza kufikia wastani wa 50 kwa mwezi,” Bw. Namwembe alimweleza Waziri Mkuu.

Vilevile, Waziri Mkuu alikagua ujenzi wa Chuo cha Uuguzi na Ukunga cha Nachingwea ambacho kipo jirani kabisa na hospitali hiyo ambako alielezwa kuwa ujenzi wake umesimama kwa sababu wanasubiri fedha za kukamilisha.

Dkt. Samizi alisema ujenzi wa chuo hicho unagharimiwa na Wizara ya Afya kwa gharama ya sh. bilioni 2.2 ambapo katika awamu ya kwanza, sh. milioni 900 zilikwishatolewa na kutumika. 

“Katika awamu ya pili, wizara imetenga sh. bilioni 1.2 ambapo baada ya kukamilika, chuo hicho kinatarajia kuanza udahili wa wanafuzi kati ya 300 – 400 ifikapo Oktoba, 2026,” alisema.

Mapema asubuhi, Waziri Mkuu alikagua bandari ya Lindi iliyoko eneo la Barazani mjini Lindi na kuiagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania ikamilishe masuala ya kitaalamu kuhusu bandari hiyo.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zainab Tellack alisema wanatamani bandari hiyo ifanyiwe ukarabati kwa kuongeza kina ili iweze kuhudumia meli nyingi zaidi kwani imeanza kuchangamkiwa na wafanyabiashara wakiwemo wa nchi jirani ambao huagiza vyakula na mifugo kutoka Tanzania.

“Mizigo inayopita hapa inafikia tani 1,000 kwa mwezi. Tuna ng’ombe wanatoka Kanda ya Ziwa, wanakaa hapa kwa muda mrefu hadi wanapoteza uzito, hii ni hasara kwa wauzaji.”

Kauli ya Mkuu wa Mkoa iliungwa mkono na Mbunge wa Lindi Mjini, Bw. Mohamed Utaly ambaye alisema anaomba bandari hiyo ikarabatiwe kwani ni nyenzo muhimu katika uchumi wa wana-Lindi. “Wakulima wanalazimika kupeleka korosho zao hadi Mtwara ambayo ni gharama kubwa kwao; kama bandari hii ingetumika, ingewapunguzia mzigo sana,” alisema.



Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...