Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mheshimiwa Mobhare Matinyi, akisalimiana na Mfalme Carl XVI Gustaf wa Sweden, kwenye Kasri la Mfalme jijini Stockholm, tarehe 9 Desemba, 2025. Kushoto ni Binti Mrithi wa Ufalme, Victoria, katikati ni Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Sweden, Balozi Maria Christina Lundqvist, na kulia ni Mke wa Balozi, Yvonne Matinyi. Katika mazungumzo yao mafupi, Mfalme Gustaf na Balozi Matinyi walijadiliana kuhusu uimarishaji wa uhusiano baina ya nchi hizo mbili, hususani, katika nyanja za biashara, uwekezaji na utalii. (Picha kwa hisani ya Kasri la Mfalme).
Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.


Comments
Post a Comment