Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Ongezeko la Mapato Namanga Lamkosha Dkt. Biteko


📌Ailekeza TANESCO kufunga Kituo cha Kupoza Umeme Longido

📌Maelekezo ya Serikali yatekelezwa Longido

📌Amuagiza Makonda kusimamia ufungaji vifaa vya maabara Sekondari ya Longido Samia


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameeleza kufurahishwa kwake na ongezeko la ukusanyaji wa mapato katika kituo cha huduma za pamoja mpakani mwa Tanzania na Kenya cha Namanga.

Akizungumza Aprili 24, 2025 Namanga mkoani Arusha wakati katika ziara yake ya kutembelea miradi ya maendeleo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano Dkt. Biteko ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania Kituo cha Namanga kwa kufanya kazi kwa ufanisi.

“ Nimefurahishwa sana na urahisi wa biashara na kila eneo limekuwa na ukuaji wa watu na bidhaa kwenye kusafirisha nje ya nchi ili kuleta fedha ya kigeni zitakazowezesha kufanya shughuli zingine nawapongeza sana, nawashukuru kwa kuwa na malengo makubwa ya kukusanya shilingi bilioni 124 na hadi kufikia leo mmekusanya shilingi bilioni 101 huku mkiwa na miezi kadhaa ya kuendelea kukusanya mapato” amesema Dkt. Biteko.

Amewataka watendaji hao kuendelea kuwa na utaratibu mzuri wa kurahisisha biashara kwa kuondosha mizigo inayosafirishwa kwa kutumia muda wa dakika 30 hadi 40 badala ya saa 2 kama ilivyokuwa hapo awali.

Ameendelea kusema kuwa Kituo hicho cha Namanga kilichofunguliwa mwaka 2018 na aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, hayati Dkt. John Pombe Magufuli na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta kwa lengo la kurahisisha biashara kati ya nchi hizo mbili. Hivyo, watendaji hao waendelee kuwa mabalozi wazuri kwa kutangaza taswira njema ya Tanzania wakati wakitekeleza majukumu yao.

Awali akikagua Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Longido  Samia, Dkt. Biteko amesema kuwa baada ya siku kadhaa Kampuni ya Taifa Gesi itafunga miundo mbinu ya mfumo wa gesi shuleni ikiwa ni sehemu ya Serikali ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Pia, Dkt. Biteko amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Makonda kuhakikisha Shule hiyo inapata vifaa vya maabara ili wanafunzi waweze kujifunza kwa vitendo na si nadharia pekee.

“ Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya hakikisheni hizi maabara zinafanya kazi kwa kupata vifaa, tabia ya wanafunzi kuchora bunsen bunner badala ya kuziiona na kuzitumia kwa kujifunzia kwa vitendo iishe, ” amesema Dkt. Biteko.

Amebainisha kuwa amemuelekeza Mkuu huyo wa Mkoa kuangalia namna ya kuweka uzio na kupata gari kwa ajili ya shule hiyo, huku akiwataka wanafunzi kujifunza kwa bidii ili watimize ndoto zao  na kuwa Shule hiyo ni kielelezo cha Mkoa wa Arusha.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara katika kijiji cha Mundarara, Dkt. Biteko amesema madini ni kichocheo kikubwa katika maendeleo ya kiuchumi na kuwa Kijiji cha Mundarara kimekuwa na uzalishaji wa madini ya rubi na kuwa anafurahishwa kwa kuona sasa Watanzania wanaweza kufanya kazi za uchimbaji wa madini.

Kuhusu umeme, Dkt. Biteko amesema “Vijiji vyote 52 vina umeme, kuna vitongoji 176 na vitongoji vyenye umeme ni 112 pekee. Kuna maeneo ambayo yanahitaji nguzo 25 na nimemuelekeza Meneja wa TANESCO ndani ya wiki tatu nguzo ziwekwe na watu wapate umeme. Nimemuelekeza pia Meneja na bosi wake transforma ije hapa wiki ijayo ifungwe na watu wapate umeme,” amesema Dkt. Biteko.

Vilevile, Dkt. Biteko ameelekeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kujenga njia nne za kupeleka umeme Loliondo, Namanga, Mundarara na Kamwanga na baadae kujenga kituo cha kupokea, kupoza na kusafirisha umeme ili kusaidia wananchi kupata umeme na kufanya shughuli zao za kiuchumi.

Pamoja na hayo, amesema kuwa Rais Samia amefanya kazi kubwa ya kuwaletea Watanzania maendeleo na kuwaasa wamuunge mkono. Aidha, ametoa wito kwa wananchi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu kwa kuchagua viongozi watakao waletea maendeleo.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amebainisha kuwa katika kusheherekea miaka 61 ya Muungano ni vyema kila Mtanzania ajiulize kwa nafasi yake, amefanya nini yeye binafsi, lakini pia amefanya kitu gani hasa cha kukumbukwa kwa watu wake wa karibu, kwa jamii inayomzunguka na pia kwa Taifa.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Wizara ya Madini na Mbunge wa Longido, Mhe.  Dkt. Steven Kiruswa amesema kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan imeendelea kusaidia miradi ya maendeleo ambapo wachimbaji wadogo wilayani humo sasa  wana umeme wa uhakika.

Ameendelea kusema Wilaya hiyo imenufaika na miradi ya maendeleo ambapo usanifu wa barabara ya kutoka Siha hadi Longido unaendelea.

“ Mgodi wa magadi soda wa  Engaruka umetengewa fedha na tayari watu wako tayari kuja kuwekeza na itasaidia kujenga mji wa kisasa, tuna zaidi ya tani milioni 768 ambayo tunaweza kuchimba kwa muda mrefu bila kuisha. Katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Samia wachimbaji wadogo wameweza kupata kiasi cha shilingi bilioni 9.999 ambapo Serikali inapata mapato, ”amesema Dkt. Kiruswa.

Amesisitiza “ Wilaya hii tumepewa fedha ya kujenga shule za  sekondari sita katika kata zetu na tumebakiza kata tatu ambazo hazina shule za sekondari, kazi ya kujenga shule katika kata hizo inaendelea. Mafanikio haya yasingeweza bila kuwa na ushirikiano na mshikamano kati aya Chama Cha Mapinduzi, Serikali na viongozi wa kimila.”

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Makonda amesema kuwa maelekezo ya Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Mchengerwa kuhusu ujenzi wa daraja, upatikanaji wa haki na kituo cha afya yamefanyiwa kazi. 

“ Tayari fedha zaidi ya shilingi milioni 250 imetolewa na baada ya wiki moja itaonekana kwenye mfumo kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kituo cha afya. Kuhusu barabara, katika bajeti hii imetengwa fedha shilingi milioni 270, fedha hizi ni kwa ajili ya barabara ya Resingita yenye urefu wa km 13 na barabara ya Longido kwenda Meloe imetengewa shilingi milioni 105,”amesema Mhe. Makonda.






Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...