Dar es Salaam
Ernest Sungura, Katibu Mtendaji wa MCT (Kulia), na Baraka Mgohamwende, Mkurugenzi Mtendaji wa UWEZO Tanzania, wakisaini makubaliano ya kushirikiana katika kuwawezesha waandishi wa habari kuandika habari za elimu kwa weledi, kwa kutumia ushahidi na kwa kuzingatia usawa wa kijinsia, Oktoba 1, 2025, jijini Dar es Salaam.
Habari bora za elimu zina mchango mkubwa katika kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii. Kwa kuzingatia hilo, makubaliano haya yanaweka mkazo katika uandishi jumuishi kwa kuhakikisha sauti za wasichana, makundi yaliyotengwa, na wanafunzi walioko katika mazingira hatarishi zinatambuliwa na kupewa nafasi katika vyombo vya habari. Wanaoshuhudia ni; Greyson Mgoi, Mkuu wa Mawasiliano wa Uwezo Tanzania, na Josephat Mwanzi, Meneja wa Programu wa MCT.











