Naibu Waziri mkuu na waziri wa nishati Dk Dotto Biteko amewataka wanakagera walioko ndani na nje kuendelea kuwaunga mkono wawekezaji waliowekeza na wanaotaka kuwekeza ili kuendelea kuinua uchumi wa mkoa huo wenye fursa nyingi za uwekezaji.
Amesema hayo wakati wa jukwaa la uwekezaji mkoani Kagera ampo ni mwendelezo wa wiki ya tamasha la IJUKA OMUKA ambalo linawahimiza wazawa wa Mkoa wa Kagera kurudi nyumbani na kuwekeza ili kuchochea uchumi wa mkoa huo pamoja na kuongeza ajiran kwa wananchi wake husa vijana.
"Najua Kuna wawekezaji wengi wanataka kuja lakini maneno ya kukatisha tamaa huwa hayaishi ,na vikwazo ,kama tutaondoa vikwazo na kuwaunga mkono mkoa wa Kagera utabadilika kwani Fursa nilizozisikiliza hapa zikitajwa na mkuu wa mkoa na viongozi wake ni nyingi sana"ameeleza Biteko
Amesema mkoa huo unafursa nyingi kutokana na kuzungukwa na nchi za Afrika Mashariki.
Kwa upande wake Waziri wa mambo ya ndani Inocent Bashungwa amesema wataendelea kushirikiana na mkuu wa mkoa huo ili kuhakikisha wanasukuma mbele mamaendeleo ya mkoa huo huku akiishukuru Serikali na wawekezaji kuendelea kuwekeza Kagera.
Mkuu wa mkoa wa Kagera Fatuma Mwasa amesema kuwa wawekezaji ni wakati wao sasa kuja kuwekeza mkoani humo kwani jografia ya mkoa huo soko ni kubwa kutokana na kupakana na nchi zenye idadi kubwa ya watu wanaojihusisha na biashara mbali mbali wanaopkuja na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera.
Amesema tamasha hilo limezaaa matunda mbali mbali ikiwa ni kuanzisha viwanda vipya na mkoani humo pamoja na mambo mengi ya kinaendelea
Amesema sehemu kubwa iliyopoteza mapato ya mabilioni mkoani Kagera ni sehemu ya uvuvi ambayo haina uwekezaji wa kutosha kwani mvua kubwa inaathiri ukaushaji wa dagaa na wanahoifadhi dagaa wengi wanahoifadhi kwa unyevu nyevu hivyo hali sio nzuri na mabilioni ya fedha yanapotea.
"Amesema matamanio yake ni kuona tunaanzisha ufugaji wa vizimba vya dagaa na Samaki ,naangalia magarini kwenye magara dagaa wamehifadhiwa vibaya na wanunuzi wakubwa ni wafanyabiashara kutoka Rwanda ,natamani sana tuanzishe na tuwekeze katika eneo la Kukausha dagaa na kufunga Samaki wa vizimbo tutapata fedha nyingi sana.
Baadhi ya watalaam wa uwekezaji akiwemo Mhandisi Emmanuel Manyanda kutoka wakala wa barabara mjini na vijijini amesema kuwa usanifu wa miradi ya kimkakati ya stendi,kingo za mto Kanoni pamoja na soko la kisasa umekamilika na hivi karibun wakazi wa mkoa wa Kagera wataona matunda yake .
Kwa upande wa mkurugenzi wa kuendeleza kilimo Tanzania Daktari John Kyaruzi alisema kuwa mradi wa uwekezaji wa vizimba mia nne hamsini tayari umepata muwekezaji kutoka Nchini Marekani wakati mhadhiri wa chuo kikuu Cha sokoine Daktari Philmon Nyinondi akisema tayari taasisi ya tume ya sayansi COSTEC wametenga fedha Kwa ajili ya utafiti wa njia Bora ya uvunaji wa senene.
Tamasha hili la ijuka omuka limebeba neno la kihaya lenye maana ya kumbuka nyumba ambao limeandaliwa na ofisi ya mkuu wa mkoa huo pamoja na wadau wa maendeleo mkoani humo lengo likiwa ni kuwataka wazawa wa Kagera kukumbuka nyumbani na kuwekeza ili kuinua mkoa wa Kagera kiuchumi.