Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mavunde Aongoza Kikao cha Kimkakati wa Kiuchumi wa Nchi Kupitia Shirika la Madini la Taifa (Stamico)


▪️Lengo ni kuiwezesha Taifa Kushiriki kikamilifu katika uvunaji Rasilimali Madimi kupitia uwekezaji Mkubwa wa STAMICO 

▪️STAMICO kuweka nguvu kubwa katika madini mkakati na adimu

▪️Mapato ya Shirika yatarajiwa kuongezeka kwa asilimia zaidi ya 500 ifikapo mwaka 2029

▪️Yaja na kauli mbiu mpya ya 𝙈𝘼𝙎𝙏𝘼𝙎𝙃𝘼(𝙈𝙖𝙠𝙚 𝙎𝙏𝘼𝙈𝙄𝘾𝙊 𝙎𝙝𝙞𝙣𝙚 𝘼𝙜𝙖𝙞𝙣)


*Dodoma*

Shirika  la  Madini la Taifa  (STAMICO) limekaa Mguu Sawa kuhamia kwenye Uwekezaji Mkubwa wa  Madini Muhimu na Madini Mkakati huku tayari likiwa na mafanikio kadhaa ikiwemo kuachana na utegemezi kwa Serikali kwa asilimia 100 na likiwa limekwisha toa gawio kwa Serikali  ya kiasi cha shilingi bilioni 9.

Mbali na hayo, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha Shirika hilo linakua kubwa kama ilivyo malengo ya kuanzishwa kwake ya kuwekeza kwa niaba ya Serikali ambapo miongoni mwa majukumu yake ni pamoja na kuwekeza  kwenye miradi ya kimkakati ya utafutaji na uchimbaji madini  ili kuongeza manufaa zaidi kwa taifa.

Hayo  yamebainishwa Mei 19, 2025 zikiwa zimepita siku kadhaa tangu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lipitishe Bajeti ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2025/26 ambapo miongoni mwa yaliyopangwa kutekelezwa mwaka ujao ni pamoja na kuzijengea uwezo taasisi zilizo chini ya Wizara pamoja na kuendeleza mnyororo wa thamani katika madini muhimu na mkakati.

Kikao hicho ni cha pili baada ya kikao cha kwanza kilichofanyika Mei 12, 2025 jijini Dodoma ambavyo vyote vimeongozwa na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde vikihusisha Menejimenti ya Wizara na Taasisi zake ili kujadili kwa pamoja andiko la kuiwezesha STAMICO) kuwekeza katika uchimbaji mkubwa wa madini nchini.

Awali, STAMICO liliwekwa kwenye orodha ya mashirika yanayopaswa kufutwa na Serikali  na miaka ya karibuni, kupitia Falsafa ya 4 Rs za Mhe. Rais wa Awamu ya sita Dr. Samia Suluhu Hassan Shirika lineweza kuishi mageuzi jayo kwa vitendo na kuweza kujipambanua  kuwa miongozi mwa mashirika ya mfano yanayofanya vizuri na sasa  limejikita kuwekeza katika shughuli za uchimbaji mkubwa na wa Kati wa madini muhimu na mkakati pamoja na dhahabu katika zama hizi  ambazo mataifa mengi duniani yanapambana  kuhakikisha yananufaika na rasilimali madini zilizopo kwenye nchi zao.

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Mavunde amesema miradi inayotarajiwa kufanywa na STAMICO italirejesha tena shirika hilo kwenye ramani ya dunia na kusisitiza kwamba, matamanio yake ni kuliona  shirika  hilo linakua  kubwa kama ilivyo kwa Kampuni kubwa kama  Barrick Gold Mine na AngloGold Ashanti  ili liweze kuongeza manufaa zaidi kwa  nchi kupitia rasilimali madini zinazopatikana nchini.

‘’ Ninawapongeza STAMICO kwa hatua kubwa mliyopiga hadi mlipo sasa. Miradi hii pindi itakapotekelezwa, kama taifa tutakwenda kunufaika ipasavyo na kusema, ‘’tukipata nafasi ya kuifanya kazi wenyewe, manufaa yake ni makubwa.

Shirika hili ni muhimu sana katika kuisaidia nchi yetu kunufaika na rasilimali madini,tutatumia maarifa na ujuzi wote kuhakikisha STAMICO inakuwa moja kati ya mashirika makubwa ya umma katika kushiriki kikamilifu kwenye sekta ya madini barani Afrika kwa kuja na kauli mbiu ya  MASTASHA (𝙈𝙖𝙠𝙚 𝙎𝙏𝘼𝙈𝙄𝘾𝙊 𝙎𝙝𝙞𝙣𝙚 𝘼𝙜𝙖𝙞𝙣)kulirudishia ari,nguvu na malengo iliyokuwa nayo wakati  wa uanzishwaji wake’’ amesema Waziri Mavunde.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Dkt. Venance Mwasse amekielekeza kikao hicho kuhusu mipango kabambe iliyopangwa kutekelezwa na shirika hilo, pamoja na kueleza manufaa ya miradi hiyo ikiwemo kutoa ajira za moja kwa moja, mapato kwa serikali, kuongeza ushindani na  uwekezaji kutoka nje  kwa lenfo la kuongeza tija na kuchochea maendeleo ya teknolojia.

Dkt. Mwase ameongeza kwamba, miongoni mwa miradi itakayotekelezwa, ipo ambayo itatekelezwa na shirika lenyewe na ile itakayotekelezwa kwa ubia na kuongeza kwamba tayari STAMICO inazo leseni zake  nyingine za uchimbaji zikihusisha madini ya dhahabu na kinywe.

STAMICO lilianzishwa Mwaka 1972 kwa lengo la kuwekeza kwa niaba ya Serikali katika mnyororo mzima wa thamani wa madini.







*#𝙈𝙖𝙠𝙚𝙎𝙏𝘼𝙈𝙄𝘾𝙊𝙎𝙝𝙞𝙣𝙚𝘼𝙜𝙖𝙞𝙣#

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...