Mwandishi wa habari Mwandamizi na mtetezi wa Haki za binadamu Edwin Soko amesema kuelekea kwenye uchaguzi mkuu October 29,2025 , Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeendelea kudhihirisha kuwa ndicho chama kinachosikilizwa zaidi na wapiga kura nchini.
Amesema hii ni kutokana na misingi yake ya muda mrefu ya uongozi, sera thabiti na mtandao mpana wa kisiasa unaogusa wananchi kuanzia shina hadi Taifa kwa ujumla
Akizungumza na waandishi na waandishi wa habari leo October 28,2025 amefanya uchambuzi wa mwenendo wa kampeni za wagombea wa vyama mbalimbali kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
"Wananchi waelewe kwamba takwimu na tafiti mbalimbali za kisiasa zimeonyesha kuwa, licha ya kuwepo kwa vyama vingine vya upinzani vinavyoimarika, CCM bado kinaongoza kwa ushawishi mkubwa katika mijadala ya kisiasa, majukwaani, na hata katika majadiliano ya wananchi mitaani"alisema Soko
Aidha ameongeza kuwa, Nguvu ya Historia ni mtaji kwa CCM, chama kilichoasisiwa mwaka 1977 kufuatia muungano wa TANU na ASP, kimejijengea heshima kupitia historia yake ya kushika hatamu za uongozi kwa zaidi ya miaka 45 hivyo
Kupitia misingi ya umoja, amani na maendeleo, chama hicho kimeendelea kuwa kinara wa kuaminika kwa Watanzania wengi wanaotafuta uthabiti wa kisiasa na kiuchumi.
Soko amesisitiza kuwa, miongoni mwa sababu zinazoendelea kukifanya CCM kusikilizwa ni pamoja na viongozi wanaotokana na chama hicho kusimamia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati, ikiwemo ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), miradi ya nishati kama Bwawa la Julius Nyerere, na kuboresha huduma za afya na elimu.
Baadhi ya wapiga kura waliozungumza na vyombo vya habari wamesema wanakipendelea chama hicho kwa sababu ya uthabiti wake wa kisera na uongozi wa tulivu
Ikumbukwe kua zaidi ya vyama 18 vitashiriki uchaguzi mkuu kwa mwaka 2025 na wananchi watachagua viongozi watatu akiwemo Raisi wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mbunge pamoja na Diwani

