Na Shomari Binda-Musoma
WANANCHI wa eneo la Kariakoo Kata ya Bweri manispaa ya Musoma wamepewa elimu ya uhifadhi na utunzaji wa barabara.
Elimu hiyo imetolewa na Wakala wa Barabara Tanroads mkoa wa Mara jana julai 12 kwenye eneo hilo huku ikipangwa kutolewa maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mara.
Moja ya elimu iliyotolewa ni kuacha kufanya biashara eneo la barabara kwani usababisha ajali kwa madereva kwa kupunguza upeo wa kuona.
Meneja wa Tanroads mkoa wa Mara Mhandisi Vedastus Maribe amesema barabara ni kiungo muhimu cha mawasiliano kwa jamii katika sekta ya usafirishaji na ipo kwa mujibu wa Sheria ya Barabara ya mwaka 1932 na Sheria ya mwaka 1962 na Sheria mpya ya barabara ya mwaka 2007.
Amesema baada ya kujenga barabara kulingana na mahitajj ya wakati huo eneo la hatua kadhaa uachwa kila upande wa barabara kwaajili ya upanuzi wa baadae wa barabara au kupisha barabara ya mchepuko pale panapokuwa na matengenezo kwenye barabara.
Mhandisi Maribe amesema kwa kuzingatia Sheria ya barabara Na.13 ya mwaka 2007 na kanuni zake za mwaka 2010 zinaonyesha upana wa hifadhi ya barabara ni mita 30 au futi 99 kutoka katikati ya barabara kwa pande zote mbili kushoto na kulia.
" Maafisa wa Tanroads mkoa wa Mara wanapita kwa wananchi kutoa elimu juu ya uhifafhi na kulinda barabara kwa mujibu wa Sheria.
Nawaomba wananchi wazingatie elimu inayotolewa ili kujiepusha na matatizo yanayoweza kutokea hasa wale wanaofanya biashara eneo la barabara"Amesema Maribe
Meneja huyo wa Tanroads mkoa wa Mara amesema kwa wananchi wanaotaka kununua ardhi na kujenga ni muhimu kuzingatia kufika kwenye mamlaka husika kama vile halmashauri.manispaa na Tanroads ili kuonyesha eneo la hifadhi ya barabara.
Amesisitiza kuwa fidia hutolewa kwa wale ambao barabara inapita sehemu ambayo awali haikutengwa kama sehemu ya hifadhi ya barabara.
Kwa upande wao wananchi waliopata elimu hiyo kutoka Tanroads wamesema yapo mambo waliyokuwa hawayaelewi kabla hawajapata elimu.


Comments
Post a Comment