Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mafanikio ya Sekta ya Madini katika Kipindi cha Miaka Minne ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan



*Dondoo za Aliyoyasema Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde katika Mkutano na Wahariri wa Vyombo vya Habari, Mei 24, 2025 Jijini Dar es Salaam.*


*Mada: Mafanikio ya Sekta ya Madini katika Kipindi cha Miaka Minne ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan*

1. Ongezeko la Bajeti – Bajeti ya Wizara ya Madini imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Kutoka shilingi bilioni 89 mwaka wa fedha 2023/2024 hadi shilingi bilioni 231 kwa mwaka 2024/2025. Kwa mwaka ujao wa fedha 2025/2026, tumeidhinishiwa bajeti ya shilingi bilioni 224. Asilimia kubwa ya bajeti hii inaelekezwa kwenye Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kwa ajili ya kufanya tafiti za kina za jiolojia na ujenzi wa maabara ya kisasa ya uchambuzi wa madini katika eneo la Kizota, Dodoma. Lengo ni kuifanya GST kuwa kitovu cha huduma za maabara ya madini kwa Afrika nzima. Pia, maabara nyingine zinajengwa katika mikoa ya Geita na Chunya (Mbeya) ili kuboresha huduma za uchambuzi wa madini nchini.

2. Ongezeko la GDP – Mchango wa Sekta ya Madini katika pato la taifa (GDP) umeongezeka kwa kiwango kikubwa. Sera ya Madini ya mwaka 2009 pamoja na Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo kwa Miaka Mitano unalenga sekta kuchangia angalau asilimia 10 ya GDP ifikapo mwaka 2025. Hadi kufikia Desemba 2024, mwaka mmoja kabla ya muda uliopangwa, sekta ya madini tayari ilikuwa imefikia mchango wa asilimia 10.1, hatua ambayo ni ya kihistoria na ya kujivunia.

3. Mining Vision 2030: Kauli mbiu ya mpango huu ni “Madini ni Maisha na Utajiri.” Mpango huu unalenga kuongeza kiwango cha tafiti za kina za madini kutoka asilimia 16 ya sasa hadi asilimia 50 ifikapo mwaka 2030. Sekta ya madini pia inatajwa kuwa kichocheo kikuu cha sekta nyingine kama maji, kilimo, afya, viwanda, ujenzi na uchumi kwa ujumla. Kwa sasa sekta imechangia mzunguko wa fedha wa takribani trilioni 1.7 na mauzo yamefikia asilimia 56.2 ya jumla ya mauzo nje ya nchi.

4. Maduhuli – Katika mwaka wa fedha 2015/2016, sekta ya madini ilikusanya maduhuli ya shilingi bilioni 162. Makusanyo haya yameongezeka kwa kasi hadi kufikia bilioni 678 mwaka 2022/2023, na bilioni 753 mwaka 2023/2024. Kwa mwaka huu wa fedha 2024/2025, tumewekewa lengo la kukusanya shilingi trilioni 1. Hadi kufikia tarehe 24 Mei 2025, tayari tumekusanya shilingi bilioni 930, ikiwa ni mafanikio makubwa huku zikiwa zimebaki siku 37 kabla mwaka wa fedha kumalizika.

5. BOT yaanza ununuzi wa Dhahabu – Kufuatia marekebisho ya Sheria ya Madini mwaka 2024, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeanza rasmi kununua dhahabu kutoka kwa wazalishaji wa ndani. Sheria sasa inawataka wamiliki wote wa leseni za uchimbaji wa dhahabu kutenga angalau asilimia 20 ya uzalishaji wao kwa ajili ya kuuza BoT. Kuanzia Oktoba 2024 hadi sasa (miezi 8), BoT imenunua tani 3.7 za dhahabu. Kwa hatua hii, Tanzania inajiweka kwenye nafasi nzuri kuwa miongoni mwa nchi zenye akiba kubwa ya dhahabu barani Afrika – mfano, hivisasa Algeria barani Afrika inaongoza kwa kuwa na akiba ya tani 174, na Msumbiji iko nafasi ya 10 kwa tani 3.6.

6. Uwezeshwaji Wachimbaji Wadogo – Wachimbaji wadogo hivi sasa wanachangia asilimia 40 ya mapato yote yatokanayo na sekta ya madini. Serikali imefuta leseni na maombi 2,648 ili kuwawezesha wachimbaji wadogo kupata maeneo halali ya uchimbaji. Shirika la STAMICO limejipambanua kuwa mlezi wao, ambapo limewanunulia mashine 15 za kuchoronga miamba (drilling rigs). Pia, Serikali imefanya mazungumzo na benki mbalimbali kuwahamasisha kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo, ambapo sasa wanakopesheka. Tumeunda timu ya wataalam sita kutoka sekta binafsi na serikali kwa ajili ya kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu namna bora ya kuwainua wachimbaji wadogo. Kupitia Mfuko wa Dhamana wa Hazina (Credit Guarantee Scheme), wachache wataanza kunufaika na matarajio ni kueneza huduma hiyo kwa wengi zaidi.

7. Viwanda vya kuongeza thamani – Kifungu cha 100 cha Sheria ya Madini kinawataka wawekezaji wanaoomba leseni kuwa na mpango wa kuongeza thamani ya madini. Eneo la Mgodi wa Buzwagi (unaofungwa baada ya kusitisha shughuli za uchimbaji) limegeuzwa kuwa eneo maalum la uwekezaji wa viwanda (Special Economic Zone). Moja ya viwanda vitakavyojengwa ni pamoja na Kiwanda cha Kusafisha Makinikia cha Tembo Nickel Refining Limited, hatua inayolenga kuongeza thamani ya madini ya nickel na ajira nchini.

8. Minada ya Vito – Serikali imerejesha rasmi minada ya ndani ya madini ya vito kwa lengo la kuongeza thamani ya madini haya, hasa Tanzanite ambayo ni adimu duniani. Tumefanya minada Mirerani mwezi Desemba 2024 na Arusha Februari 2025, juhudi hizi pia ni sehemu ya rebranding ya Tanzanite ili kutambulika zaidi kimataifa.

9. Marekebisho ya Sheria – tumefanya marekebisho ya Sheria mwaka 2024, ambapo sasa inabainisha kuwa leseni za uchimbaji mdogo wa madini ni kwa ajili ya Watanzania pekee. Hata hivyo, msaada wa kitaalamu kutoka kwa wageni unaruhusiwa kwa masharti maalum, ikiwemo mkataba rasmi unaopitiwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini ili kuhakikisha Watanzania wananufaika. Pia, Marekebisho haya yamepunguza migogoro mingi kati ya wachimbaji wadogo na wawekezaji.

10. Miradi Mikubwa – Serikali inaendelea kusimamia na kuvutia uwekezaji kwenye migodi mikubwa kama ule wa Nyanzaga uliopo wilayani Sengerema.

11. STAMICO – Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limepiga hatua kubwa kutoka kuingiza mapato ya shilingi bilioni 1 hadi bilioni 84 ndani ya kipindi cha miaka minne. Hivi sasa shirika linajilipa mishahara lenyewe, linatoa gawio Serikalini na limepanga kuanzisha miradi mikubwa ya kimkakati kuanzia mwaka wa fedha ujao ili taifa linufaike zaidi. Kuna pia mpango wa kuanzisha kampuni tanzu ya miradi.

12. Local Content & CSR – Ajira kwa Watanzania kwenye sekta ya madini zimeongezeka. Kwa sasa ajira za moja kwa moja ni zaidi ya 19,356, ambapo asilimia 97 ya ajira hizo ni kwa Watanzania. Watanzania pia wanashikilia nafasi nyingi za juu kwenye migodi. Aidha, wameanza kutoa huduma muhimu kama vile utengenezaji wa vifaa vya migodini, hatua ambayo inachochea uchumi wa ndani.

13. Madini Mkakati – Serikali iko mbioni kukamilisha mkakati maalum wa namna ya kuyavuna na kuyaendeleza madini mkakati kama vile graphite, nickel, rare earths n.k., kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo.

14. MBT – Mining for a Brighter Tomorrow – Mpango huu unalenga kusaidia makundi ya wanawake na vijana kwa kuwapatia leseni na maeneo ya uchimbaji. Tayari tumeanza Nyamongo, mkoa wa Mara, kwa kugawa zaidi ya leseni 2000, na wadau mbalimbali wameonyesha nia ya kushiriki katika kuwawezesha makundi haya.

15. Vituo vya Ukodishaji Mitambo – Serikali imeanzisha vituo vya ukodishaji wa mitambo ya kisasa kwa bei nafuu ili kuwasaidia wachimbaji wadogo kuchimba kwa tija na kwa ufanisi zaidi.

16. Gold Coins – Serikali ipo kwenye mazungumzo na Benki Kuu ya Tanzania kuhusu kuanzisha sarafu za dhahabu (Gold Coins) kwa ajili ya uwekezaji na akiba ya thamani. Lengo ni kuwawezesha Watanzania kuhifadhi dhahabu benki na kuitumia kwa malipo kama vile mafuta ya petroli na dizeli.

17. Vikao vya majadiliano na wawekezaji – Serikali inaendelea kufanya vikao vya wazi na wawekezaji wa Sekta ya Madini – wa Kati na Wakubwa – ili kusikiliza changamoto zao na kuzitatua kwa wakati, kwa lengo la kuimarisha mazingira ya uwekezaji nchini.

18. Masoko na vituo vya ununuzi – Serikali imeimarisha upatikanaji wa masoko ya uhakika kwa wachimbaji wadogo kupitia vituo vya ununuzi wa madini. Hatua hii inalenga kuwapa wachimbaji bei nzuri, kuwasaidia kupata mapato ya haki na kudhibiti utoroshaji wa madini nje ya mfumo rasmi. Tuna masoko 43 nchi nzima na Vituo vya Ununuzi 109.

19. Mahusiano ya Kimataifa (MoUs) – Wizara ya Madini imesaini mikataba ya ushirikiano na nchi mbalimbali ikiwemo Uingereza (UK), Sweden, Finland na nyingine nyingi kwa ajili ya kukuza ujuzi, teknolojia na kupata mitaji kwa ajili ya maendeleo ya sekta kwa manufaa ya taifa.






Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...