Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rc Mtambi Aongoza Majadiliano ya Uelekeo wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025-2050




MKUU wa mkoa wa Mara  Kanali Evans Mtambi ameongoza majadiliano yaliyohusisha wananchi na viongozi kuelekea maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2026-2050.

Akizungumza kwenye kikao maalum cha kamati ya ushauri ya mkoa ( RCC ) kilichofanyika agosti 19 kwenye ukumbi wa uwekezaji amesema tayari majadiliano hayo yamefanyika ngazi ya wilaya na sasa ni mkoa kabla ya kupelekwa maoni ngazi ya taifa kwenye tume ya mipango.

Amesema Dira ya Taifa ya Maendeleo ni suala la msingi katika masuala mbalimbali hivyo mkoa unayo nafasi kwa wananchi na viongozi kujadiliana

Mtambi amesema lengo la kikao hicho ni kutoa fursa kwa wananchi na viongozi wa mkoa wa Mara kutoa maoni yao kuhusu Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050 ambayo ipo katika hatua za maandalizi. 

“Dira inaonyesha matamanio na vipaumbele vya wananchi,serikali na taasisi binafsi zinapo tamani kufikia kwa muda flani na mipango mbalimbali inawekwa ili kufikia lengo hilo”

 Mchakato wa maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 ulizinduliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango April, 2024 mkoani Dodoma ns Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan hivi karibuni amezindua ushirikishwaji wa wadau wote kutoa maoni" Amesema. 

Kanali Mtambi amesema Tume ya Mipango imewasilisha katika Mkoa wa Mara maelekezo ya namna ya kukusanya maoni, mapendekezo na ushauri ili wananchi, viongozi na taasisi zitoe maoni kwa ajili ya dira mpya ya maendeleo ya Taifa kwa miaka 25 ijayo. 

Amesema kwa kawaida Nchi inakuwa na mipango ya muda mrefu, muda wa kati na muda mfupi na utekelezaji wake unaweza kulitoa taifa kutoka katika eneo moja kwenda eneo lingine.

Mkuu huyo wa mkoa  amesema anatamani katika mipango ya miaka ijayo reli ya kisasa ya SGR iwe imefika mkoa wa Mara kutokea Arusha au Mwanza ili kurahisisha usafiri kwa watu na mizigo kutoka katika mkoa wa Mara na kuinua uchumi.

Akizungumza katika kikao hicho Naibu Waziri wa Sheria na Katiba  Jumanne Sagini amesema mkoa wa Mara umepiga hatua kubwa katika miundombinu ya barabara ambapo hapo awali wananchi walikuwa wanatumia zaidi usafiri kupitia nchi za Kenya na Uganda wakati wa kwenda Dar es Salaam na mikoa mingine. 

 Sagini ameshauri mkoa utilie mkazo kuhusu urejeshaji wa bandari ya Musoma ili iweze kufanya kazi kuunganisha na treni ya SGR ambayo inatarajiwa kufika mkoa wa Mwanza na hivyo itasaidia katika usafirishaji wa mizigo na kurahisisha upatikanaji wa bidhaa. 

Naibu Waziri huyo amesema tayari serikali imeshajenga meli nyingi na inaendelea kujenga nyingine na hivyo inawezekana bandari ya Musoma ikifufuliwa itasaidia katika kuimarisha usafiri wa mizigo na kuvutia wawekezajai zaidi katika Mkoa wa Mara. 

Mhe. Sagini amesema katika sekta ya elimu nchi imepiga hatua kubwa sana tumepanuka sana, walimu wapo wachache, walimu na wazazi tunaowajibu kuhakikisha wanafunzi wanasoma. 

 Mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini Profesa Sospeter Muhongo amesema wakati taifa linatoa maoni ni vizuri wataalamu wa mipango wakajiuliza wakati huo Dira inapotekelezwa Tanzania itakuwa na watu wangapi, dunia pia itaakuwa na watu wangapi ili kupanga mipango yenye uhalisia.  

Prof. Muhongo amesema katika mwaka wa 2050 Tanzania inakadiriwa kuwa na watu milioni 120 hadi 141ambao ni zaidi ya mara mbili ya watu waliopo sasa na mipango yote inatakiwa kuwekwa kwenye mahesabu watu hao ili Tanzania isipange mipango kwa ajili ya watu wachache wakati inakadiriwa kutakuwa na watu wengi. 

Amesema idadi ya watu ni muhimu kwa ajili ya kuangalia maendeleo tunayoyahitaji ni kwa ajili ya kuhudumia watu wangapi na kama mipango ya Taifa inaendana na idadi hiyo ya watu wanaotegemewa kuwepo wakati huo. 

Ametolea mfano wa umeme na kusema kuwa kwa sasa umeme unatosheleza kwa kuwa bado idadi ya watu na viwanda na maofisi ni ndogo ukilinganisha na wakati huo na kutahadharisha kuwa ili kuwa na umeme wa uhakika wa wakati huo ni lazima kuangalia mahitaji halisi ya umeme kwa wakati huo na sio hali ya sasa hivi tu. 

Aidhavwashiriki wengi wamepongeza maendeleo yaliyofikiwa katika sekta mbalimbali hapa nchini na kuitaka serikali kuendelea kuimarisha utendaji kazi katika utumishi wa umma ili maendeleo yaweze kufikiwa kiurahisi zaidi.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...