Waziri wa Ulinzi na Jkt Azungumza na Wazee wa Mkoa wa Mara

GEORGE MARATO TV
0

 


Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho akizungumza na wazee wa Mkoa wa Mara katika eneo la Komaswa, Wilaya ya Tarime leo tarehe 24 Disemba, 2025. 


Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Chama cha Mapinduzi Mhe. Fadhili Maganya, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi, Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) Mhe. Christopher Gachuma, Mtoto wa Baba wa Taifa, Madaraka Nyerere.







Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na wazee zaidi ya 160, wazee wameazimia kulinda na kudumisha amani na utulivu katika Mkoa wa Mara na kufanya kikao kama hicho kila mwaka.








Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top