Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Maboresho bandari ya Tanga, yaanza kulipa


* Fedha zilizotolewa na serikali zarudi

Na Mwandishi Wetu, Tanga

FEDHA zilizotolewa na serikali kiasi cha shilingi bilioni 429.1 kwa ajili ya uwekezaji katika bandari ya Tanga, fedha hizo zimerudi na kubaki salio la shilingi bilioni 56.7.

Akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake Leo Julai 10, Meneja wa bandari ya Tanga Mhandisi Maosud Mrisha alisema kuwa kwa kipindi cha miezi 24 taasisi mbili za serikali za TPA na Mamlaka ya mapato nchini TRA, wameweza kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 484.8.

"Ile fedha iliyotolewa na serikali kiasi cha shilingi bilioni 429.1 imesharudishwa na taasisi mbili za TPA na TRA kwa miezi 24 na chenji pembeni imebaki," alisema Mhandisi Mrisha na kumpongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji huo.

Akifafanua kuhusu makusanyo hayo alisema kwamba TPA  imeendelea kuvunja rekodi ya mapato kutokana na uwekezaji uliofanywa na Serikali na kupelekea ongezeko la shilingi bilioni 30 ya mapato ambayo waliwekewa lengo la kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 45.56 hadi kufikia makusanyo ya shilingi bilioni 75.139.

Aidha alisema katika mwaka wa 2023/2024 Bandari ya Tanga iliweza kukusanya kiasi cha Bilioni 38.7 tofauti na makusanyo ya shilingi  bilioni 75.139 ikiwa ni ongezeko la asilimia 94.

Meneja huyo alisema makusanyo hayo ni kwa taasisi mbili za serikali ambapo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mwaka wa fedha 2024/2025 waliweza kukusanya shilingi bilioni 215 kati ya hizo Bilioni 107 zimetoka Bandari ya Tanga kupitia mizigo mchanganyiko.

Pia alisema kwa upande wa makusanyo ya mafuta waliweza kukusanyia kiasi cha shilingi  bilioni 108 hivyo ukichukua makusanyo hayo kwa taasisi hizo ni kiasi cha shilingi bilioni 215.22  na TPA wamekusanya shilingi bilioni 75.159 na kufanya jumla kuwa shilingi bilioni 290 ambazo zimeweza kukusanywa kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kwa kipindi cha miezi  24.

Aliongeza  kutoka mwaka 2023/2024 Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) na Mamlaka ya Mapato (TRA) waliweza kukusanya kiasi cha Bilioni 195 na ni taasisi mbili tu kwa mchanganuo huo kwamba TPA walikusanya Bilioni 38.7 na TRA walikusanya Bilioni 156.75  hiyo jumla yake ni zaidi Bilioni 195.

Alieleza kwamba ukichukua miezi 24 mwaka 2023/2024 ilikuwa ni Bilioni 195 na pointi zake  na 2024/2025 nilikuwa ni bilioni 290 ukizijumulisha zote unapata kwa miezi 24 TRA na Bandari ya Tanga imeweza kukusanya Bilioni 485.8. 

Meneja huyo alisema kwamba katika Bandari ya Tanga  June 30 mwaka huu, mwaka wa fedha uliomalizika wameweza kuhudumia shehena tani milioni 1,416,127  wao wamefanikiwa kuhudumia mertiki tani milioni 1,326,415.

Alieleza katika mwaka wa fedha uliopita 2023/2024 bandari iliweza kuhudumia metric tani milioni 1,191,480 ukichukua tofauti ya mwaka huu na mwaka 2023/2024 na mwaka 2024/2025 waliohudumia watapata tofauti ya laki 1,340,000 utaona kuna ongezeko la asilimia 11.3 kati ya mwaka 2023/2024 na mwaka 2024/2025 bandari imeweza kuongeza kiwango cha kuhudumia shehena.

Akizungumzia kuhusu meli zilizohudumiwa na Bandari hiyo alisema kwamba walipewa lengo la kuhudumia meli 222 lakini kwa mwaka wa fedha 2024/2025  baada ya kupewa malengo hayo wameweza kuhudumia meli 458 katika meli hizo meli 148 za Bahari kuu na Meli 310 ni za Mwambao.

Mwaka 2023/2024 Bandari ya Tanga iliweza kuhudumia meli 307 utaona kuna tofauti ya meli 151 ni sawa na asilimia 49.1 wameongeza idadi ya kuhudumia meli zaidi  na upande wa makasha walipewa lengo la kuhudumia makasha 8,351 lakini wamefanikiwa kwa mwaka wa fedha 9,026 ni ongezeko la asilimia 8 lakikni mwaka 2023/2024 waliweza kuhudumia makasha tools  7,817 ukiangalia ni ongezeko la asilimia 15.46 ,

Upande wa abiria mwaka 2024/2025 walipewa lengo la kuhudumia abiria 120,000 lakini hawakufanya vizuri waliweza kuhudumia kwa asilimia 50 ambapo abiria 59,960 waliweza kuhudumiwa kwa kipindi cha mwaka 2024/2025.

Alisema mwaka wa nyuma yake 2023/2024 waliweza kuhudumia abiria 62,904 hiyo kwa sababu katika eneo hilo ni wadau binafsi wenye meli ndio wenye jukumu la wa kuwasafirisha abiria kutoka Tanga kwenda maeneo mengine kama Zanzibar maeneo ya Pemba na Unguja. 




Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...