Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Wawekezaji Wakaribishwa Kagera


 

*📌 Dkt. Biteko asisitiza teknolojia itumike uchakataji zao la ndizi*

*📌Dkt. Biteko ahimiza uwekezaji viwanda vya kuongeza thamani mazao ya uvuvi na ufugaji*

*📌 Kagera yaongoza kwa uzalishaji zao la ndizi nchini kwa asilimia 60*

*📌 Mradi wa Mashamba Makubwa ya Kahawa Kagera kunufaisha watu 10,000*


*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*

Wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi wamekaribishwa kuwekeza mkoani Kagera kufuatia hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi ambazo mkoa wa huo umefikia ikiwa ni pamoja na mipango ya maendeleo na fursa nyingi za uwekezaji zilizopo. 

Mkoa wa Kagera ni wa pili kwa uzalishaji wa samaki na fursa ya uvuvi nchini ukitanguliwa na Mkoa wa Mwanza fursa ambayo inawanufaisha wakazi wake kwa kuwapatia ajira, lishe bora, kipato na maendeleo ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa makazi bora kutokana na shughuli za uvuvi.

Akizungumza Desemba 19, 2024 katika Uwanja wa Kaitaba wilayani Bukoba mkoani Kagera wakati aliposhiriki katika Tamasha la Pili la Uwekezaji la mkoa huo ikiwa sehemu ya Wiki ya Tamasha la Ijuka Omuka (Kumbuka Nyumbani), Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa wananchi wa mkoa huo kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vya kuongeza thamani mazao ya uvuvi, viwanda vya kutengeneza zana za uvuvi kama nyavu, kamba, vifaa vya kujiokolea na mashine za boti badala ya kuagiza vifaa hivyo kutoka nje ya nchi.

Dkt. Biteko amesema kuwa Mkoa wa Kagera unaongoza kitaifa kuwa na ranchi 6 za mifugo kati ya ranchi 15 zilizopo nchini. Ametaja ranchi hizo kuwa ni Missenyi, Mabale, Kikulula, Mwisa II, Kitengule na Kagoma. 

Ameendelea kusema kuwa mkoa huo kupitia halmashauri zake zote umetenga jumla ya hekta 345,430.97  kwa ajili ya malisho ya mifugo ambapo uwepo wa maeneo hayo ya malisho na ufugaji yanatoa fursa kubwa ya uwekezaji kwa kuanzisha ufugaji wa kisasa wa ng’ombe wa nyama na maziwa ili kuvutia uanzishwaji wa viwanda vya kuchataka nyama na maziwa hasa katika maeneo yenye ranchi za Taifa.

“ Naiona Kagera inakwenda kukua kwa kasi kubwa sana na nitumie fursa hii kuwaomba na kuwaalika wawekezaji kote nchini na nje ya nchi kuja kuwekeza Kagera kutokana na fursa zilizopo kwani mazingira ya uwekezaji ni mazuri na uongozi wa mkoa umejipanga vyema kuwapokea na kuwahudumia kwa viwango,” amesema Dkt. Biteko 

Ameongeza kuwa Mkoa wa Kagera pia unaongoza kwa uzalishaji wa zao la ndizi kwa wastani wa tani milioni 2.4 kati ya tani milioni 3.6 zinazozalishwa  sawa na asilimia 60 ya uzalishaji wa zao hilo nchini. Kwa wastani zao la ndizi mkoani humo linawaingizia wakulima kati ya shilingi bilioni 240 – 300 kwa mwaka, hivyo kuwa na mchango mkubwa katika uchumi wa mkoa na Taifa kwa ujumla. 

Pia, Dkt. Biteko amesema bado ipo fursa ya kuwekeza kwenye teknolojia na miundombinu ya uchakataji wa zao la ndizi ili kuongeza thamani na kuzalisha bidhaa nyingine zinazotokana na zao la hilo.

“Ninafahamu kwamba, mkoa umebuni na kuanzisha mradi wa Mashamba Makubwa ya Kahawa yenye ukubwa wa ekari 10,000. Mradi ambao unalenga kuwanufaisha watu wapatao 10,000 wakiwemo vijana na utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2024 – 2027. Kwa kuanzia tayari shamba lenye ukubwa wa ekari 400 katika Kijiji cha Makongora wilayani Muleba ambapo kila kijana amegawiwa ekari moja ya shamba lililoandaliwa na kupewa miche bure,” amesema Dkt. Biteko.

Aidha, lengo la mradi huo likitajwa kuwa ni kuongeza ajira kwa vijana, pato la mtu mmoja na pato la mkoa pamoja na kuongeza pato la halmashauri kupitia ushuru wa zao la kahawa na kuliingizia Taifa fedha.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mhe. Fatma Mwassa amesema kuwa Tamasha la Ijuka Omuka (Kumbuka Nyumbani), limelenga kuwakutanisha pamoja wakazi wa Kagera na kuibua fursa za uwekezaji mkoani humo.

Amesema kuwa kupitia tamasha hilo wanautangaza Mkoa wa Kagera licha ya kutokuwepo kwa jitihada za kufanya hivyo hapo awali ili wananchi wa mkoa huo kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi kuvutiwa na fursa zilizopo na kwenda kuwekeza katika sekta mbalimbali.

Tamasha la Ijuka Omuka 2024 limeanza Desemba 18, 2024 na linatarajiwa kuhitimishwa Desemba 21, 2024. Tamasha hilo limesheheni matukio mbalimbali  ikiwemo maombezi kwa Mkoa wa Kagera na Taifa, Kongamano la Uwekezaji, maonesho ya biashara, tamasha la utamaduni, maonesho ya mavazi ya asili, mashindano ya pikipiki na mechi kabambe ya mpira wa miguu Desemba 21, 2024 kati ya Klabu ya Simba na Kagera Sugar katika Uwanja wa Kaitaba mkoani humo.







Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...