CHAMA cha waandishi wa habari mkoa wa Mara(MRPC), Kimefanya Maadhimisho ya siku wa Uhuru wa vyombo vya habari mei 23 mwaka 2025, Kwa kuzingatia kauli mbiu ya mwaka huu kwa lengo la maendeleo ya tasnia ya habari.
Akifungua maadhimisho hayo, mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Tarime Meja Edward Gowele alitoa wito kwa waandishi hao kuwa wazalendo, kwa kutathmini kazi zao, huku akiweka mkazo juu ya uweledi na ufanisi wa kalamu wanazotumia kuwa zinaweza kujenga au kubomoa jamii.
"Tunataka maendeleo makubwa ya vyombo vya habari, kwa hiyo tuitumie hii siku kujitafakari fanyeni tathmini ya kazi zenu kwa mwaka uliopita ili kubaini mapungufu na changamoto ili kwamba muweze kuongeza ufanisi wa kazi zenu" alisema Gowele
Mwenyekiti wa chama hicho Jacob Mugini, amesema kuwa kauli mbiu hiyo kwa lugha ya kingereza "The impact of artificial intelligence on press freedom and media"kwa maana ya Mchango wa akili Mnemba kwa Uhuru wa vyombo vya habari, wakiwemo waandishi wa habari wenyewe inavyoweza kusaidia katika kuleta maendeleo kwa wanahabari na kwa jamii .
Uongozi wa chama hicho, ulifanikiwa kuteuwa baadhi ya wanachama wa MRPC walioshiriki na kupata mafunzo mbalimbali yanayohusu kauli mbiu hiyo na kutoa elimu ya Akili Mnemba kwa Waandishi wa habari walioshiriki Maadhimisho hayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa DimaOneline, Dina Maningo ni miongoni mwa waandishi wa habari walioshiriki semina za mafunzo ya (artificial intelligence ) kwa maana akili mnemba alitoa elimu juu ya umuhimu wa matumizi ya akili mnemba kwa waandishi hao wa habari.
" Kupitia akili mnemba, unaweza kubaini taarifa halisi na taarifa feki, Kuna kitu kinaitwa google lens kwenye simu janja na kimpyuta kutumia app iyo unaweza kubaini picha na eneo ya picha husika mahali ilipo,anaeleza frat ladder twenty for pia inaweza kuonesha taarifa za usafiri wa anga kama ikiwa hauna mawasiliano ya msemaji wa serikali" alisema.
Amesema kuwa akili mnemba inaweza pia kupotosha na kwa kupunguza ubunifu wa kibinadamu kwa mtumiaji husika jambo ambalo anasema pia akili mnemba inaweza kutengeneza nyaraka bandia huku akisisitiza umakini zaidi mwandishi wa habari au muhariri atakae tumi akili mnemba kwenye kazi zake kwani ina uwezo pia wa kutengeneza taarifa zamani na kuwa taarifa za kisasa.
Fresha Kinasa, pia ni mmoja wa waandishi wa habari walioteuliwa na MRPC kutoa elimu ya akili mnemba kupitia mada ya 'Usalama Mtandaoni' (Digital Security) alieleza kuwa usalama mtandaoni ni hali ya mwandishi wa habari, vifaa vyake vya kazi na ujumbe anaoutoa kwa jamii vyote kwa pamoja vinakuwa katika hali ya usalama.
" Mwandishi wa habari katika kazi zako taarifa unazotoa kwa umma hakikisha ziko salama kwa maana ya wewe binafsi, vifaa vyako vya kazi kama kamera, simu na kompyuta vinakuwa salama endapo kompyuta yako haina usalama ni rahisi mtu kuiba taarifa zako" Anasema Kinasa.
Amesema ili mwandishi wa habari na vifaa vyake vya kazi kuwa salama kwanza anapaswa kutopenda kuchangia nywila (password) na mtu mwingine hata kwa mtua anayemfahamu, pia kuacha tabia ya kujihusisha na (Wi-Fi), kwakufanya hayo taarifa,habari huweza kudukuliwa.
Mwandishi wa Jambo Tv Helena Magabe, alieleza mafunzo aliyoshiriki yalikuwa yanahusu uandishi wa habari za uchuguzi, kwa kuzingatia serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inatarajia kufanya uchaguzi mkuu utakaohusisha madiwani, wabunge na Rais.
Helena aliwaeleza wanachama na wasiowanachama wa MRPC katika kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika octoba,2025, Mwandishi wa habari haruhusiwi kuajiriwa na mgombea kwa kufanya hivyo atapaswa kuacha kazi ya uandishi wa habari.
"Tumetakiwa kupitia tena sheria zilizotungwa mwaka 2024 na kanuni za mwaka 2025 zilizotungwa mwaka 1977, Sambamba na hilo kipindi cha uchaguzi tunapaswa kujali usalama wetu kwa maana ukihisi upotevu wa amani eneo la tukio chukua tahadhari kwa kuondoka haraka eneo hilo" Anasema Helena.
Maadhimisho hufanyika Mei 3 duniani Kitaifa yalifanyika mwishoni mwa mwezi uliopita Mkoani Arusha ambapo Mgeni rasmi alikuwa ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, huku kauli mbiu ikiwa ni" The impact of artificial intelligence on press freedom and media' (Mchango wa akili mnemba kwa uhuru wa vyombo vya habari, Matumizi ya teknolojia hiyo kwa waandishi wa habari katiaka kuleta Maendeleo ya ukuaji wa sekta ya habari)
































Comments
Post a Comment