Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mara yaliomba Shirika la Emedo Kupanua Shughuli zake

Na Rs; Mara

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Dominicus Lusasi Februari 28 Mwaka huu amezindua Mpango Shirikishi wa Uvuvi Salama katika Kijiji cha Busekela, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. 

Mpango huo unatekelezwa na Shirika lisilo la kiserikali la EMEDO ambalo Lusasi ameliomba shirika hilo kupeleka elimu ya kuzuia kuzama maji katika Wilaya nyingine za Mkoa wa Mara zinazozunguka ziwa Victoria. 

Lusasi amesema ajali za majini zimesababisha watu wengi kupoteza maisha na kuwa chanzo cha familia nyingi kuishi maisha duni kwa kupoteza nguzo muhimu katika familia zao. 

“Eneo kubwa la Mkoa wa Mara linazungukwa na Ziwa Victoria na mradi huu unavisaidia vijiji viwili tu vya Wilaya ya Musoma, kama itawezekana tunaomba mpanue huduma za mradi huu ili Wilaya zote zinufaike na mradi huu” amesema Bwana Lusasi. 

Lusasi amesema kuwa takwimu zinaonyesha kuwa kwa mwaka watu laki tatu duniani hupoteza maisha kwa kuzama maji na zaidi ya asilimia 90 ya vifo hivyo vinatokea katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati ikiwemo Tanzania. 

Ameliasa Shirika la EMEDO kuhakikisha kuwa majaketi okozi yanapatikana katika maeneo ya wavuvi na kwa kulipia kidogo kidogo ili kuwawezesha wavuvi kumiliki vifaa hivyo vya usalama katika maisha yao. 

Aidha ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kuendelea kutoa elimu kuhusu usalama wa majini na uokoaji kwa wavuvi kupitia mikutano ya hadhara katika maeneo ya wavuvi ili kuwawezesha kufahamu namna ya kujikinga na ajali na kutoa msaada wakati wa dharura. 

Kaimu Katibu Tawala huyo wa Mkoa Mara pia amewahimiza wananchi kuzingatia utabiri wa hali ya hewa na kuchukua tahadhari kabla ya kusafiri majini na kuwataka wamiliki wa vyombo vya majini kuzingatia sheria na taratibu zote za usalama kwenye maji kabla ya vyombo vyao kuanza safari sanjari na kuzingatia usafi, kujenga vyoo bora na kuvitumia ili kuweza kujilinda na magonjwa ya mlipuko yanayotokana na uchafu. 

Kwa upande wake,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Mhe. Charles Nyambita Magoma amelishukuru Shirika la EMEDO kwa kuvifikia vijiji hivyo viwili katika mradi wao na kuwaomba kuongeza vijiji zaidi ili wananchi waweze kupata elimu. 

“Halmashauri yetu ina kata 21 na kati ya hizo Kata 18 zimeguswa na Ziwa Victoria na wananchi wa kata hizi bado hawajapata elimu ya namna ya kujilinda na kuzama majini kama wenzao wa Busekera na Kome” amesema Mhe. Magoma. 

Aidha, Mhe. Magoma amewataka wavuvi na wananchi wote kwa ujumla kuzifuata sheria ambazo wamezitunga ili kudhibiti ajali za kuzama majini na kuwataaka wananchi wa vijiji hivyo kutoa elimu kwa wenzao kuhusu sheria hizo na taratibu za vijiji ili ziweze kuenea katika mialo mingine ya wavuvi wa Ziwa Victoria. 

Kwa upande wake, Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma,Wakili Anabu Shariph amesema katika mchakato wa kutunga sheria hizo maoni yote ya wadau yalizingatiwa na sheria hizo zilipita katika Kikao cha Kamati ya Menejimenti, Kamati ya Mipango na Fedha na hatimaye kuidhinishwa na Baraza la Madiwani.

Wakili Shariph amesema sheria hizo zipo kwa ajili ya kudhibiti na kuwaokoa wananchi kutokana na ajali mbalimbali za kuzama na namna wanavyoweza kujikinga kwa kufuata na kuzingatia sheria hizo. 

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Shirika la EMEDO, Editrudith Lukanga amesema mradi huo umeibuliwa umetokana na utafiti uliofanywa na shirika hilo na kwa sasa unatekelezwa katika Wilaya za Nyamagana na Ukerewe (Mwanza), Muleba (Kagera) na Musoma (Mara). 

Lukanga amesema kwa Mkoa wa Mara mradi huu unatekelezwa katika Vijiji vya Busekera na Kome na mpaka sasa mradi huu umefanikiwa kutoa elimu kwa watu 1,300 na robo yao wakiwa ni wanawake na mwaka huu wanategemea kutoa elimu kwa wavuvi 400. 

Aidha ameiomba Serikali kulipa kipaumbele suala la usalama wa majini katika mipango na bajeti zake ili kudhibiti ajali zinazotokana na uzembe na watu kutokuzingatia sheria na taratibu za usalama majini. 

Kwa Mujibu wa Lukanga,Mradi huo utatoa elimu kwa wananchi, utasambaza majaketi okozi ya gharama nafuu na kulipa kwa awamu pamoja na kufunga mabango ya utabiri wa hali ya hewa ya kisasa ili wananchi waweze kutambua kabla ya kuanza shughuli za uvuvi. 

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi huo Bwana Arthur Wihabu Mugema amesema Shirika la EMEDO litasambaza majaketi okozi ambayo yatakuwa yanapatikana katika maeneo mbalimbali na wananchi watalipia kwa bei ya ruzuku shilingi 40,000. 

“Ili kuwarahisishia katika malipo wavuvi, shirika litatoa majaketi haya kwa mkopo na mvuvi atatakiwa kulipia taratibu hadi atakapokamilika deni lake la jaketi okozi” amesema Bwana Mugema.  

Mugema amesema shirika hilo pia litafunga mbao tano za taarifa za hali ya hewa ambapo mbao mbili zitafungwa katika Kijiji cha Kome na mbao tatu zitafungwa katika Kijiji cha Busekera ili kuwawezesha wavuvi kupata taarifa sahihi za hali ya hewa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA).

Aidha,Mugema amesema Shirika kwa kushirikiana na wadau mbalimbali litaendelea kutoa elimu ya usalama majini na namna ya kufanya uokoaji kwa kushirkiana na wadau mbalimbali ikiwemo Jeshi la Polisi, Halmashauri na Serikali kwa ujumla.




Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...