Daraja la Mto Pangani ni Kichocheo cha Uchumi-Dkt. Mwigulu

GEORGE MARATO TV
0


_Asema ameridhishwa na kiwango cha uwekezaji kilichofanywa na Rais Dkt. Samia kwenye daraja hilo_

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuwa mradi wa ujenzi wa daraja la Pangani na barabara unganishi utasaidia kukuza shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa maeneo hayo.

Ameongeza kuwa ameridhishwa na kiwango cha uwekezaji kilichofanywa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika daraja hilo ambalo “Si kila kiongozi anakuwa na maono na ujasiri wa kuweza kuchukua hatua za kujenga miundombinu ya aina hii”

 Amesema hayo leo Jumapili (Februari 15, 2026) wakati alipokagua Miradi wa Ujenzi wa Daraja la Pangani lenye urefu wa mita 525 na barabara unganishi zenye urefu wa kilomita 25.6. Gharama ya mradi ni Shilingi bilioni 124.9.




Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa ujenzi wa barabara na daraja hilo utaweka alama ya kudumu katika wilaya hiyo “Tuendelee kumkumbuka na kumuombea Mheshimiwa Rais Dkt. Samia, hii ni kazi ya kiongozi mwenye maono.”

Kadhalika Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amewataka viongozi wa wilaya hiyo kuweka  mpango wa kuwa na kituo cha mabasi cha kisasa ili iendane  na viwango vya daraja na barabara hiyo ya kimataifa.

Naye, Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi, Godfrey Kasekenya amesema kuwa wamejipanga kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati na ubora ili wananchi wa maeneo hayo waweze kunufaika. 

Aidha,  Mhandisi Kasekenya amesema kuwa Serikali  imejipanga  kutekeleza mradi wa ujenzi wa Barabara ya Bagamoyo (Makurunge) – Mkange – Pangani – Tanga yenye urefu wa kilometa 256, “Tunampango wa kuwa na Tanga bypass yenye urefu wa Kilomita 63” kwasasa mhandisi mshauri amepatikana na ataanza kazi mwezi huu na ataanzia Muheza-Kisimatui-Pongwe-Pambe hadi Kiomoni."

Hadi sasa, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 64 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Februari 5, 2027.

Kwa upande wake Waziri wa Maji, Jumaa aweso amesema sasa ni wakati wa Wilaya ya Pangani kuwa na Fast boat ili watu wanaotoka Tanga mjini, Mombasa, Arusha, Kilimanjaro na Manyara badala ya kutembelea umbali kwenda kupanda meli Dar es Salaam sasa wakaipandie Pangani

“Sisi hapa tunazungumzia uchumi, heshima ya binadamu ni uchumi, mmetujengea barabara sasa tunanachopigania ni uchumi na maisha ya maendeleo ya watu wetu”



Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top