Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tarura yatekeleza Miradi Mikubwa ya Miundombinu ya Barabara ya Bilioni 302.95


#Katika kipindi cha Miaka Minne 

Dodoma

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Mhandisi Victor Seff amesema katika kipindi cha miaka minne (4) ya Serikali ya Awamu ya Sita, Wakala umekamilisha ujenzi wa miradi mikubwa ya miundombinu ya barabara za Wilaya yenye thamani ya Shilingi Bilioni 262.46 huku miradi yenye thamani ya Shillingi Bilioni 40.49 ikiwa katika hatua mbalimbali za utekelezaji na miradi yote ikikamilika itakuwa na thamani ya Shilingi Bilioni 302.95.

Mhandisi Seff amesema mafanikio hayo yametokana na ongezeko la bajeti lililofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita kwa TARURA ambapo awali walikuwa wakipokea bajeti ya Shilingi Bilioni 275 kwa mwaka lakini baada ya Serikali ya Awamu ya Sita kuona kazi kubwa ya TARURA bajeti iliongezeka kutoka Bilioni 275 kwa mwaka hadi kufikia Shilingi Trilioni 1.1 sawa na ongezeko la asilimia 230.

“Baadhi ya miradi iliyokamilika ni ujenzi wa barabara za lami Kilomita 58.5 katika mji wa Serikali Mtumba-Dodoma, daraja la Berega mita 140 wilayani Kilosa-Morogoro, daraja la Mbwemkuru mita 75 wilayani Ruangwa-Lindi, barabara ya lami Visiga-Zegereni Kilomita 12.5 wilayani Kibaha-Pwani na barabara ya lami Kilomita 5.1 katika eneo la viwanda Dodoma”, amesema.


Ameeleza kuwa, Wakala umeendelea na usimamizi madhubuti wa miradi ya wadau wa maendeleo ya Benki ya Dunia na Umoja wa Nchi za Ulaya. Miradi hiyo ni Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP 2) wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1,136.172 {US$ 438 milioni}), Uendelezaji wa Bonde la Mto Msimbazi (MBD) wenye thamani ya Shilingi Bilioni 608.4 {US$ 260 milioni) na Uboreshaji wa Miji 45 (TACTIC) wenye thamani ya Shilingi Bilioni 959.4 {US$ 410 milioni}).

Miradi mingine ni uboreshaji wa barabara za vijijini na fursa za kijamii na kiuchumi kwenye maeneo yenye fursa za kilimo (RISE) wenye thamani ya Shilingi Bilioni 811.65 {US$ 350 milioni}) na Ujenzi wa barabara kwenye maeneo ya kilimo cha mazao ya Kahawa, Chai, matunda na mbogambaga (Agri-connect) wenye thamani ya Shilingi Bilioni 138.528 {EUR 48 milioni}).

“Miradi hii ikikamilika itagharimu takribani Shilingi Trilioni 3.68 na hadi sasa utekelezaji wa jumla umefikia asilimia 40 na miradi yote inategemewa kukamilika ifikapo mwezi Aprili 2030. Miradi hii ikikamilika jumla ya Kilomita 1,242.52 za barabara za lami, Kilomita 151 za mifereji, masoko 56 na stendi za mabasi 39 vitakuwa vimejengwa”, ameongeza.

Aidha, Mhandisi Seff amesema Wakala umetekeleza miradi ya ujenzi na matengenezo ya barabara za Wilaya kwa kuzingatia sera za ushiriki, ushirikishwaji na uwezeshaji wa jamii kiuchumi ambapo asilimia 99.2 ya zabuni za ujenzi na matengenezo ya barabara za vijijini na mijini zimekuwa zikitolewa kwa makandarasi wazawa kila mwaka huku asilimia 30 ya bajeti ya Mfuko wa Barabara hutumika kutoa zabuni kwa makundi maalumu kila mwaka.

“Jumla ya vikundi 344 vya wananchi vimeshiriki kwenye kazi za matengenezo ya barabara na hadi kufikia Julai, 2025 ajira 173,760 zilitolewa kwa wananchi kwenye miradi ya ujenzi wa barabara”, amesema.

Vilevile, ameongeza kuwa Wakala kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (Economic and Social Research Foundation-ESRF), umefanya tathmini ya matokeo ya uboreshaji wa barabara za vijijini na ufikiwaji wake kwa wananchi, mwaka 2025. Tathmini hiyo imeonesha matokeo makubwa yaliyopatikana baada uboreshaji wa mtandao wa barabara za Wilaya.

“Tathmini imeonesha, muda wa usafiri na usafirishaji kwenda kwenye huduma za kijamii na kiuchumi kama masoko na hospitali umepungua kwa dakika 17.5, gharama za usafiri na usafirishaji zimepungua kwa asilimia 75.3, hali ya upatikanaji wa usafiri na usafirishaji imefikia asilimia 86 ikilinganishwa na asilimia 20 kwa barabara ambazo hazijaboreshwa na endapo barabara zikiboreshwa kwa kiwango cha lami au changarawe hali ya usafiri inaongezeka kwa takribani asilimia 66 na upotevu wa mazao umepungua kwa asilimia 72.5 kutokana na uboreshaji wa barabara vijijini”.

Ameendelea kufafanua “kiwango cha ufikiwaji wa mtandao wa barabara za Vijijini unaopitika majira yote ya mwaka kimeongezeka kutoka asilimia 24.6 mwaka 2016 hadi asilimia 61.0 mwaka 2025, hii inaonesha kwamba sehemu kubwa ya wakazi wa vijijini wana pata huduma za usafiri na usafirishaji jambo ambalo ni muhimu kupunguza umasikini, upatikanaji wa huduma na ukuaji wa Uchumi”.

Katika hatua zilizochukuliwa kukabiliana na changamoto za mitaji kwa Makandarasi Wazawa katika kutekeleza kazi za barabara za Wilaya, Mhandisi Seff ameeleza kuwa Wakala kwa kushirikiana na Benki ya CRDB imeratibu uanzishwaji wa Hati Fungani ya Miundombinu iitwayo “SAMIA INFRASTRUCTURE BOND” kwa lengo la kukusanya jumla ya Shilingi Bilioni 150 ili kuwasaidia Wakandarasi wazawa kupata fursa za mikopo ya fedha na dhamana za kazi kwa gharama nafuu.

“Kiasi cha Shilingi Bilioni 323.09 zimekusanywa ikiwa ni asilimia 215.4 ya lengo lililowekwa ambapo kiasi cha Shilingi Bilioni 223.8 kimeombwa na Wakandarasi Wazawa wapatao 276 kwa ajili ya utekelezaji wa kazi za mikataba ya matengenezo na ujenzi wa barabara”.




Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...