Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Vyuo Bora vya Malaysia Kuonesha Fursa za Masomo Serena Hotel, Dar es salaam


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Tanzania inatarajiwa kupokea ujumbe mkubwa wa viongozi wa elimu ya juu kutoka Malaysia, wakiwemo viongozi kutoka Wizara ya Elimu ya Malaysia, Education Malaysia Global Services (EMGS), pamoja na wawakilishi wa vyuo vikuu tisa vitakavyoshiriki Maonesho ya Elimu ya Malaysia yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 1 hadi 3, 2026 katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam.

Ujumbe huo wa watu 19 kutoka Malaysia unatarajiwa kuwasili nchini tarehe  ikiwa ni maandalizi ya kushiriki maonesho hayo pamoja na kufanya vikao vya kimkakati na wadau mbalimbali wa elimu nchini, ikiwemo Wizara ya Elimu, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), vyuo vikuu vya Tanzania, shule, wazazi, walezi na wanafunzi.

Maonesho hayo, yanayoratibiwa kwa ushirikiano wa Global Education Link (GEL) na wadau wa elimu kutoka Malaysia, yanalenga kufungua fursa za udahili, ufadhili wa masomo, ushirikiano wa kitaaluma, pamoja na kuimarisha mahusiano ya elimu ya juu kati ya Tanzania na Malaysia.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdumalik Mollel, alisema ujio huo ni wa kimkakati kwa Tanzania kwa kuwa unahusisha mamlaka muhimu za elimu ya juu kutoka Malaysia, vyuo vikuu, pamoja na taasisi zinazoratibu masuala ya wanafunzi wa kimataifa, ikiwemo taratibu za udahili na visa.




Bwana Mollel alisema ujumbe huo utajumuisha viongozi kutoka Wizara ya Elimu ya Malaysia, viongozi wa EMGS na wawakilishi wa vyuo vikuu tisa ambavyo vitatoa taarifa za moja kwa moja kuhusu programu za masomo, gharama, mazingira ya kujifunzia, taratibu za udahili na nafasi za scholarship kwa wanafunzi wa Tanzania.

“Hii siyo exhibition ya kawaida ya udahili pekee. Ni fursa ya kitaifa ya kuunganisha Tanzania na Malaysia katika elimu ya juu, scholarship, programu za pamoja, tafiti, ubunifu na makubaliano ya ushirikiano kati ya vyuo vya pande zote mbili,” alisema Bwana Mollel.

Alisema miongoni mwa taasisi zinazotarajiwa kushiriki ni Asia Pacific University of Technology and Innovation (APU), University of Malaya, University Putra Malaysia (UPM), University Kebangsaan Malaysia (UKM), UCSI University, University Kuala Lumpur, University Selangor (UNISEL) na Putra Business School, huku taasisi nyingine zikitarajiwa kuthibitishwa kupitia mwongozo rasmi wa maonesho.

Kwa mujibu wa Bwana Mollel, ujio wa vyuo hivyo ni fursa kubwa kwa wanafunzi wa Tanzania wanaotafuta elimu ya kimataifa katika maeneo ya sayansi, teknolojia, biashara, afya, uhandisi, TEHAMA, ubunifu, ujasiriamali na taaluma nyingine zenye mahitaji makubwa katika soko la ajira la sasa na la baadaye.

Alisema tofauti na maonesho mengine ya elimu, ujumbe huu umebeba agenda pana inayohusisha ushirikiano wa kitaasisi kati ya vyuo vya Malaysia na vyuo vya Tanzania. Alibainisha kuwa vyuo vya Malaysia vimeonyesha utayari wa kusaini Hati za Makubaliano ya Ushirikiano, yaani MoU, na vyuo vya Tanzania vitakavyokuwa tayari kushirikiana katika maeneo ya tafiti, ubadilishanaji wa wanafunzi na wahadhiri, programu za pamoja, mafunzo ya muda mfupi, teknolojia na ubunifu.

“Vyuo vya Malaysia vipo tayari kukutana na vyuo vya Tanzania. Vipo tayari kusikiliza mahitaji ya vyuo vyetu na kuona namna ya kujenga ushirikiano wenye manufaa kwa pande zote mbili. Hii ni nafasi nzuri kwa vyuo vyetu kujiunganisha na mfumo wa elimu wa kimataifa,” alisema Bwana Mollel.

Aliongeza kuwa ujumbe huo pia upo tayari kufanya kikao cha pamoja na vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu nchini Tanzania, ambapo vyuo vya Malaysia vitapata nafasi ya kufanya mawasilisho mafupi kuhusu programu zao, malengo yao nchini Tanzania na maeneo wanayotaka kushirikiana na Tanzania.

Kwa upande wa Tanzania, baadhi ya vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu zitapata nafasi ya kueleza maeneo yao ya kipaumbele katika ushirikiano, ikiwemo programu za “2+2”, tafiti za pamoja, mafunzo ya kitaaluma, ubunifu, ujasiriamali na kuimarisha mahusiano ya kitaaluma kati ya Tanzania na Malaysia.

Mollel alisema maonesho hayo yana umuhimu mkubwa pia kwa Wizara ya Elimu nchini Tanzania, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Kamati ya Samia Suluhu Hassan Scholarship Scheme, shule, wazazi, walezi na vijana kwa ujumla, kwa kuwa yatafungua majadiliano ya moja kwa moja kuhusu nafasi za ufadhili wa masomo na ushirikiano wa elimu ya juu.

Alisema kwa Wizara ya Elimu, ujio huo ni fursa ya kujenga daraja la mahusiano ya kitaaluma kati ya Tanzania na Malaysia, hasa katika eneo la elimu ya juu, ubora wa programu, utaratibu wa wanafunzi wa kimataifa na mifumo ya kuvutia wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali.

Kwa TCU, Bwana Mollel alisema maonesho hayo yanaweza kufungua nafasi ya kubadilishana uzoefu na mamlaka za elimu ya juu kutoka Malaysia kuhusu usimamizi wa ubora, ithibati, uendelezaji wa programu za pamoja na uratibu wa wanafunzi wanaokwenda kusoma nje ya nchi.

Aidha, alisema Kamati ya Samia Suluhu Hassan Scholarship Scheme nayo inaweza kutumia ujio huo kujadiliana na vyuo vya Malaysia kuhusu uwezekano wa kuongeza nafasi za scholarship kwa Watanzania, hususan katika taaluma zenye umuhimu kwa maendeleo ya taifa.

“Tunataka Study in Malaysia Exhibition iwe mwanzo wa safari mpya ya ushirikiano wa elimu kati ya Tanzania na Malaysia. Hii ni fursa ya udahili, lakini pia ni fursa ya diplomasia ya elimu, maendeleo ya vijana na ujenzi wa rasilimali watu kwa taifa,” alisema Bwana Mollel.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...