George Michael Uledi.
Waziri Mkuu wa JMT Mh Kassim Majaliwa Majaliwa ni kama amekoleza tena mjadala wa "wasomi" kwenda kujiunga VETA kwa ajili ya kozi za Muda mfupi lakini zenye soko kubwa la ajira kwa sasa!
Mh Waziri Mkuu Majaliwa alishangaliwa mara kwa mara na washiriki wa Mkutano huo wa maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwa mamlaka hiyo Nchini!(VETA).
"..tutumie vizuri maadhimisho haya ambayo yamekuja wakati huu kuna mjadala muhimu wa umuhimu wa mafunzo ya VETA kwa "Wasomi " Nchini..." Waziri Mkuu alisisitiza!
Tangu Waziri Mkuu kuja na MAONO hayo ya jinsi VETA inavyoweza kupunguza tatizo la ajira kwa "wasomi" wenye Shahada na kuendelea Nchini, kumejitokeza Vijana mbalimbali wenye Elimu ya Shahada na kuendelea ambao wamekuwa wakitoa ushuhuda wa jinsi walivyoweza kujiunga na mafunzo ya VETA na sasa wanafanya shughuli zao mbalimbali ambazo zinawapa kipato kikubwa kuliko ajira za kawaida(ajira za Degree).
VETA SASA KUTEMBEA NA MAONO YA MH WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA!👇🏿👇🏿
Kama VETA itaweza kuanzia sasa kuvutia wahitimu mbalimbali wa Shahada za Vyuo Vikuu na kuendelea basi ni wazi kuwa wataweza kuongeza "thamani" ya taasisi yao na hivyo kuondoa dhana kwamba VETA ni kwa ajili ya watu wenye Elimu ya kawaida!
MAONO haya ya Mh Waziri Mkuu yamekuja wakati Taifa lipo katika "crisis" kubwa ya ajira Nchini wakati huo VETA ikiwa na fursa nyingi za ujuzi ambao unahitajika sana mitaani kwa sasa na wenye kuvuna fedha nyingi!
Idara ya Elimu, Mawasiliano na Masoko ya VETA kama ipo inapaswa kuja na mkakati Maalum wa Elimu kwa Vijana wa ngazi ya Shahada ili waweza kujua fursa zilizopo ndani ya programu za VETA,fursa zilizopo kwenye soko la ajira kwa sasa zenye kuhitaji wahitimu wa VETA na vipato ambavyo vijana waliopita VETA wanapata kwa siku/mwezi ukilinganisha na wahitimu wa kada kama ya WALIMU wa Degree!
USHAURI MWINGINE KUTOKA KWA MH WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KWENDA VETA LEO!👇🏿👇🏿
Mh Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka VETA sasa kuja na MTAZAMO Maalum wa aina mbili katika kutengeneza programu zao za (I)Programu za kuweza "kumeet demands" ya soko na (II)programu za kuweza "kubeat demands" ya soko husika!Mh Waziri Mkuu ametoa darasa hilo kwa kusema ni muhimu sana VETA wafanye tafiti mara kwa mara kuhusu mahitaji ya "soft market" ya bidhaa na huduma Gani ambazo zitazalishwa na VETA zitakuwa na soko sana miaka ya 2030 hadi 2035 kufuatana na mabadiliko ya teknolojia na mahitaji ya binadamu wa miaka hiyo!
Mh Waziri Mkuu Majaliwa amesisitiza kuwa Programu hizo za masomo ya ufundi zinapaswa zianzishwe sasa kwa ajili ya mahitaji ya mbele(Programs which beat demands).
Kongamano hilo la miaka 30 ya VETA limefanyika leo katika UKUMBI wa JNCCC huku Mh Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa mgeni RASMI!

.jpg)
.jpg)
.jpg)
Comments
Post a Comment