MARA
TAASISI ya Nyansaho foundation imetoa mifuko elfu sita ya saruji kwa wabunge wa Mkoa Mara ambapo Kila Mbunge amepata mgao wa mifuko mia tano ambago inalengo kuboresha sekta za Afya na Elimu.
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi Mifuko hiyo ya saruji kwa Wabunge kumi na mbili wa mkoa wa Mara leo Machi 22,2026,mwenyekiti wa tassisi hiyo ya Nyansaho Foundation Dkt Rhimo Nyansaho,amesema kila Mbunge atafanye kazi iliyokusudiwa na aje na matokeo chanya ili baadae apate bati za kuezeka alichokifanya Jimboni kwake.
Amesema kuwa mifuko hiyo mia tano ya simenti kwa kila mbunge itengenezwe mfumo kwamba inaenda kutekeleza nini.
"baada ya miezi miwili, kuanzia sasa tupate taarifa kwamba ile mifuko elfu sita imefanya maboma kama ni maboma au kama ni kufanya chochote". Ameongeza
"Baada ya miezi miwili tukimaliza bunge la bajeti wakati tunakuja nitakuwa pia nimeshajipanga kupitia kwa wadau tutawaletea tena bati". Amesisitiza
"kila mbunge aseme hii mifuko kwenye jimbo X itakwenda kufanya moja, mbili, tatu Tukifanya vile kamati ya ulinzi na usalama sasa kupitia kwa wakuu wa wilaya na inatolewa taarifa mifuko hii iliyoenda hapa imefanya swala hili,ni vizuri tukaeelekeza ikaenda kwenye elimu na afya". Amesema Nyansaho ambaye pia ni waziri wa ulinzi na jeshi LA kujenga Taifa.
Hata hivyo mh Nyansaho amewataka viongozi wa mkoa wa Mara kufikiria namna bora ya kumuenzi baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
"Tunajua ile tarehe ya kifo chake Taifa limekuwa likifanya jambo, lakini hatuzuii sisi wa mkoa wa Mara kufanya jambo LA kumuenzi kiongozi huyu ambaye alizaliwa katika mkoa huu, kuna tassisi hata hapa Mara zipo zinatumia jina lake, tuone sasa tunafanya nini kumuenzi"alisema Dkt Nyansaho.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara Patrick Chandi, ametumia jukwaa hilo Kwa kuipongeza taasisi ya Nyansaho foundation ambapo amesema taasisi hiyo imetambua kuwa mfuko wa Jimbo pekee hautoshi hivyo ni vema kuongeza nguvu ili kufanikisha maendeleo kwa haraka katika mkoa wa Mara.
Kwa upande wake mjumbe wa halmashauri kuu mkoa wa Mara Christopher Gachuma,amesema taasisi hiyo imelenga kusaidia majimbo ya mkoa wa Mara hivyo ameyasisitiza majimbo hayo Kutumia saruji hizo Kwa malengo yaliyokusudiwa.
Nao wabunge wa Mkoa wa Mara walio hudhuria hafla hiyo akiwemo Mbunge wa Bunda Ester Bulaya ameishukuru taasisi ya Nyansaho foundation ambapo amesema yeye alishakaa na diwani wake Kwa Kushirikiana na Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na watendaji wa kata kuwa mifuko hiyo itaenda Kwenye Ujenzi wa shule na vituo vya Afya.
"Sisi tulishaimaliza. Hata ukitaka taarifa leo Bunda mjini, utaipata.Na mheshimiwa mkuu wa mkoa, nikuhakikishie, ukija kukagua utaona mambo yanaenda vizuri". Amesema
"Naomba nikusifie, kutoa ni moyo. Lakini wewe umekuwa ukijitoa sana kwa ajili ya mkoa wako. Sisi wabunge wako tutakupa ushirikiano, tutakuombea kwa mwenyezi mungu".. Ameongeza
Naye Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini mh Mgore Miraji, amesema kutokana na changamoto ya madarasa katika baadhi ya shule Kwenye jimblo la Musoma Mjini ,kupitia Mifuko hiyo waliyopewa wataenda Kuboresha madarasa pamoja na vituo vya Afya.
Mbunge wa Jimbo la Butiama mh Dkt Charles Mahera,amesema wao wameshafanya tathmini mwezi wa kumi na mbili ambapo tayari mifuko hiyo itakwenda kuingia katika shule za msingi na sekondari 25 na mifuko 40 itakayo baki itaenda kwenye makanisa na misikiti.
kadhalika, Mbunge wa jimbo la Serengeti mh Mary Daniel ameishukuru Nyansaho foundation Kwa kazi kubwa na nzuri inayoifanya ambapo amesema mifuko hiyo waliyopewa katika Jimbo la serengeti itakwenda kufanya kazi iliyokusudiwa.
Mbunge wa Jimbo la Mwibara Mh Kangi lugola, ameishukuru taasisi ya Nyansaho foundation ambapo amesema mifuko waliyoipata itakwenda katika sekta ya Elimu na Afya na kwamba itatoa ajira kwa vijana ambao wataanza kufanya kazi ya ukarabati ili wapate maokoto kupitia Nyansaho foundation.
Aidha, wabunge wa viti Maalumu mkoa wa Mara Mh Ghati Chomete na Mh Agness Methew Marwa,wameipongeza taasisi ya Nyansaho foundation ambapo wamesema Kwa mifuko hiyo ya saruji waliyokabidhiwa watahakikisha inaenda kuleta tija katika maeneo Mbalimbali ili wananchi wanufaike na msaada huo.
aasisi ya Nyansaho foundation imetoa jumla ya mifuko yelfu sita ya saruji ambapo Kwa kila mbunge wa Jimbo na viti maalum amepata mifuko mia tano ya saruji kwa dhamira ya kwenda Kuboresha Sekta za Afya na Elimu Mwisho

















