Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tanzania Yafungua Ukurasa Mpya wa Kiuchumi



📍SEKTA YA FEDHA YAKUA, YAONDOLEWA KWENYE ORODHA YA MATAIFA HATARISHI

Na Mashaka  Mhando, Tanga

SEEIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza mafanikio makubwa katika sekta ya fedha, huku rasilimali za kibenki zikipaa hadi kufikia shilingi trilioni 71.8 na nchi kuondolewa rasmi katika orodha ya mataifa yenye vihatarishi vya kifedha (Grey List) duniani.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Deogratius kwa niaba ya Waziri wa Fedha Balozi Khamis Mussa Omar, wakati akifungua Maadhimisho ya Tano ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yaliyofanyika katika Viwanja vya Usagara, jijini Tanga, Januari 21, 2026.

Akizungumza mbele ya mamia ya wananchi na wadau wa fedha, Naibu Waziri amesema kuondolewa kwa Tanzania kwenye orodha ya nchi hatarishi (High-Risk List) na Umoja wa Ulaya (EU) ni ushindi mkubwa utakaofungua milango ya uwekezaji na kurahisisha miamala ya kimataifa kuanzia Januari 29, 2026.


Takwimu zinaonesha kuwa sekta ya kibenki imeendelea kuimarika kwa kasi, ambapo amana za wateja zimeongezeka kutoka shilingi trilioni 42.7 mwaka 2024 hadi kufikia shilingi trilioni 50.2 mwezi Septemba 2025.

Aidha, mikopo kwa sekta binafsi imeshuhudia ukuaji wa asilimia 24, ikifikia shilingi trilioni 42 ikilinganishwa na shilingi trilioni 35 za mwaka uliopita, huku kiwango cha mikopo chechefu kikidhibitiwa vyema na kubaki asilimia 2.78, kiwango ambacho ni chini ya ukomo wa kisheria wa asilimia 5.

Katika kusaidia wajasiriamali wadogo, Naibu Waziri ameeleza kuwa Serikali imefanikiwa kutoa jumla ya shilingi bilioni 41.49 kwa wanufaika 10,288 ndani ya siku 100 pekee (Novemba na Desemba 2025) kupitia mifuko 76 ya uwezeshaji nchini. 

Upande wa sekta ya bima nao umeonesha kishindo kikubwa, ambapo Naibu Kamishna wa Bima, Khadija Said, amebainisha kuwa uandikishaji wa ada za bima umekua kwa asilimia 20 na kufikia thamani ya shilingi trilioni 1.52

Khadija amesisitiza kuwa soko la bima limeendelea kutanuka likiwa na jumla ya wanufaika milioni 25.9, huku madai ya bima yaliyolipwa kwa wananchi waliofikwa na majanga yakifikia shilingi bilioni 545.4.

Kuhusu utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote, Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA) imetangaza kusajili skimu saba za bima ya afya na vituo 8,500 vya kutolea huduma nchi nzima ili kuhakikisha kila Mtanzania anapata matibabu bila kikwazo cha fedha.

Sekta ya masoko ya mitaji na dhamana (CMSA) pia imeweka rekodi mpya, ambapo thamani ya uwezekaji imefikia shilingi trilioni 63.07, huku kukiwa na bidhaa mpya za kijani (Green Bonds) na hatifungani za kijamii zinazovutia wawekezaji wengi.

Kwa upande wa Hifadhi ya Jamii, ripoti inaonesha mifuko mitatu mikuu ina jumla ya wanachama milioni 3.05 ikiwa na thamani ya mali ya shilingi trilioni 25.56, jambo linalohakikishia usalama wa maisha ya baadaye kwa wafanyakazi.

Maendeleo ya kidijitali yamechangia kwa kiasi kikubwa huduma jumuishi za fedha kufikia asilimia 76 mwaka 2023, ikiwa ni ongezeko kutoka asilimia 65 ya mwaka 2017, shukrani kwa kukua kwa matumizi ya simu za mkononi na mawakala wa benki waliofikia 145,430.

Hata hivyo, Naibu Waziri huyo ametoa onyo kali dhidi ya wakopeshaji wasio rasmi maarufu kama "Mikopo Kausha Damu", na kuiagiza Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuongeza udhibiti ili kuwalinda wananchi wasipoteze mali zao.


Waziri amewahimiza wananchi wa Tanga na Tanzania kwa ujumla kutumia wiki hii ya maadhimisho kujifunza kusoma mikataba ya fedha na kujiunga na taasisi zilizosajiliwa kisheria ili kuepuka hasara zisizo za lazima.

Maadhimisho haya ya Tano yanayofanyika Tanga ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha (2021/22-2029/30) unaolenga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara na fedha barani Afrika.

Awali Kaimu Mkuu wa mkoa wa Tanga na Mkuu wa wilaya ya Tanga, Dadi Kolimba alisema kwa upande wake akitoa salamu za mkoa huo alisema kuwa pato la mkoa  kiuchumi limekuwa hadi kufikia sh Tril 9.3 mwaka 2024 kutoka sh Tril 6.8 mwaka 2020.

Huku pato la mtu mmoja mmoja likikuwa kutoka wastani wa sh Mil 2.7 mwala 2020 hadi kufikia Mil 3.4 mwaka 2024.






Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...