Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Wanawake Wachangia 35% ya Pato la Taifa


 

📌 Dkt. Biteko afungua Mkutano wa TAWiFA

📌 Dkt. Biteko awataka wanawake kuwekeza katika teknolojia kufikisha huduma vijijini

📌 Uwekezaji kwa wanawake si hisani ni kimkakati kwa maendeleo ya Taifa


Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Wanawake nchini Tanzania wametajwa kuwa na mchango mkubwa katika Pato la Taifa ambapo takwimu zinaonesha kuwa asilimia 35 ya uchumi wa Tanzania unatokana na juhudi za wanawake ambao wanachangia asilimia 70 ya nguvu kazi ya kilimo ni wanawake hasa katika mazao ya chakula.

Mchango wa mwingine wa wanawake unajidhihirisha katika biashara, viwandani na katika huduma za kifedha kupitia utafiti uliofanywa na Chama cha Mabenki Tanzania (TBA) mwa ka 2022 umeonesha wanawake ni 47% ya wafanyakazi wote wa sekta ya fedha. Pia wanashika 10% ya nafasi za kufanya maamuzi. Vile vile, 18% wakiwa wajumbe katika bodi za wakurugenzi sawa na wastani wa wanawake wawili katika kila bodi.

Hayo yamebainishwa leo Aprili 14, 2025 jijini Dodoma na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko wakati aliposhiriki katika ufunguzi wa Mkutano wa mwaka wa Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha (TAWiFA).

Pamoja na mafaniko hayo, Dkt. Biteko ametaja changamoto zinawakabili wanawake katika sekta ya fedha kuwa ni uhaba wa upatikanaji wa mikopo yenye riba nafuu, elimu duni ya masuala ya kifedha na uchache wa nafasi za kushiriki katika maamuzi ya Sera za Fedha.

Amewataka wanawake nchini kuzingatia misingi ya malezi kwa watoto wao kwa kuwapa nafasi sawa watoto wa kike na wa kiume ili kukabili changamoto zinazotokana na mila, desturi utamaduni.

“ Kwa kushirikiana na wadau wengine Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe.  Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuchukua hatua za makusudi ili kutatua changamoto zinazomkabili mwanamke na hivyo kuchochea maendeleo" amesema Dkt. Biteko.

Amebainisha baadhi ya hatua hizo kuwa  ni kuwaamini na kuwapa wanawake nafasi za juu za uongozi na maamuzi, kufanya Mapitio na Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Jinsia na Maendeleo ya Wanawake ya mwaka 2000,  kuandaa miongozo mbalimbali ikiwemo  Mwongozo wa Ulinzi na Usalama wa Wanawake na Vijana Vyuoni uliozinduliwa mwaka 2023 na kutoa fursa nyingine mbalimbali za kifedha na kiuchumi kwa wanawake.

Amesisitiza kuwa wanawake wanatakiwa kuwekeza zaidi katika mifumo ya kidigitali ili kuendana na mabadiliko ya kidigitali "Naomba hapa nitoe rai kwenu kuwa, mkiwa mnaendelea kutekeleza majukumu yenu, msisahau kuhusu kuwekeza katika teknolojia. Maana Dunia ya sasa inazidi kwenda zaidi katika maisha ya kidigitali. Hii itasaidia kurahisisha biashara na kufikisha huduma kwa wepesi hususan katika maeneo ya vijijini,”

Fauka ya hayo, Dkt. Biteko amesema kupitia mijadala na maazimio yatakayotolewa katika mkutano huo, zitapatikana  mbinu mpya za kuongeza ushiriki wa wanawake katika sekta ya fedha na uchumi wa nchi kwa ujumla kupitia mabenki, kampuni za bima, masoko ya mitaji. Pamoja na mbinu na njia mbalimbali za fedha mtandao zinazotatua changamoto zinazomkabili mwanamke katika sekta ya fedha.

Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha, Mhe. Hamad Chande amewapongeza wanawake nchini kwa kuanzisha Chama hicho kinacholenga kusaidia wanawake kiuchumi. 

Amewahakikishia kuwa Serikali imeandaa mazingira rafiki kwa wanawake katika ukuzaji wa uchumi “ Serikali imeweka mazingira wezeshi kwa kutunga sera na sheria za kiuchumi ili wanawake na makundi mbalimbali yaweze kuimarika kupitia taasisi na vyama kama hivi. Aidha, Serikali itaendelea kushirikiana nanyi ili kuimarisha TAWiFA ili kuhakikisha nafasi ya mwanamke inazidi kuwa juu katika jamii.”

Rais wa Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha (TAWiFA), Fikira Ntomola amesema kuwa wanawake nchini wameendelea kujishughulisha ili kuhakikisha sekta ya fedha nchini inakuwa. Aidha, jamii inapaswa itambue uwekezaji kwa wanawake si hisani bali ni uwekezaji wa kimkakati kwa maendeleo ya Taifa.

“ Tunaahidi kufikisha elimu ya fedha kwa wanawake katika maeneo mbalimbali nchini kwa kuandaa mafunzo na warsha kwa lengo la kuongeza uwezo wa kusimamia masuala yao ya fedha na biashara,” amesema Bi. Ntomola.

Ameongeza kuwa TAWiFA imedhamiria kuleta mabadiliko chanya kuhusu ushiriki wa wanawake katika sekta ya fedha, aidha wameishukuru Serikali kwa kuendelea kuweka sera na sheria zinazochochea uchumi jumuishi  na uwepo wa usawa wa kijinsia kiuchumi na kijamii.

“Tumekuwa tukiwajengea uwezo wanawake wa kuendesha biashara zao kiufanisi, kukuza biashara zao na kupanua  wigo wao kuhusu sekta ya fedha,” amebainisha Bi. Ntomola.

Amewaomba wadau mbalimbali nchini kufungua milango ya fursa kwa wanawake, na kuwa TAWiFA ipo tayari kushirikiana nao kwa ajili ya kutoa elimu ya fedha kwa umma, pamoja na tafiti za kuendeleza miradi ya kusaidia wanawake ili kujenga sekta ya fedha iliyo jumuishi.

Makamu wa Rais wa Chama cha Wanawake katika Sekta ya Fedha (TAWIFA), Nangi Massawe amesema kuwa Chama hicho kinakutanisha wanawake katika sekta ya fedha ili kujenga sekta yenye usawa kwa manufaa ya Taifa.

TAWiFA kina jumla ya wanachama 204 na kimeendelea kuhakikisha wanawake wanashiriki katika sekta hiyo ili kuchochea maendeleo.





Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...