Waziri Mkuu amesema Rais amefanya mabadiliko makuba katika Sekta saba muhimu za kijamii

GEORGE MARATO TV
0

 

Waziri mkuu mh Kassim Majaliwa,amesema Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ameweka mikakati mikubwa katika utekelezaji wa miradi saba inayowagusa wananchi kila kukicha na kutoa fedha nyingi za utekelezaji wake na kuvunja rekodi katika historia ya nchi yetu na hivyo kuvuka yale yaliyopangwa katika ilani ya uchaguzi ya CCM.


Mh waziri mkuu ametaja miradi ambayo mh Rais Dkt Samia ameweka mkakati wa utekelezaji wa ilani mh Rais ameweka mkakati wa utekelezaji wake na kuongeza bajeti ni pamoja na miradi afya,ujenzi barabara wa moundo mbinu ya barabara na nishati ya umeme huku sekta za uvuvi na kilimo yakiendelea kupewa kipaumbele zaidi kwa serikali ya awamu ya sita.


Waziri mkuu ameyasema hayo wakati akikagua mradi wa ujenzi wa tenki la maji eneo la Bujora, ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 93 na kwamba ujenzi wake ukikamilika utawezesha wananchi wa kata za Bujora, Kisesa na Bukandwe, yakiwemo maeneo ya wilaya ya Ilemela kupata maji safi na ya uhakika kutoka ziwa Victoria.

Amesema kuwa katika miradi ya maji,Rais Samia ameweza kuongea bajeti kubwa ili kuhakikisha miradi yote inatekelezwa na kukamilika kwa wakati.

Kuhusu sekta ya elimu,waziri mkuu amesema Rais Samia amendelea kuwezesha kila mtoto wa kitanzania anapata elimu kuanzia msingi hadi kidato cha sita bila kulipa ada na kwamba ameongeza fedha nyingi katika bajeti ya elimu katika mikopo ya elimu ya juu.



Waziri mkuu akizungumzia sekta ya afya,amesema Serikali ya awamu ya sita imehakikisha kila halmashauri inajenga hospitali yenye hadhi ya wilaya huku maboresho makubwa yakifanywa katija hospitali za mikoa na rufaa ikiwa ni pamoja na ununuzi wa dawa na vifaa tiba.

Katika sekta ya uvuvi katika ziwa victoria,waziri mkuu amesema kuwa hivi sasa Rais Samia ameweka mpango mkubwa ununuzi wa boti na nyavu hatua ambayo inalenga kufanya mabadiliko makubwa katika sekta ya uvuvi wa kutumia vizimba na kwamba mpango mkubwa inawekwa kuongeza zana hizo za uvuvi na kuzigawa kwenye vikundi vya vijana.


Waziri mkuu amesema katika sekta ya Kilimo serikali chini ya Rais imeweka mikakati mikubwa katika kuinua sekta ya kilimo ikiwa ni pamoja kuongeza mazao ya biashara na chakula huku akisema Tanzania itakuwa eneo muhimu linalotegemewa katika uzalishaji wa chakula Afrika.

Hata hivyo mh waziri Majaliwa amesema kuwa kwenye sekta ya nishati ya umeme Rais Samia amefanya kazi kubwa ya kusambaza nishati hiyo katika vijiji vyote nchini na baadhi ya maeneo nishati hiyo sasa inasambazwa ngazi ya vitongoji kwa gharama elfu 27 tu kwa maeneo ya vijijini. 

Kuhusu miundombinu ya barabara waziri mkuu amesema Serikali ya awamu ya sita ipeleka fedha nyingi kwa wakala wa barabara nchini Tanroads na ule wakala wa barabara vijijini na kwamba kazi kubwa inafanyika katika ujenzi wa miundombinu hiyo.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top