Wananchi wa Mkoa wa Dar Es Saalam Tujitokeze Kwenye Mikutano Yote ya Dkt Samia-Msama

GEORGE MARATO TV
0

 


Aliyekuwa mtia nia wa Ubunge Jimbo la Ukonga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Production, Alex Msama, ametoa wito kwa wananchi wa Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kumpokea na kushiriki katika kampeni za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM na mgombea urais kupitia chama hicho.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Msama amesema ujio wa Rais Samia katika jiji la Dar es Salaam ni tukio muhimu linaloonesha dhamira yake ya kukutana na wananchi na kuwasikiliza moja kwa moja kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29. Amefafanua kuwa Rais Samia amekuwa akipokelewa kwa shangwe na hamasa kubwa katika mikoa yote aliyoitembelea, hali inayoonyesha mapenzi makubwa ya wananchi kwake.

“Rais wetu amezunguka katika mikoa mingi na kila alipofika amepokelewa kwa furaha kubwa. Sasa anakuja Dar es Salaam, hivyo ni jukumu letu wakazi wa jiji hili kujitokeza kwa wingi kumpokea na kumuunga mkono katika kampeni zake ambazo zitafanyika katika maeneo ya Kinondoni,












Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top