Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

CV ya Dkt. Nchimbi imeshiba Mno, anatosha Kwenda Kuwa Msaidizi wa Kwanza wa Rais Samia




Na Bwanku M Bwanku.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinachoongoza Taifa Tanzania kimekua na wiki ya aina yake kuanzia Jumamosi na Jumapili Januari 18 na 19, 2025 kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

CCM imekua na Mkutano Mkuu wake Maalum ambao ulikua na ajenda mbalimbali kubwa ikiwa kumchagua Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho baada ya aliyekua akishika nafasi hiyo Ndugu Abdulrahman Kinana kujiuzulu, hatimaye Ndugu Stephen Masatu Wasira akachaguliwa kuziba nafasi hiyo.

Kwenye Mkutano Mkuu huu Maalum licha ya ajenda zake Mama zilizokua zinajulikana na shughuli zilizofanyika kama hiyo ya kumchagua Makamu Mwenyekiti, kupokea taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Chama na mabadiliko madogo kwenye Katiba yake, kumpitisha Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Mgombea Urais wa CCM na Dkt. Hussein Mwinyi kuwa Mgombea Urais wa CCM Zanzibar, Mkutano huu umefanya jambo lingine kubwa ambalo halikutarajiwa na yeyote na kutikisa Taifa wakati huu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu hapo baadae.

Kwa mshangao mkubwa, bila kujulikana wala kutarajiwa na yeyote, hatimae Mkutano Mkuu huu umemthibitisha Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza wa CCM wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2025.


Hili linatokea baada ya Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango na ambaye alitarajiwa kuwa Mgombea Mwenza wa Dkt. Samia kwenye Uchaguzi Mkuu kuomba na kuandika barua kwa Rais Samia ya kupumzika na hatimaye ndani ya Mkutano huo kikafanyika kikao cha haraka haraka cha Kamati Kuu ya CCM ambacho kilikuja na jina la Dkt. Nchimbi na Mkutano Mkuu kumthibitisha papo hapo. Hakuna aliyetarajia, Taifa limepata mshangao mkubwa sana. 

Imekua ghafla na historia bila ya kutarajiwa na yeyote CCM kwenye Mkutano Mkuu wake huu ambao hata haukua na ajenda hiyo kumpata Mgombea Mwenza atakayesimama na Rais Samia kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka huu 2025 ambaye ni Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi.


Sasa, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ni nani?

Jina la Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi sio jina geni kwenye anga la siasa za Tanzania. Ni moja ya wanasiasa wakubwa, mahiri na wakongwe wanaoendelea kuteka uga huu wa siasa za Tanzania. 

Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi ni moja ya wanasiasa wakubwa sana kwenye siasa za Tanzania. Kwa utumishi na uzoefu wake mkubwa ndani ya CCM na serikali akiwa na zaidi ya miaka 35 akishika nafasi kubwa na nyeti za maamuzi.

Ndiye Katibu Mkuu wa CCM kwasasa, Chama kinachoongoza Taifa hili.
 
Ameshika nafasi mbalimbali kwenye ngazi za chini na za msingi za CCM, akiwa Chuo mwaka 1997 alichaguliwa kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na mwaka mmoja mbele 1998, alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Jumuiya aliyoiongoza mpaka mwaka 2008. Pia amewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda iliyoko mkoani Mara wakati wakati wa Awamu ya 3 ya Hayati Benjamin Mkapa kuanzia mwaka 2003 hadi 2005.

Kuwa Kiongozi Mkuu wa Jumuiya hiyo ya Vijana kwa ngazi ya Taifa, moja kwa moja kukampa tiketi ya kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Halmashauri Kuu (CC & NEC). Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM ni moja ya vikao vya juu kabisa vitatu vya CCM kando ya Mkutano Mkuu wa CCM Taifa ambavyo vinafanya maamuzi makubwa ndani ya Chama hicho ikiwemo kumpitisha Mgombea Urais wa CCM, Mwenza, Wabunge lakini vikiwa ni vikao vinavyojadili hali ya CCM na utekelezaji wa Ilani yake na serikali na mengine mengi makubwa yanayogusa maslahi ya Taifa zima. 

Baada ya kuhudumu kwenye nafasi kubwa ndani ya Chama na zenye maamuzi makubwa ndani ya Chama na Taifa, Mwaka 2005 Dkt. Nchimbi aligombea Ubunge kwenye Jimbo la Songea Mjini na kushinda ambapo moja kwa moja Rais wa Awamu ya 4 wa kipindi hicho Dkt. Jakaya Kikwete alimteua kuwa Naibu Waziri kwenye Wizara 3 akianza kuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo kuanzia Januari 2006, kisha Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana mwaka huohuo Oktoba pamoja na Naibu Waziri wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa alikohudumu kuanzia Februari 2008 hadi 2010 kwenye Uchaguzi Mkuu. 

Mwaka 2010 aligombea tena na kushinda na hapo sasa Rais wa Awamu ya 4 Dkt. Jakaya Kikwete akamteua kuwa Waziri kamili akianza kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo na baadae Waziri wa Mambo ya Ndani.

Mwaka 2016, Dkt. Nchimbi aliteuliwa na Aliyekuwa Rais wa Awamu ya 5 Hayati John Magufuli kuwa Balozi wa Tanzania nchini Brazil kabla ya baadae mwaka 2022 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kumbadilishia Kituo cha kazi ya Ubalozi kwa kumteua kuwa Balozi wa Tanzania nchini Misri, nafasi aliyohudumu mpaka mwaka Jana 2023 alipomaliza muda wake na kurudi nchini kwa mujibu wa sheria.

Baada ya kazi kubwa akianzia ngazi za chini za uongozi, Uenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Taifa (UVCCM), Mbunge, Naibu Waziri hadi Waziri kamili na Ubalozi hatimaye Januari 15, 2024 Dkt. Nchimbi aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Mtendaji Mkuu wa Chama hiki kinachoongoza Taifa letu Tanzania

Anasifika kwa misimamo madhubuti isiyoyumba (hili nitalichambua) akiwa na ushawishi mkubwa ndani ya Chama na Nje hasa kwa kufanya kazi ndani na Nje ya Nchi. 

Kwa CV yake hii ilivyoshiba akishika nafasi kubwa na nyeti akianzia ngazi za chini, ni mtu madhubuti kuweza kuwa msaidizi namba moja wa Mkuu wa Nchi.

Ni ukweli usiopingika kwamba kwa Rais kariba ya Dkt. Samia anayefanya mageuzi makubwa ya maendeleo ndani ya nchi anahitaji kuwa na wabobezi wakubwa wa siasa na utumishi kumsaidia kutafsiri maono yake.


Balozi Nchimbi ni Msomi mzuri aliyebobea kwenye masuala ya Fedha na Benki akihitimu Shahada ya Uzamivu (PHD) kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe mwaka 2011.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...