Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Wakuu Wa Wilaya Musoma/ Rorya Tokeni Ofisini


Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 17 Februari, 2025 ameitembelea kambi ya wagonjwa wa kuharisha na kutapika katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na kuwaagiza wakuu wa Wilaya za Musoma na Rorya pamoja na wataalamu wa Halmashauri kutoka ofisini na kushughulikia chanzo cha ugonjwa huo. 

Mhe. Mtambi ametoa maagizo hayo katika Zahanati ya Bwai ambayo kwa sasa inatumika kama Kituo cha Halmashauri ya Musoma kwa ajili ya kutibu wagonjwa wa kuharisha na kutapika katika eneo hilo na kujionea hali halisi ya kituo hicho na kuzungumza na viongozi, wataalamu na wananchi waliokuwepo eneo hilo. 

“Ninawataka Wakuu wa Wilaya na Wataalamu wa Halmashauri za Wilaya ya Musoma na Rorya kutoka ofisini na kufanya kampeni maalum ya ujenzi wa vyoo katika maeneo ambayo yamekumbwa na tatizo hilo na kushughulikia chongamoto zozote zinazoweza kuendeleza changamoto hizi katika maeneo yao” amesema Mhe. Mtambi. 

Mhe. Mtambi amezitaka Wilaya hizo kuanzisha operesheni maalum ya kukagua vyoo bora na salama na matumizi ya vyoo hivyo na hususan maeneo yenye mikusanyiko kama vile kambi za wavuvi, masoko na majengo ya huduma mbalimbali kuhakikisha yana vyoo vinavyotumiwa na wananchi. 

Mhe. Mtambi amewataka wananchi wa eneo hilo na Mkoa wa Mara kwa ujumla kubadilisha namna wanavyoishi maisha yao na kutekeleza kwa vitendo maelekezo ya wataalamu wa afya ili kujilinda na kuwataka katika hili wasisubiri kusukumwa. 

Mhe. Mtambi amesema kwa sasa Halmashauri za Wilaya ya Rorya na Musoma zina wagonjwa wa kutapika na kuharisha na kuwataka viongozi kuchukua hatua za haraka na maksudi kukabiliana na chanzo cha tatizo hilo ambalo ni matumizi ya vyoo safi na salama.  

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Dkt. Joseph Fwoma amesema tangu tatizo hilo lilipoanza Januari 23, 2025 Halmashauri hiyo imepata jumla ya wagonjwa 63 na kati yao mmoja amefariki dunia na wengine kuruhusiwa baada ya kupona na wagonjwa tisa tu ndio wanaendelea na matibabu katika kituo hicho. 

Dkt. Fwoma amesema tatizo hilo linatokana na kuwepo kwa mwalo mkubwa wa wavuvi katika eneo hilo pamoja na kisiwa kilichopo jirani ambacho kinachokaliwa na wavuvi jirani na Zahanati ya Bwai na ndio sababu ya kuchagua zahanati hiyo kama kituo cha halmashauri cha kuwahudumia wagonjwa hao. 

Bwana Fwoma amesema jitihada mbalimbali zimefanyika na Halmashauri pamoja na Mkoa ikiwa ni pamoja na kuwahamishia wataalamu zaidi katika kituo hicho, kuweka dawa za kutosha, kusambaza dawa za kutibu maji, kuwahamishia wagonjwa wa kawaida katika majengo mapya ya Kituo cha Afya Bwai kilichopo jirani na eneo hilo na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kujikinga dhidi ya ugonjwa huo. 

Akizungumza katika kituo hicho, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka amesema kama Wilaya wanaendelea kutoa elimu kwa wananchi na kuwahamasisha wananchi kujenga na kutumia vyoo bora na hususan katika vijiji vilivyoko kando kando ya ziwa. 

“Tayari jitihada mbalimbali zimeshafanyika ikiwa ni pamoja na kuzungumza na wananchi na kuwaagiza RUWASA Wilaya ya Musoma kukamilisha kwa haraka mradi wa maji unaotekelezwa katika Kata ya Busambara ili wananchi wa eneo hili wapate maji safi na salama” amesema Mhe. Chikoka. 

Mhe. Chikoka ameahidi kuongeza nguvu kwa kufanya operesheni maalum ya kutoa elimu pamoja na kuhamasisha ujenzi na matumizi ya vyoo, kuchemsha maji ya kunywa na kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya katika eneo hilo. 

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Bwai Dkt. Justus Francis Haule amesema hadi wakati Mkuu wa Mkoa anatembelea, kituo hicho kilikuwa na wagonjwa tisa ambapo kati yao wagonjwa saba ni wanaume huku wawili wakiwa ni wanawake. 

Dkt. Haule amesema kwa sasa kituo hicho kina dawa zote muhimu za kukabiliana na tatizo hilo na tayari Halmashauri imeagiza dawa nyingine kama ugonjwa wa kuharisha na kutapika utaendelea katika eneo hilo. 

Katika ziara hiyo, Mhe. Mtambi aliambatana na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usalama wa Wilaya ya Musoma, baadhi ya watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mkurugenzi na baadhi ya watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, viongozi wa vijiji na Kata wa eneo hilo. 






Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...