Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Maua ya Alizeti Yavutia Masoko Ng'ambo


 
Na Mwandishi Wetu;Nairobi

ALIZETI ambayo kwa miaka mingi imekuwa ikitumika kama malighafi ya utengenezaji mafuta ya kupikia na kuunda chakula cha mifugo, maua yake sasa yameanza kushabikiwa kurembesha mazingira.

Yamegeuka kuwa kivutio kipya na kuorodheshwa miongoni mwa maua ya mapambo yanayouzwa ng’ambo.

Kenya, ikijivunia kuwa miongni mwa wazalishaji nguli wa maua duniani na kushikilia nafasi ya nne katika uuzaji wa maua hususan ya umaridadi, sasa inajumuisha alizeti kwenye orodha ya maua yenye ushindani mkuu sokoni.

Aghalabu, Kenya husafirisha asilimia 99 ya maua yake kwa zaidi ya nchi 80 ulimwenguni haswa aina ya waridi ‘rose’, carnation na alstroemeria. Alizeti sasa imejiunga rasmi na utandawazi huu wa maua ya kuvutia.

Alizeti sasa inakumbatiwa kama maua ya urembesho. Picha|Sammy Waweru

Ikiwa nyuma ya Colombia na Ecuador, katika nafasi ya tatu kimataifa kwa uzalishaji wa maua yaliyokatwa, Kenya inalenga kubadilisha sura ya maua yake kwa kuingiza maua ya kiangazi (summer flowers) yenye rangi ang’avu na matumizi mbalimbali, na alizeti inashirikishwa kwenye mageuzi haya.

Mbali na alizeti, maua mengine ya kiangazi ambayo yanaongeza upekee katika masoko ambayo Kenya inawahi ni pamoja na gypsophila, delphinium, limonium, snapdragons, matthiola incana, marigold, na lisianthus.

“Alizeti imekuwa ikijulikana kwa utengenezaji wa mafuta na chakula cha mifugo, lakini kutokana na utafiti tumezalisha aina mpya zinazoshabikiwa sokoni kama maua ya mapambo,” anasema Mildred Anyango, Mwakilishi wa Mauzo wa Ball SB ukanda wa Afrika Mashariki, kampuni ya kimataifa ya uzalishaji maua.

Ball SB, tawi la kampuni ya Ball Horticultural yenye makao yake makuu Chicago, Amerika, inashughulika na uzalishaji, upandikizaji na usambazaji wa miche kwa wakulima wa kitaalamu.

Mildred Anyango, Mwakilishi wa Mauzo wa Ball SB ukanda wa Afrika Mashariki akikagua mashada ya maua ya alizeti wakati wa Makala ya 13 ya Maonyesho ya Kimataifa ya Maua (IFTEX) 2025, yaliyofanyika Jijini Nairobi. Picha|Sammy Waweru

Anyango anaeleza kuwa ipatayo miaka mitano iliyopita, walitambua mwanya katika soko la maua ya mapambo, na wakajumuisha aina maalum za alizeti zilizobuniwa kwa ajili ya mashada na mapambo ya kifahari.

“Awali, mashada ya maua yalitawaliwa na waridi. Lakini sasa, maua ya alizeti yanachangia kuboresha rangi, haiba, na kuleta furaha ya kipekee,” anasema Anyango.

Tofauti na alizeti za kawaida zenye kichwa kikubwa kwa ajili ya mafuta, aina za mapambo zimezalishwa kwa minajili ya muonekano—zikiwa na rangi mbalimbali na muundo wa petali (petals) wa kuvutia.

Miongoni mwa aina maarufu ni Ziggy, yenye petali mbili zenye rangi mseto, Marley – yenye rangi mbili pia na mvuto wa kipekee, Carnival Sun yenye maua makubwa yenye petali nyingi, Pro-cut Red yenye petali nyekundu za kuvutia, na Vincent Fresh – aina isiyo ya kawaida yenye kitovu cha kijani.

Alizeti maridadi ya rangi ya manjano. Picha|Sammy Waweru

“Aina hizi si tu nzuri kwa macho, bali pia ni rahisi kusafirisha, hudumu kwa muda mrefu (ikilinganishwa na maua mengine) na hazichukui nafasi kubwa kwenye ndege (freight),” Alisema Anyango kwenye mahojiano ya kipekee.

Ball SB ilikuwa miongoni mwa kampuni zinazozalisha maua, kujamiisha, za kupandikiza, kusafirisha ng’ambo, na wadauhusika wengine waliohudhuria Makala ya 13 ya Maonyesho ya Kimataifa ya Maua (IFTEX) 2025, yaliyofanyika Jijini Nairobi, kuanzia Juni 5.

Baadhi ya wazalishaji wa Kenya tayari wanasafirisha aina hizo mpya za alizeti kwa masoko ya ughaibuni kama vile Ulaya na na nchi za Uarabuni za Mashariki ya Kati, ambayo ni masoko ya jadi ya maua ya Kenya. Soko vilevile limepanuka hadi Asia Mashariki.

Kulingana na Clement Tulezi, Afisa Mkuu Mtendaji wa Baraza la Maua Kenya ‘Kenya Flower Council’, ongezeko la maua ya kiangazi kama vile alizeti linachangia ukuaji wa sekta hii.

Kulingana na Mildred Anyango kutoka Ball SB alizeti inatumika kupiga jeki maua mengine kwenye mashada. Picha|Sammy Waweru

“Tunaendelea kushuhudia ongezeko la masoko mapya Barani Asia na maeneo mengine ya Ulaya,” Tulezi anasema.

Isitoshe, kuna mabadiliko jinsi maua yanavyosafirishwa—wazalishaji sasa wakiandaa mashada tayari kwa matumizi ya moja kwa moja sokoni badala ya kusafirisha yakiwa maua ghafi.

Tulezi anasema hatua hiyo inaongeza thamani kwenye maua, na kuvutia soko la ndani kwa ndani Kenya ambalo kwa muda mrefu halijakuwa la kuridhisha.

“Ingawa kiwango cha matumizi ya maua humu nchini bado ni cha chini, baadhi ya wapenzi wa maua wameonyesha kuvutiwa na yale ya alizeti,” Anyango anakiri.

Anahimiza haja ya Wakenya kufurahia mashada ya maua, kama inavyoshuhudiwa Ulaya. Alizeti za mapambo pia ni rahisi kulima, na zinakomaa kwa muda mfupi – karibu miezi miwili. Kwa wenye chanzo cha maji, wanakuza mfululizo hivyo basi kudumisha wanunuzi.

Maua maridadi, yakiwemo ya alizeti ambayo Ball SB huzalisha mbegu na miche yake kwa minajili ya ukuzaji kuwahi masoko ya ng’ambo. Picha|Sammy Waweru

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...