Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Fahamu Ubunifu wa Majiko ya Solar Yenye Uwezo wa Kupika Chakula cha Wanafunzi Zaidi 600 Katika Shule Moja Nchini Tanzania



Na Emmanuel Chibasa


👉Ni teknolojia Yenye Kuleta Suluhisho ya Kupunguza Matumizi ya Kuni na Mkaa Katika Taasisi za Elimu

👉Inawezesha kupika ugali, Maharage,Makande pamoja na wali Kwa ajili ya chakula cha wanafunzi wengi na wafanyakazi kwa haraka zaidi pamoja na kupunguza gharama za matumizi.


Katika dunia ya leo, nishati ya umeme jua inachukua nafasi muhimu katika kukabiliana na changamoto za mazingira, kijamii na kiuchumi na taasisi za elimu zinapokua sehemu ya matumizi haya faida zake zinaonekana wazi.

Matumizi ya nishati safi ya kupikia ni agenda mahususi ambayo imechukua nafasi kubwa katika Sera, Mipango na Mikakati ya Serikali mbalimbali duniani. Umuhimu wa agenda hii unasukumwa na ongezeko la uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi pamoja na athari za kiafya zinazotokana na matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia.

Umeme jua ni chanzo cha nishati kisichokua na uchafuzi wa mazingira, kwa kutumia paneli za jua, shule zinaweza kupata umeme kwa gharama nafuu kwa ajili ya shughuli zao za kila siku, ikiwa ni pamoja na kupikia chakula, hii inasaidia kuboresha lishe ya wanafunzi na kupunguza matumizi ya nishati isiyo safi kama vile kuni na mafuta.

Pia matumizi ya umeme jua katika shule yanasaidia kujenga ufahamu wa mazingira miongoni mwa wanafunzi wanapojifunza kuhusu nishati mbadala wanakuwa na ufahamu wa kuhifadhi mazingira na kupunguza athari za mabadiriko ya tabia nchi.

Kwa mujibu wa takwimu za Benki ya Dunia za Mwaka 2023, idadi ya Watanzania wanaotumia nishati safi ya kupikia imekua ikiongezeka kwa kiwango kidogo kutoka asilimia 1.5 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 6.9 mwaka 2021. Kiwango hiki ni chini ya kiwango cha wastani cha dunia cha asilimia 71 kwa Mwaka 2021, ambapo nchi ya Kenya ilikua na watumiaji asilimia 23.9 huku uganda ikiwa na asilimia 0.7 ya wananchi walikuwa wanatumia nishati safi ya kupikia mwaka 2021.

Katika kukabiliana na ongezeko la uharibifu wa mazingira na mabadiriko ya tabia nchi pamoja na athari za kiafya zinazotokana na matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia Serikali imeandaa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ambao unatoa mwelekeo wa nchi wa kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia. Mkakati huu una lengo la kuhakikisha kuwa asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Matumizi haya yanaweza pia kupunguza matatizo ya kiafya yanayotokana na moshi wa nishati za kawaida za kupikia kama vile magonjwa ya mfumo wa kupumua hasa wanawake na watoto, wanakabiliwa na magonjwa ya mfumo wa hewa kama pumu na magonjwa mengine yanayohusiana na moshi.

Takwimu zinaonyesha kuwa matumizi ya kuni na mkaa ni chanzo kikubwa cha vifo vinavyotokana na magonjwa ya kupumua hivyo umeme wa jua sio tu unatoa suluhusho la nishati lakini pia unaleta manufaa kwa afya na mazingira.

Hata hivyo, bado kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa nishati nafuu, endelevu na za uhakika kwa ajili ya matumizi mbalimbali hususani ya kupikia hasa kwa nchi zilizopo Kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania. Hali hii inasababisha wananchi wengi na baadhi ya Taasisi kuendelea kutumia nishati isiyo safi ya kupikia, jambo linaloendelea kuchochea ongezeko la athari za kimazingira, kiafya, kiuchumi na kijamii.

Kwa mujibu wa Mwongozo wa Benki ya Dunia kuhusu nishati safi ya Kupikia (World Bank Multi-Tier Framework- MTF), wa mwaka 2020, nishati safi ya kupikia hupimwa kwa ufanisi, urahisi wa kutumia, upatikanaji, usalama, unafuu na yenye kiwango kidogo cha sumu. 

 Vilevile, Mwongozo wa Shirika la Afya Duniani wa mwaka 2021 umeeleza kuwa nishati safi na teknolojia hupimwa kwa viwango vya chembechembe ndogo za vumbi zenye ukubwa usiozidi 2.5μm (PM2.5) na hewa ya kaboni monoksaidi zinazotolewa.

Katika kuhamasisha jamii matumizi ya nishati ya umeme jua katika taasisi za elimu hapa nchini chama cha nishati jadidifu Tanzania (Tarea) imekua ikiwakutanisha waatalam wa nishati ya umeme jua pamoja na wadau mbalimbali kujadili fursa na matumizi ya umeme wa jua katika taasisi mbalimbali ikiwa ni pamoja na shule kama mkakati wa kulinda mazingira, kupunguza matumizi ya kuni na mkaa, kupunguza gharama pamoja na vifo vitokanavyo na magonjwa ya kupumua.

Magnificat sekondari iliyopo Sanya Juu mkoa wa Kilimanjaro ni moja ya shule za sekondari nchini Tanzania ambayo imeanza kutumia teknolojia ya nishati ya umeme wa jua (Solar) kwa ajili ya kupika chakula cha wanafunzi 640 pamoja na wafanyakazi 50 na hivyo kuondokana na uchafuzi wa mazingira pamoja na kuondokana na gharama kubwa za kununua kuni kwa mwezi.

Zoltan Muellekarpe ni mkurugenzi wa kampuni ya Atmosfair Gmbh  na Prosper Magali ni mkurugenzi wa kampuni ya Watu na Umeme nchini Tanzania, wakizungumza katika mkutano ulioandaliwa na Tarea kwa njia ya mtandao kuhusu uvumbuzi wa teknolojia ya jikoni ya PV ya jua kwa ajili ya taasisi nchini Tanzania, wamesema teknolojia hiyo ni suluhisho la Kupikia kwa Umeme wa Jua na imeleta mapinduzi katika upikaji katika taasisi za Afrika, ambazo zinategemea kuni kwa kiasi kikubwa.

“ Tunatumia nguvu ya jua kuleta umeme katika upikaji wa taasisi na tunatoa dhamana ya upikaji kwa kutumia umeme wa gridi na uhifadhi kama akiba.

Amesema katika shule ya Magnificat Sekondari iliyopo Sanya juu yenye wanafunzi 640 na wafanyakazi 50, gharama za kununua kuni zilifikia zaidi ya TZS 1.5 milioni (USD 600) kwa mwezi. Gharama hizi zinachukua sehemu kubwa ya bajeti ya shule, ikikwamisha mipango ya maendeleo na kuboresha huduma za elimu.” Amesema Zoltan

Hata hivyo, mfumo wa Kupikia Umeme wa Jua umenatoa suluhisho endelevu kwa changamoto hizi. Shule iliyoanzisha mfumo wa umeme wa jua wenye uwezo wa 60kWp na betri za Lithium Phosphate za 30kWh imeweza kuhamasisha matumizi ya wapishi wa umeme wa nishati ya kuhifadhi. Hii inamaanisha kwamba shule itakuwa na uwezo wa kupika chakula kma vile ugali, maharage, uji, wali kwa gharama nafuu na kwa ufanisi, huku ikipunguza madhara kwa mazingira.

Awali katibu wa chama cha nishati jadidifu Tanzania(Tarea) Matthew Matimbwi akizungumza katika mkutano huo amesema chama cha hicho kimekua kikiandaa mikutano mbalimbali kwa kushirikiana na wadau ili kutoa elimu kwa jamii na taasisi mbalimbali juu ya matumizi ya nishati jua ili kuwajengea uwezo kufahamu faida za nishati hiyo katika kupunguza gharama pamoja na uharibifu wa mazingira hapa nchini.

Oliva ni mmoja wa wadau waliohudhuria katika mkutano huo kwa upande wake ameuliza kama teknolojia hiyo ya solar kwa ajili ya kupikia inaweza pia kutumika katika kilimo cha umwagiliaji ili kusaidia wanafunzi kuendesha mradi wa kilimo ili kupata kipato.

Akizungumzia hoja hiyo Zoltan Muellekarpe amesema ubunifu huo wa matumizi ya solar kwa ajili ya kupikia katika taasisi za elimu unaweza kutumika pia katika shughuli nyingine ikiwa ni pamoja na kilimo cha umwagiliaji katika eneo husika la shule.

Kupikia nishati ya umeme jua kua faida chanya ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja kwa malengo yote 17 ya maendeleo endelevu(SDGs).

Kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi kama vile umeme wa jua, Tanzania ina njia nzuri ya kupunguza uharibifu wa mazingira, gharama za nishati, na matatizo ya kiafya yanayohusiana na matumizi ya mkaa. Mfumo wa kupikia umeme wa jua ni suluhisho linaloweza kuleta mabadiliko chanya katika shule na taasisi nchini.

Nishati na teknolojia zinazotumika kupikia nchini ni pamoja na kinyesi cha wanyama na mabaki ya mimea, kuni,mkaa, mafuta ya taa, mkaa mbadala, bayoethano, LPG, gesi asilia, bayogesi, umeme, majiko banifu na majiko ya nishati ya jua. Kwa mujibu wa Cooking Energy Action Plan ya Mwaka 2022, asilimia 82 ya nishati kuu inayotumika nchini inatokana na tungamotaka (biomass).

Kwa matumizi ya kupikia, inakadiriwa kuwa takribani asilimia 90 ya kaya nchini hutumia nishati ya kuni na mkaa kama nishati kuu ya kupikia ambapo matumizi ya kuni ni asilimia 63.5 na mkaa ni asilimia 26.2. Asilimia 10 zilizobaki zinajumuisha asilimia 5.1 za LPG, asilimia 3 za umeme na asilimia 2.2 za nishati nyingine

Picha Kwa Hisani ya Atmosfair, Watu na Umeme Limited pamoja na AI.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...