Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amekagua hali ya athari iliyosababishwa na mvua katika eneo la kidete, Kilosa mkoani Morogoro.
Akiwa eneo hilo Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amewahakikishia wakazi wa eneo hilo kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ilishachukua hatua za kukabiliana na mvua kwa kuamua kujenga mabwawa katika eneo hilo.







