-ATAKA WAACHIWE WANA CCM CHAGUO LAO
Na Shomari Binda-Musoma
MBUNGE wa Jimbo la Tarime Vijijini Mwita Waitara amezishukia Kamati za Siasa za Chama cha Mapinduzi ( CCM) za Wilaya ya Musoma mjini na Tarime Vijijini kuacha kuwachagulia mbunge wana CCM wanaomtaka wao.
Kauli hiyo ameitoa jana juni 14,2025 kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na mbunge wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo kwaajili ya kuwashukuru wananchi kwa kumpa ushirikiano kwa miaka 5 ya uwakilishi wake.
Mbele ya wanachama na wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye eneo la soka la kwa saa nane Kata ya Mshikamano amesema yapo mambo ambayo yanafanywa na Kamati hizo za Siasa ambàyo hayapaswi kunyamaziwa.
Amesema mbunge wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo amefanya kazi nzuri katika utekelezaji wa ilani na anapofanya ziara ya kusoma kamati inakaa pembeni.
Waitara amesema hayo mambo sio ya kunyamaziwa kuona watu wanatembea na mgombea wao mfukoni na yale mazuri yaliyofanywa na mbunge wanayabeza
Amesema anatamani sana maendeleo yaliyofanyika ndani ya jimbo la.Musoma mjini lakini wapo wanaobeza ambaye yeye hakubaliani nao.
Mbunge huyo ambaye amekuwa hapendezwi na kutothaminiwa kazi zinazofanywa na viongozi wakiwemo wabunge katika kuwatumikia wananchi.
" Mathayo amefanya kazi nzuri na wanachama wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) na wananchi wanampenda lakini wachache wanakuwa wanataka kuturudisha nyuma.
" Viongozi baadhi ndani ya chama chetu hatuwezi kukubaliana nao wanakwenda ndivyo sivyo na tutaendelea kusimamia kwenye ukweli",amesema.
Amesema leo jimbo la Musoma mjini watu wanapata umeme kwa elfu ishirini na saba kama vijijini na hiyo ni kazi iliyofanywa na mbunge Mathayo.
Waitara amesema mambo yanayofanyika Musoma mjini ndiyo yanayofanyika katika jimbo la Tarime Vijijini kwa viongozi wa chama kutowathamini wabunge na yeye anasimama kama jeshi la mtu mmoja na atakayesimama mbele yake atapita nae.
"Kamati za Siasa baadhi ya wajumbe wake wakuu ndio wenye kutoa maamzi katika mapendekezo lakini wao wanawagombea wao na kila leo wanapiga vifuo kuwa kama hukubaliani nao kwa mambo binafsi hawawezi kukupendekeza sasa hapo hakuna haki,ndio maana nasema kama nimefanya vizuri kwenye utekelezaji wa ilani na wanaccm wanakubali hilo ngoja niwe jeshi la mtu mmoja lakini sio kukipigia magoti kikundi cha wachache kwa maslahi yao binafsi"alisema Waitara huku akishangiliwa na maelfu ya wananchi waliokuwa katika viwanja hivyo.
Aidha ameiomba Kamati ya Siasa ya CCM mkoa wa Mara kuangalia kwa makini hali ya siasa za Musoma mjini na Tarime.
Akizungumza wakati akiwashukuru wananchi kwa kumpa ushirikiano kwa kipindi cha miaka 5 mbunge wa Jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo amesema amefarijika kwa namna wana CCM na wananchi kwa kuonyesha upendo mkubwa kwake na hata kufikia hatua ya kumchangia fedha kuchukua fomu.
Mathayo amesema alishapita na kusoma utekelezaji wa ilani na yaliyofanyika yanaonekana na ziara yake imekuwa ni kutoa shukurani.
Amesema kwa kuwa wananchi wamemuomba kugombea tena atafanya hivyo kwa kuchukua fomu tarehe ikifika kwa kuwa bado anazo nguvu za kuwatumikia.
Kwa upande wao wanachama wa CCM waliohudhuria mkutano huo wamesema bado wana imani na mbunge huyo na kuahidi kumchagua kwa mara nyingine mwaka huu.