Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Ujenzi Skimu 738 za umwagiliaji, Dkt. Samia utaacha alama isiyofutika sekta kilimo

 


Na: Dkt. Reubeni Lumbagala

Kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania. Hii inatokana na ukweli kuwa kilimo kimeajiri Watanzania wengi zaidi ya asilimia 60 hasa waishio maeneo ya vijijini. Kutokana na kilimo kuwa na tija, wananchi waishio maeneo ya mjini nao siku hizi wanajishughulisha na kilimo kidogo (small scale agriculture) katika makazi yao hasa kilimo cha mbogamboga na matunda. Kimsingi, kilimo kina tija ukizingatia kinaacha athari chanya ya moja mwa moja hasa katika kuwapatia wananchi chakula na fedha.

Kwa nchi yetu ya Tanzania ambayo tunakubaliana kuwa kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wetu, kama nchi hatuna budi kuweka mikakati madhubuti inayotekelezeka ili kuhakikisha tunakuza kilimo chetu ili kugusa kundi kubwa la wananchi ambao wamejiajiri katika sekta hii. Ikumbukwe kuwa sekta ya kilimo imefungamanishwa pia na sekta za ufugaji na uvuvi.

Umuhimu wa sekta ya kilimo hauishii tu kutupatia chakula na fedha lakini pia kilimo kina mnyororo mkubwa wa thamani. Kupitia kilimo, wafanyabiashara wa usafirishaji wanapata fedha kupitia usafirishaji wa mazao kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Pia, kilimo kinatoa ajira kupitia wafanyabiashara wa mazao ambao wananunua mazao kutoka kwa wakulima na kwenda kuyauza sokoni.

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tangu aingie madarakani mwaka 2021, amefanya makubwa katika sekta ya kilimo hasa katika kuongeza maradufu bajeti ya sekta ya kilimo kutoka shilingi bilioni 294 mwaka 2021 hadi kufikia shilingi Trilioni 1.242 mwaka 2025, ongezeko hili ni sawa na asilimia 322. Ongezeko la bajeti limelenga kutekeleza vipaumbele vya sekta ya kilimo ikiwemo kuimarisha utafiti, matumizi ya zana bora, maendeleo ya umwagiliaji, usalama wa chakula, ushirikishwaji wa kifedha na kuongeza thamani ya bidhaa.

Moja ya mkakati mkubwa unaoweza kuleta mapinduzi makubwa ya kilimo (agrarian revolution) ni kutoa msukumo mkubwa hasa katika kilimo cha umwagiliaji (Irrigation farming). Hii inatokana na ukweli kuwa kwa muda mrefu, kilimo chetu kimekuwa kikitegemea mvua na kwa kuzingatia changamoto ya kidunia iliyopo sasa ya mabadiliko ya tabia nchi,  maji ya mvua pekee hayataweza kukuza kilimo chetu badala yake tutarudi nyuma kimaendeleo kwani pale Ujenzi Skimu 738 za umwagiliaji, Dkt. Samia utaacha alama isiyofutika sekta kilimo ukame na upungufu wa mvua, kama Taifa tutegemee kuingia kwenye njaa kubwa, kudidimia kwa sekta za viwanda na biashara.

Oktoba 11, 2025, Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ni Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwa katika kampeni za uchaguzi wilayani Maswa mkoani Simiyu alisema atafanikisha ujenzi wa skimu 738 za umwagiliaji nchi nzima ili kukuza zaidi sekta ya kilimo kwa asilimia 10 na hatimaye kuchangia maendeleo ya nchi kwa kasi kubwa.

"Kilimo cha umwagiliaji maji ndicho kipaumbele chetu, tunakwenda kujenga skimu za umwagiliaji 738 Tanzania nzima. Lengo ni kukuza sekta ya kilimo ifikapo mwaka 2030, nikitoka kwenda kupumzika niache sekta ya kilimo imekuwa kwa asilimia 10 kwa mwaka." Sambamba na hilo, Dkt. Samia akaongeza kuwa "Sasa hivi tunakua kwa asilimia nne hadi tano, nataka niikuze kwa asilimia 10 kwa mwaka hili ndilo lengo langu. Ninapozungumza sekta ya kilimo ni mifugo na uvuvi vyote vinaingia kwenye kilimo."

Kimsingi, ujenzi wa skimu 738 za umwagiliaji utaboresha kilimo chetu kutoka kilimo cha kubahatisha cha kutegemea mvua hadi kuwa na kilimo cha uhakika cha umwagiliaji ambapo wakulima wataweza kulima hadi mara tatu kwa mwaka, hali itakayoboresha maisha yao moja kwa moja. Ule wimbo tuliozoea kuusikia ya kuwa "Kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wetu" unakwenda kuimbika vizuri chini ya uongozi  mahiri wa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ukweli ni kwamba suala la kilimo kuwa uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzani halitabaki kuwa maneno matupu bali wananchi watajionea kwa macho yao namna kilimo kilivyo na tija kwa kubadilisha hali zao za maisha kwani skimu za umwagiliaji ni kichocheo muhimu cha ukuzaji sekta ya kilimo.

Ni vyema Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) ijipange vyema kuhakikisha mpango huu wa ujenzi wa skimu 738 unafanikiwa kikamilifu kwani wananchi tunasubiri kwa hamu utekelezaji wake ambao una tija kubwa kwa maendeleo ya Taifa letu. Ni muhimu pia kuzingatia suala la utunzaji mazingira, hii itasaidia kupata maji ya uhakika yatakayotumika katika skimu zetu za umwagiliaji kwa maendeleo ya kilimo na uchumi wetu. Kwa hakika mafanikio ya ujenzi wa skimu za umwagiliaji ni jambo ambalo litaacha alama kubwa katika historia ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Reubeni Lumbagala ni Mwalimu wa Shule ya Sekondari Funguni ya wilayani Pangani mkoani Tanga.

Maoni: 0620 800 462.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...