Skip to main content

Mabausa Wanaodaiwa Kumuua Mteja kwa Kipigo Wapandishwa Kizimbani


Na: Dawati la Habari Polisi; Mwanza

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limewafikisha Mahakamani mlinzi (baunsa) pamoja na mfanyakazi wa usafi waliokuwa wakifanya kazi katika baa ya Las Vegas, wakituhumiwa kwa mauaji ya Mkazi wa Mwanza, Mzafuru Faisal Yunusu.

​Washtakiwa hao ni Yohana Paul Peter (22), ambaye ni mlinzi wa eneo lilipotokea tukio hilo na Hamis Juma Mussa (27), mfanyakazi wa usafi. 

Wawili hao wamepandishwa kizimbani leo Alhamisi Mei 14, 2026, katika Mahakama ya Wilaya ya Ilemela na kusomewa shtaka la mauaji.




​Akisoma shauri hilo la jinai namba 10492 la mwaka 2026 mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilemela, Mhe. Christian Mwalimu, Wakili wa Serikali Clara Muhando, akisaidiana na Evance Kaiza, aliieleza mahakama kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo mnamo tarehe 05.02.2026 katika baa ya Las Vegas iliyopo eneo la Kona ya Bwiru, mtaa wa Nyamanoro, wilaya ya Ilemela.

​Washtakiwa wote wawili, wakiwa katika baa hiyo ya Las Vegas, wanadaiwa kumshambulia na kumuua Mzafuru Faisal Yunusu kinyume na kifungu cha 196 na 197 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2023.

​Hata hivyo, watuhumiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kisheria ya kusikiliza mashauri ya mauaji.

​"Mahakama haina mamlaka ya kusikiliza shauri hili, kwa hiyo hamtatakiwa kujibu chochote juu ya tuhuma zenu. Vilevile, kesi inayowakabili haina dhamana, hivyo mtaendelea kuwa mahabusu hadi pale upelelezi utakapokamilika," alisema Hakimu Mwalimu.

​Kesi hiyo imeahirishwa hadi Mei 28, 2026, na washtakiwa wamerejeshwa rumande.

Comments

George marato tv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.