Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali Itamuenzi Mhandisi Nyamo-hanga


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko leo tarehe 16 Aprili, 2025 amewaongoza waombolezaji katika mazishi ya Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mhandisi Boniphace Gissima Nyamohanga yaliyofanyika katika eneo la Mikungani, Wilaya ya Bunda. 

Akizungumza katika mazishi hayo, Mhe. Biteko amesema Mhandisi Nyamohanga alikuwa ni hazina kubwa ya mipango inayopimika ndani ya Serikali na amefanya kazi kubwa ndani ya TANESCO, REA na Wizara ya Nishati kwa ujumla. 

Mhe. Biteko amesema kazi kubwa alizozifanya kuwa ni pamoja na ukamilishaji wa mradi wa Bwawa la kuzalisha umeme la Nyerere na uanzishaji na utekelezaji wa mpango wa Tanzania kuanza kuuza umeme katika nchi ya Zambia.  

“Sahihi yake aliyoiweka wakati wa kufunga mkataba kati ya Tanzania na Zambia itaendelea kuwepo katika mkataba huo muda wote kutukumbusha Kazi kubwa aliyoifanya Mhandisi Nyamohanga katika sekta ya Nishati” amesema Mhe. Biteko. 

Naibu Waziri Mkuu amesema wakati Mhandisi Nyamohanga anateuliwa Shirika lilikuwa lipo katika wakati mgumu sana na kelele za umeme zilikuwa nyingi hapa nchini lakini ametatua tatizo la umeme na kujenga umoja na mshikamano baina ya watumishi wa TANESCO.  

Mhe. Biteko amesema Mhandisi Nyamohanga alikuwa anawatetea na kuwapenda watumishi wake na wakati wote likitokea tatizo alikuwa anasema “wape muda watajirekebisha” amesema Mhe. Biteko na kuongeza kuwa marehemu alikuwa tayari kubeba lawama mbalimbali ili kuwasaidia watumishi wake. 

Mhe. Biteko ametumia fursa hiyo kuwaasa waombolezaji wakiwemo viongozi na watendaji kuwa katika maisha yao waige mfano wa Mhandisi Nyamohanga na kuwa baraka ya kuwasaidia wengine na sio kuwa kama kitunguu kusababisha vilio kwa watu wanaomzunguka. 

Mhe. Biteko amewataka wanafamilia ya Mhandisi Nyamohanga pamoja na wajane wawili wa marehemu kushikamana, kupendana na kuishi kwa umoja na amani kama wakati ambapo marehemu alipokuwa hai ili waweze kuendeleza maono ya marehemu katika maisha yao.  

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Alfred Mtambi amesema Mhandisi Nyamohanga alikuwa ni mdau muhimu sana katika Maendeleo ya Mkoa wa Mara na amekuwa akitoa ushirikiano mkubwa kwa viongozi wa Mkoa wa Mara. 

“Mhandisi Nyamohanga amefariki akiwa njiani pamoja na mambo mengine alikuwa anakuja kukagua na kuona namna ya kupeleka umeme katika Shule ya Amali ya Mkoa wa Mara inayoendelea kujengwa katika Wilaya ya Butiama” amesema Mhe. Mtambi. 

Akizungumza katika mazishi hayo, Mhe. Mtambi ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara na Mkoa wa Kipolisi wa Tarime Rorya kuongeza operesheni na watu wote wanaokiuka taratibu za usalama barabarani wachukuliwe hatua za kisheria. 

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka viongozi, watumishi na wananchi kuiga mfano wa Mhandisi Nyamohanga kwa kuchapa kazi kwa bidii na kutatua kero za wananchi.  

Kwa upande wake, Msemaji wa Familia ya Nyamohanga ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) Mhe. Mwita Gachuma ameishukuru Serikali kwa uratibu mzuri wa mazishi ya Mhandisi Nyamohanga tangu msiba huo ulipotokea tarehe 13 Aprili, 2025.

Mhe. Gachuma ameiomba Serikali kusaidia kujenga jengo kwa ajili ya kumkumbuka Mhandisi Nyamohanga katika eneo hilo alipozikwa. 

Nae Mbunge wa Musoma Vijijini Prof. Sospiter Muhongo ambaye aliwahi kufanya nae kazi amesema Mhandisi Nyamohanga ni mmoja wa waanzilishi wa bei ya umeme ya 27,000 inayotumika hapa nchini kwa ajili ya kuunganishia umeme wa gharama nafuu na kuiwezesha Tanzania kuingia katika mradi wa Kimataifa wa Power Africa. 

Prof. Muhonga ameiomba Serikali kumuenzi Mhandisi Nyamohanga na kutambuliwa kama mwanzilishi wakati wa tathmini ya mradi wa Power Africa itakayofanyika Juni, 2025 ili kukumbuka mchango wake mkubwa alioutoa katika Sekta ya Nishati.

Mhandisi Nyamohanga na dereva wake Ndugu Mujahir Mohamed Haule walifariki katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia tarehe 13 Aprili, 2025 katika Kata ya Nyatwali, jirani na geti kuu la Hifadhi ya Taifa ya Serengeti lililopo eneo la Ndabaka, Wilaya ya Bunda na dereva wake alizikwa tarehe 14 Aprili, 2025 katika Mkoa wa Pwani. 

Marehemu Nyamohanga alizaliwa mwaka 1969 na amefariki akiwa na umri wa miaka 56 na kuacha wajane wawili na watoto 15 na wajukuu watano na katika uhai wake alisomea Uhandisi na baadaye  kujiendeleza katika fani za Sheria na Usimamizi wa Biashara.








Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...