Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu aagiza mkandarasi aliyekula fedha za maji, akamatwe


NA MASHAKA MHANDO, Korogwe

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amemwagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga (RPC), ACP Almachius Mchunguzi, kumsaka na kumkamata mkandarasi aliyekimbia baada ya kulipwa Shilingi Milioni 934 kwa ajili ya ukarabati wa mradi wa maji katika mji wa Mombo, wilayani Korogwe.

Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo Leo February 14 mara baada ya kukagua mradi wa maji wa Miji 28 unaotekelezwa katika wilaya nne za mkoa wa Tanga, ambapo ameeleza kukerwa na mkandarasi huyo aliyepokea fedha za umma na kutoweka bila kutekeleza mradi, huku wananchi wakiendelea kutaabika na ukosefu wa maji.

"Ameondoka na fedha wakati wananchi wanapata shida; haya ndiyo mambo yanayokera na kuchukiza. RPC, huyu mtu atafutwe popote alipo, akamatwe na awekwe ndani mpaka arejeshe fedha za umma. Sijateuliwa ili nipendwe, na sitakuwa na huruma na watu wanaohujumu miradi ya Serikali," alisisitiza Waziri Mkuu.


Mradi wa Miji 28 Kufikia Asilimia 75

Mapema, Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, alimweleza Waziri Mkuu kuwa mradi wa maji wa Miji 28 unaogharimu Shilingi Bilioni 171 umefikia asilimia 74 ya utekelezaji wake. Mradi huo unatarajiwa kuwa ukombozi kwa wakazi wa wilaya za Korogwe, Handeni, Muheza, na Pangani.

Waziri Aweso alibainisha kuwa mradi huo utazalisha lita milioni 52 za maji kwa siku, zitakazohudumia wananchi wapatao 860,000 katika vijiji 161. Alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizo na kueleza kuwa mradi unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Machi, 2026.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ametoa maelekezo ya haraka kwa wataalamu wa maji kuhakikisha wananchi wa Kijiji cha Tabora, Kata ya Mswaha (Korogwe Vijijini), ambao mradi unapita katika maeneo yao, wanapatiwa huduma ya maji mara moja ili nao wanufaike na matunda ya uwekezaji huo mkubwa.

Dkt. Mwigulu alihitimisha kwa kusema kuwa Serikali itaendelea kuwa na msimamo mkali dhidi ya mkandarasi yeyote atakayefanya kazi chini ya kiwango au kuiba fedha za miradi, akisisitiza kuwa thamani ya fedha lazima ionekane kwa wananchi.

Mapema asubuhi Waziri Mkuu akiwa wilayani Kilindi  ametoa onyo kali kwa wasimamizi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilindi, akisema atachukua hatua kali za kinidhamu na kisheria endapo itabainika kuwepo kwa ubadhirifu wa Shilingi Bilioni 2.6 zilizotolewa kwa ajili ya mradi huo.

Dkt. Mwigulu ametoa kauli hiyo mara baada ya kuweka jiwe la msingi la hospitali hiyo, ambapo licha ya kuridhishwa na ubora wa majengo yaliyokamilika, ameshitushwa na taarifa za kutoonekana kwa jengo la wodi ya mama na mtoto wakati fedha zake zilikwishatolewa na Serikali.



"Nimekuja kuweka jiwe la msingi baada ya kuridhishwa na viwango vya ujenzi wa majengo haya, lakini DED nimeambiwa fedha iliyokuja ilitakiwa ijenge majengo mengi zaidi ya haya. Nyinyi mmejenga majengo pungufu, fedha nyingine mmeipeleka wapi?" alihoji Waziri Mkuu.


Sakata la Saruji ya Mbeya na "Kichaka" cha Gharama

Waziri Mkuu amefichua mchezo unaofanywa na baadhi ya watumishi wa kuhalalisha matumizi mabaya ya fedha kwa kununua vifaa vya ujenzi mbali na maeneo ya mradi ili kuongeza gharama za usafirishaji. Ameshitushwa na taarifa kuwa saruji ya ujenzi wa hospitali hiyo imenunuliwa mkoani Mbeya badala ya kutumia viwanda vya saruji vilivyopo jirani mkoani Tanga.

"Kuna mchezo unataka kuhalalishwa hapa wa kununua vifaa mbali; najua saruji mmenunua Mbeya. Takukuru fuatilieni kila kitu kwenye hiki kichaka cha gharama ili niweze kuchukua hatua kali. Hatuwezi kuwavumilia watu wanaoisababishia Serikali hasara kiasi hiki," alisisitiza.


Mapema, John Mgalula Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi (DED), alikiri mbele ya Waziri Mkuu kuwa fedha zilipokelewa kwa ajili ya majengo tisa, lakini majengo ya kufulia na kutolea dawa hayajakamilika kutokana na kile alichodai kuwa ni kuongezeka kwa gharama za kusafirisha vifaa.

Mgogoro wa mpaka kati ya Simanjiro na Kilindi

Katika hatua nyingine, Dkt. Mwigulu amechukua hatua za haraka kutatua mgogoro wa mpaka kati ya wilaya za Simanjiro (Manyara) na Kilindi (Tanga), ambao umedumu kwa muda mrefu na kusababisha mivutano kati ya wakulima na wafugaji.

Waziri Mkuu ametangaza kuunda Kamati ya Mawaziri wa Kisekta itakayojumuisha Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Maliasili na Utalii, pamoja na TAMISEMI ili kumaliza kabisa mgogoro huo na kurejesha amani katika maeneo ya mipakani.

Kikao hicho kitakutana mkoani Tanga February 16 kabla Waziri Mkuu hajaondoka mkoani hapa kuelekea mkoani kilimanjaro. 

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...