WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na mlemavu wa miguu, Nassor Shaban Sabuni ambaye alijitokeza katika mkutano wa hadhara wa Waziri Mkuu uliofanyika katika Uwanja wa Lemore Tanga mjini leo Februari 15, 2026.
Ndugu Shabani alimuomba Waziri Mkuu msaada wa Pikipiki ya Matairi Matatu (Bajaji) ambapo Dkt. Mwigulu aliridhia ombi hilo na kuagiza Ofisi yake kumnunulia aina ya bajaji anayoitaka.
