Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Dkt Samia yupo tayari kufanya mambo makubwa kwa wenye uliemavu - Majaliwa





WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan yupo tayari kuendelea kufanya mambo makubwa kwa watu wenye ulemavu ili kukuza ustawi wa jamii hiyo kwa kuwawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Amesema hayo Oktoba 11, 2025 wakati wa hafla ya kupokea tuzo kwa niaba ya Rais Dkt. Samia ya  ya kutambua mchango wake katika kusimamia ustawi wa jamii ya watu wenye ulemavu nchini, kwenye hafla iliyofanyika kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay Jijini Dar es Salaam. Tuzo imetolewa na taasisi ya Foundation for Disabilities Hope (FDH)

 


Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia ameahidi kuendelea kuwahudumia watu wenye ulemavu kwa kuwa ana nia ya dhati ya kuona jamii hiyo inakuwa na ustawi utakaowawezesha kutumia fursa zilizopo kujikwamua kiuchumi. “Rais wetu anataka kuona watu wenye ulemavu wanafanya mambo kwa uhuru mkubwa” 

“Ndugu washiriki, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mengi sana,nataka niwaambie amenihakikishia kuwa yupo tayari kuendelea kufanya mambo mengi zaidi, niwaombe watanzania wote tuendelee kumuunga mkono” 

Amesema kuwa Serikali katika kutekeleza dhamira ya Rais Dkt. Samia ya yakuinua ustawi wa watu wenye ulemavu imeendelea kutekeleza mipango, mikakati na afua mbalimbali ikiwemo kufufua Mfuko wa Taifa kwa Watu wenye Ulemavu ambao tangu ulipoanzishwa mwaka 2010 haukuwahi kufanya kazi. 

“Mwaka 2022 serikali ya awamu ya sita imetoa shilingi bilioni 2.1 nahivyo kuwezesha Mfuko huo kutoa ruzuku inayofikia shilingi milioni 408 kwa miaka miwili mfululizo kwa vyama vya watu wenye ulemavu na Shirikisho la SHIVYAWATA” 

Ameongeza kuwa Serikali ilitoa kiasi cha shilingi bilioni 8 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa visaidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika shule za msingi na sekondari. “Vifaa hivyo ni kwa ajili ya Wanafunzi wenye Ulemavu wa kutoona na uoni hafifu, viziwi, Ualbino na wenye ulemavu wa viungo, vifaa vya kufundishia pamoja na vya michezo”

 


“Serikali kupitia mikopo inayotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri imetoa shilingi bilioni 16.4 ambayo ni asilimia mbili inayotengwa kwa Watu wenye Ulemavu kwa vikundi na mtu mmoja mmoja mwenye ulemavu. Lengo nikuwawezesha watu wenye ulemavu kujikwamua kiuchumi” Alisema Mheshimiwa Majaliwa. 

Kwa Upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete amesema kuwa tuzo hiyo inabeba mrejesho wa shukrani kwa kazi nzuri ambayo Mheshimiwa Rais. Dkt Samia ameifanya kwa watu wenye Ulemavu katika kipindi cha miaka yake minne ya uongozi.

“Katika kipindi cha uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia, tumefanikiwa kufungua milango ya upatikanaji wa ajira kwa watu wenye ulemavu, ambapo zaidi ya Wenye Ulemavu 1213 wameajiriwa katika taasisi mbalimbali za Serikali katika kada za afya, elimu, uhasibu, Lishe na Maendeleo ya Jamii”

 Aidha, Mheshimiwa Kikwete amesema kuwa Serikali imetoa ruzuku ya shilingi milioni 61 kwa Kiwanda cha KCMC Moshi Kilimanjaro kuimarisha uzalishaji wa mafuta ya kinga ya saratani ya ngozi kwa watu wenye ualbino kwa gharama nafuu. “Mafuta hayo yamezalishwa na kusambazwa katika vituo vyetu vya afya kupitia Bohari Kuu ya Dawa na yanatolewa bila malipo katika Vituo vya Afya vya Serikali”.

 

Naye, Mkurugenzi wa Taasisi ya Foundation for Disabilities Hope Michael Selali amesema kuwa watu wenye Ulemavu wameamua kutoa tuzo hiyo kutokana na jitihada za ujumuishi zinazofanywa na Rais Dkt. Samia kwa ajili ya watu wenye Ulemavu ambazo zimewawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za kiuchumi 

“Katika jitihada za kuinua Wenye Ulemavu kiuchumi, Serikali imeweza kuanzisha program za ujumuishi kwa watu wenye ulemavu ikiwemo programu ya mfuko wa jenga na Samia ambao umeanzishwa kwa ajili ya kusaidia makundi mbalimbali, ikiwemo ya Wenye Ulemavu”

Ameongeza kuwa Jamii hiyo inamshukuru sana Rais Dkt. Samia kwa namna alivyojenga ujumuishi kwa makundi ya watu wenye Ulemavu “Tumeshuhudia Serikali ya awamu ya Sita imekuwa Ni Serikali jumuishi, fedha ambazo zimepelekwa kwa watu wenye ulemavu zimewanufaisha sana, Tunajivunia na tunamuombea sana Mheshimiwa Rais”

 


Awali, Katibu Mkuu, Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu na Jonas Lubago amesema kuwa vyama vyote ambavyo chini ya SHIVYAWATA vinafurahia ruzuku inayotolewa na Serikali ya awamu ya sita. “Tumeshuhudia mikopo imekuwa ikitolewa kwa ile asilimia mbili ya Watu wenye ulemavu, tumeshuhudia watu wenye ulemavu wakipata ajira Serikalini na kupewa kipaumbele, mioyo yetu imeibeba awamu ya sita”

Ameongeza kuwa kipindi hiki cha awamu ya sita, Watu wenye Ulemavu tumenufaika kwa kuona wenzetu pia wameendelea kuhudumu katika nafasi mbalimbali za juu za uongozi Serikalini. “Katika kipindi cha hivi karibuni kumekuwa na mageuzi makubwa ya Kimfumo ambayo imewezaha kuwa na utambuzi wa idadi ya watu wenye ualbino utakaosaidia utoaji huduma kwa wenye ualbino “

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...